Posts

Showing posts from February 28, 2018

Linah asema hufanya kusudi kuwapagawisha vidume awapo jukwaani

Image
Msanii wa Bongo Fleva Linah Sanga maarufu kama 'Ndege Mnana' amefunguka na kuweka wazi kuwa huwa anafanya makusudi kuvaa nguo za nusu utupu 'fupi' akiwa kwenye show ili aweze kuwapagawisha watoto wa kiume walioko katika tamasha ambalo anashiriki. Linah amebainisha hayo wakati akizungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia ukurasa wa kijamii facebook wa EATV kila Jumatano kuanzia majira ya saa 8:00 mchana hadi 10:00 alasiri kwa saa za Afrika Mashariki na Kati. "Mashabiki zangu wengi ni watoto wa kiume hivyo wakiona vichuchu vimesimama wanapata raha sana, muda mwingine nawatega kwa mavazi kwenye 'show' ili waburudike hivyo siwezi kubadili mavazi yangu kwa sababu mimi ni msanii ila ikitokea natakiwa kwenda sehemu ya kuvaa mavazi marefu ntafanya sina jinsi", amesema Linah. Kwa upande mwingine, Ndege Mnana amesema wakati mwingine huwa anapata wakati mgumu kutokana na mavazi yake akiwa jukwaani kwani akimuuita

Linah Aanika Idadi ya Wanaume Aliyotembea Nao

Image
MWANADADA anayekimbiza kwenye muziki wa Bongo Fleva, Linah Sanga amefunguka na kutaja idadi ya wanaume ambao ametembea nao na kufaidi penzi lake tangu awe maarufu. “Kwa haraka haraka nishatoka kimapenzi na wanaume watano hivi toka hivi watu wamenifahamu kama Linah, sina idadi kubwa sana, japo siwezi kuwakumbuka wote wengine nimeshawasahau kabisa. Kuna watu wana idadi kubwa ya watu wametembea nao sema tu ni kwa sababu si wasanii, “ amesema Linah. Linah amesema hayo wakati akifanya mahojiano yake na EATV kwenye kipindi cha Kikaangoni na kuongeza kuwa idadi hiyo ya wanaume ni baada ya kupata jina, lakini aliyowahi kutoka nao kimapenzi kipindi cha nyuma kabla ya umaarufu hawakumbuki ila ni kati ya 10 au 15. Linah amesema anavutiwa kimahaba na wanaume wenye rangi ya ngozi nyeusi tofauti na wengine wanavyochagua watu wa kuwa nao katika mahusiano ya kimapenzi. “Mimi napenda wanaume weusi, warefu si unajua mimi mfupi (shoti), sipendi wanaume weupe japo nishawa

Treni ya abiria yapata ajali

Image
Treni ya kubeba abiria iliyokuwa safarini kutoka Dodoma kwenda Kigoma kupitia Tabora imepata ajali katika eneo la kijiji cha Mpeta, wilayani Uvinza kaskazini magharibi mwa Tanzania, taarifa zinasema. Watu watatu wamejeruhiwa Ajali hiyo imesababishwa na kichwa cha treni kuacha njia na mabehewa mawili kuanguka Kaimu meneja wa wamawasiliano wa Shirika la Reli la Tanzania (TRL) Mohamed Mapondela ameambia BBC kwamba watu watatu wamejeruhiwa. "Sababu ya ajali bado haijafahamika lakini, timu ya kutathmini ajali iko njiani kuelekea eneo la tukio," amesema. Ajali ilitokea majira ya saa saba na dakika hamsini mchana eneo la katikati ya stesheni ya Malagarasi na Uvinza. "Tathmini kamili ya ajali itatolewa pale ambapo mabehewa yatakuwa yameinuliwa." Bw Mapondela amesema eneo hilo si kwamba ni baya na halina historia ya kupata ajali yoyote ile, ndio maana ni vigumu kusema nini hasa kinaweza kuwa chanzo cha ajali.

TCRA yasitisha nyimbo zisizokuwa na maadili

Image
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania [TCRA] imepokea Orodha ya nyimbo zisizokuwa na maadili kutoka Baraza la Sanaa la Taifa [BASATA].

Kisutu: Yaliyojiri Kesi ya Tido Mahakamani Leo

Image
ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando,  amesomewa maelezo ya awali ya kesi ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Februari 28,2018 mbele ya Hakimu Mfawidhi, Victoria Nongwa. Tido  anayetetewa na wakili Ramadhani Maleta amekubali maelezo binafsi kwamba alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC mwaka 2006 hadi 2010,  alikuwa msimamizi wa shughuli za TBC japo si zote, pia amekubali kutoa maelezo kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kuwa alifikishwa mahakamani Januari 26, 2018. Tido anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya,  moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni. Anadaiwa pia  Juni 16, 2008 akiwa Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), akiwa Mkurugenzi Mkuu wa TBC kwa makusudi alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa kuendesha na kutangaza vipindi vya televisheni kati ya TBC na Channel 2 Group Corporation (BV1) bila kupit