Posts

Showing posts from January 2, 2014

BINTI ANALAZIMISHA NDOA ANATAKA KUNISAIDIA KUTOA MAHARI...NAOMBA USHAURI JAMANI

Image
... Awali ya yote nina mwanamke mmoja ambaye tulianza naye mapenzi toka tuanze wote kazi kwa sababu tumeajiliwa sehemu moja ila tu tunatofautiana sehemu ya kufanyia kazi yeye anafanyia wilayani na mimi nafanyia mkoani sasa toka tuanze imefika kipindi akabeba ujauzito na saizi ni miezi mitano tangu abebe huo ujauzito sasa anataka nikatoe mahali kwao ili wanitambue wazazi wake rasmi yeye ndio mpanga mahali na anasema ni milioni moja mahali pamoja na masufuria ya shangazi na babu na branket la bibi. Mimi nikamwambia kuwa hicho kiasi sina akasema kuwa yeye atoe laki nne na mimi nimalizie laki sita na leo kanipigia simu kuwa inatakiwa ipelekwe barua ya kishika uchumba pamoja na elfu therathini mimi pia nikasema kuwa saizi sina hela yeye akasema kuwa mimi niandike barua atakuja kuichukua na ataituma nyumbani kwao kwa njia ya posta na ataiweka hiyo elfu therethini na kuituma nyumbani sasa ninachojiuliza ataka tuoane mapema ili amiliki baadhi ya vitu vyangu

AVUA NGUO BAADA YA KUMFUMANIA SHEMEJI YAKE

Image
AMA kweli dunia uwanja wa fujo! Mrembo aliyetajwa kwa jina la Baby amefanya kituko cha aina yake kwa kusaula nguo mbele ya hadhara baada ya shemeji yake maarufu kwa jina la Baba K kufumaniwa. FUMANIZI LAIVU Tukio hilo la aina yake lililovuta wengi lilijiri kwenye gesti moja (jina tunalo), maeneo ya Temeke jijini Dar hivi karibuni baada ya jamaa mmoja kumwekea mtego rafiki yake aliyekuwa akimtongoza mkewe na kumfumania laivu. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, mara baada ya fumanizi hilo, mrembo huyo ambaye ni shemeji wa mwanaume aliyefumaniwa alionesha maajabu alipoamua kuvua nguo bila kusitasita. “Alianza kuvua kidogokidogo, baadaye akaamua kuvua zote na kubakia na nguo ya ndani tu. Kwa kweli iliwashangaza wengi pale kwenye eneo la fumanizi. Halafu unajua fumanizi lenyewe lilikuwa ndani ya chumba, dada yake alikuwa huko, yeye nje,” alisema mmoja wa mashuhuda. Imeelezwa kuwa, baada ya mwanamke huyo kuvua nguo  alianza kushangilia kwa nguvu huku akirukaruka kwa f

SUPER STAR RAY C SASA AONYESHA MJENGO WAKE LIVE!!

Image
  Mwaka 2013 umekuwa wa mafanikio makubwa kwa Rehema Chalamila aka Ray C. Kubwa anamloshukuru Mungu ni kuokolewa kutoka kwenye maangamizi yaliyosababishwa na kuathirika na matumizi ya madawa ya kulevya, thanks kwa Rais Jakaya Kikwete aliyeamua kugharamikia matibabu yake. Baada ya matibabu hayo, muimbaji huyo wa ‘Niwe Nawe Milele’ amerejea kwenye afya yake ya kawaida na sasa yupo busy kurekodi nyimbo mpya na huenda mapema mwaka 2014 akarejea kwa kishindo. Pamoja na kupewa gari nzuri ya kutembelea, Ray C ameionyesha nyumba yaka anayoijenga na iliyokamilika kwa asilimia kubwa huku ikifanyiwa upambaji wa ndani tu. Ray C ameionesha nyumba yake kwenye Instagram kwa kuandika: Love the color of ma new house!!!! Under construction #godisgood#workhardplayhard."

Mwanajeshi aua vijana wawili kwa bastola

Image
  Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), ambaye jina lake limehifadhiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kuwaua kwa kuwapiga risasi vijana wawili na kisha kuwajeruhi vibaya wengine wawili walipokuwa katika shamrashamra za kuukaribisha mwaka mpya. Tukio hilo lilitokea majira ya saa sita na robo usiku wa kuamkia jana, katika eneo la Pugu Kinyamwezi, Ilala jijini Dar es Salaam. Akizungumza na NIPASHE jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Marietha Minangi (pichani) alisema tukio hilo lilitokea baada kundi la vijana waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya kuzingira gari la mwanajeshi huyo aliyekuwa akielekea nyumbani kwake Pugu Kinyamwezi, akitokea katikati ya Jiji kwa shughuli zake. Alisema mwanajeshi huyo alikuwa na gari aina ya Toyota Rava 4 na baada ya kufika katika eneo hilo alizingirwa na kundi la vijana hao waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya na ndipo aliamua kutoa bastola yake na kufyatua risasi ambapo iliwapata vijana hao na kufa papo

HAWA WALIAMUA KUURIBISHA MWAKA KIPEKEE KWA KUNGONOKA MWANZO MWISHO ... HIVI NDIVYO WALIVYOUKARIBISHA MWAKA

Image
Ndani ya chumba kimoja walinaswa wasichana wakiwa nusu uchi na wavulana wao, huku waki subiri mwaka mpya kwenye. Inasemekana ni wanafunzi wa moja ya vyuo vikuu. Add caption

BREAKING NEWS:BOMU LAPATIKANA LIKIWA ARDHINI SHEKILANGO

Image
BOMU LAONEKANA MAKUTANO YA BARABARA ZA MOROGORO NA SHEKILANGO LIMEJICHIMBIA ARDHINI MAENEO HAYO HIVI SASA .  POLISI WAMESHAFIKA MAENEO HAYO NA WAKO TAYARI KWA HATUA ZAIDI... BARABARA ZIMEFUNGWA SOURCE; RADIO ONE..

VISA VYA AUNTY EZEKIEL NA MUMEWE HIVI HAPA ... FULL DATA IMO HAPA

Image
STAA wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel amekiri mumewe kukamatwa na kupata misukosuko lakini si kufungwa kama baadhi ya watu wanavyoeneza uzushi. Aunt Ezekiel. Akipiga stori na mwandishi wetu hivi karibuni, Aunt alisema mumewe, Sunday Demonte alikamatwa kutokana na viza yake kuisha ambapo alishikiliwa kwa muda na alipokamilisha taratibu za ‘kurinyuu’, aliachiwa. “Nashangaa sana mambo haya yamevuma kuwa mimi nimemuacha mume wangu amefungwa, ukweli ni kwamba mume wangu yuko huru na hata sasa ukitaka ongea naye, ni mwanamke gani atakuwa na furaha hivi wakati mumewe ana matatizo?” alihoji Aunt. Aunt akiwa na mumewe. Katika mistari mingine, Aunt alisema watu wengi wanatamani kuona ameachika au kujua mwenendo wa maisha yake na mumewe lakini wanajidanganya kwani yeye ni mwanamke aliyeamua kuolewa na amefundwa hivyo wataambulia patupu. “Siyo  rahisi mimi kutoa siri ya maisha ninayoishi na mume wangu, ni makubaliano yetu. Kimsingi ndoa yetu iko imara, watasubiri s

DINA MARIOS APIGWA MIMBA NA RUBEN "NCHA KALI" ... DINA MARIOS AANIKA LIVE KILA KITU KUHUSU MAHABATI YAO

Image
  Dina Marios na Ruben Ndege ‘Ncha Kali’. SIYO siri tena! Uhusiano wa kimapenzi kati ya watangazaji nyota Bongo, Dina Marios na Ruben Ndege ‘Ncha Kali’ sasa upo hadharani. Kwa muda mrefu Dina na Ruben wamekuwa kwenye uhusiano lakini wamekuwa wakijitahidi kuuficha usijulikane na watu, lakini hata hivyo watu wa karibu hasa wanaofanya nao kazi, walifahamu juu ya uhusiano huo. Akizungumza katika Kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na Radio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Ijumaa iliyopita kwa mara ya kwanza Dina alifunguka kuhusu kuwa na uhusiano na Ruben huku akiweka wazi kuwa ana mimba yake. “Ni kweli baba mtarajiwa wa mtoto wangu ni Ruben Ndege ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Skylight Band. Wengi hapa kazini mnajua kuwa tulianza naye mbali. Kulikuwa na kupanda na kushuka, mara kwa mara lakini nashukuru sasa uhusiano wetu umeimarika,” alisema Dina. Alisema, katika muda aliokuwa katika uhusiano na Ruben, kuna wakati walikuwa wakiac

BABY MADAHA AZIDI KUMWANDAMA DIAMOND

Image
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha ‘amemshika uchawi’ msanii mwenzake, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kufuatia madai kuwa, kuna msanii maarufu Bongo alikwenda kwa mganga wa kienyeji Tanga akitaka kumfanyizia ‘madongoloji’ mrembo huyo ili mambo yake yaende ndivyo sivyo. Baby Joseph Madaha. ILIKUWAJE KWANI? Desemba 22, mwaka jana, mtu mmoja aliyedai ni sangoma aishiye Tanga mjini alituma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kupitia simu ya chumba cha habari Global akiomba namba ya Baby Madaha. Mtu huyo alisema anaomba namba hiyo kwa sababu kuna mtu alikwenda kwake (Tanga) akitaka amfanyizie Baby Madaha mambo yaende kombo. Nasibu Abdul ‘Diamond’. NAMBA YA BABY MADAHA YARUSHWA Baada ya meseji hiyo kusomwa, mtu huyo alirushiwa namba ya Baby Madaha kisha ujumbe wake ukafowadiwa kwa mrembo huyo. BABY MADAHA AENDA HEWANI Dakika tano baada ya Madaha kufowadiwa ujumbe huo, alikwenda hewani kwa simu iliyomtumia ujumbe ambapo bila salamu alisema: “Huyo atakuwa Diamond tu

BONY MWAITEGE AFANYA KWELI TAMASHA LA KRISMAS DODOMA

Image
Mwimbaji wa muziki wa injili nchini Bony Mwaitege akiimbisha mashabiki wake kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma wakati akiimba kwenye tamasha la Krismas lililofanyika leo na kushirikisha waimbaji wa muziki wa injili kutoka maeneo mbalimbali nchini  Tanzania , Tamasha hilo linaandaliwa na kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es salaam na tamasha la leo lilikuwa linahitimisha ziara ya mikoa minne ya Tanzania ambako matamasha hayo yamefanyika ambayo ni Dar es salaam, Morogoro, Tanga, Arusha na tamasha la  leo mjini Dodoma.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DODOMA) Mwimbaji wa muziki wa injili nchini Bony Mwaitege akisalimiana na mashabiki wake wakati alipokuwa akiimba kwenye uwanja waJamhuri Mjini Dodoma leo. Mgeni rasmi Mbunge wa jimbo la Tarime na Mwandishi wa vitabu Nyambari Nyangwine akitoa neno kwa mashabiki  waliohudhuria kwenye tamasha la Krismas kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma, kulia ni Alex Msama Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion. aadhi ya mas