Posts

Showing posts from January 6, 2016

Wema atumbua Mil.300

Image
Wema Sepetu ‘Madam’. Na Mwandishi Wetu WEMA Sepetu ‘Madam’ ni mashine ya kutafuna fedha! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia habari za mjini kumtaja staa huyo wa Bongo Movies kuwa ameteketeza takriban Sh. Mil. 300 za mbunge ambaye anadaiwa kuwa ndiye anayemweka mjini kwa sasa, Risasi Mchanganyiko limenasa ubuyu kamili. KUMBUKUMBU MUHIMU Wema na mbunge huyo (jina kapuni kwa sasa) wanadaiwa kuwa walianzisha uhusiano wa kimapenzi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana ambao matokeo yake yalimpa ushindi Dk. John Pombe Magufuli wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa Rais wa Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Inadaiwa uhusiano huo tayari umezaa matunda kwani mlimbwende huyo ni mjamzito. TUJIUNGE NA CHANZO Kwa mujibu wa chanzo makini, mara baada ya mrembo huyo asiyechuja Bongo kuwa ‘klozi’ na mbunge huyo kijana mwenye pesa ndefu katika kampeni hadi sasa, amemchuna mbunge huyo kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya matumizi na zawadi mbalimbali ali

TRA YAVUKA LENGO YAKUSANYA TRILIONI 1.4 KWA MWEZI

Image
  kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka Tanzania (TRA) (Katikati) Alphayo Kidata akisisitiza jambo wakati alipofanya mazungumzo na waandishi wa habari kuhusu taarifa za ukusanyaji wa mapato wa kila mwezi Kushoto ni Kaimu Kamishna wa Forodha Jocktan Kyamuhanga na kulia    ni Kaimu Kamishna wa Kodi za Ndani Yusufu Salum .   Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka Tanzania (TRA) (Katikati) Alphayo Kidata akizungumza na waandishi wa Habari wakati akitoa taarifa za ukusanyaji wa mapato wa kila mwezi. Picha Na raymond Mushumbusi MAELEZO   Jumla ya shilingi trilioni 1.4 imekusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi cha mwezi Desemba mwaka uliopita wa 2015. Kiasi hicho ni sawa na ongezeko la wastani wa shilingi  bilioni 490 kwa mwezi ukulinganisha na wastani wa makusanyo ya kuanzia Julai hadi Novemba ambapo ,TRA ilikuwa imekusanya wastani wa shilingi bilioni 900 kwa mwezi. Takwimu hizo zimetolewa leo jijini Dar es salaam na Kaimu Kamishna Mamlaka ya Mapato

BREAKING NEWZZ: MOTO WA WA RAIS MAGUFULI SASA KILA KONA WAWAKA WATUMISHI 9 WAMETIMULIWA KAZI LEO

Image
Watumishi 9 wakiwemo wakuu wa idara 7 wasimamishwa kazi kwa kuuza majengo ya serikali na kuisababishia hasara ya Sh milioni 9 Kigoma CHANZO: RADIO ONE

Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira afanya ziara makao makuu ya Vodacom Tanzania‏

Image
Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira,Mhe Anthony Mavunde (wapili toka kushoto) akikagua vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini vya mfanyakazi wa kigeni wa Vodacom Tanzania , Valentino Giron (kushoto),wakati alipofanya ziara ya kikazi Makoa makuu ya Vodacom Tanzania yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam hivi karibuni,Anayeshuhudia kulia ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo,Matina Nkurlu. Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira,Mhe Anthony Mavunde(Kulia) akisisitiza jambo kwa wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,wakati alipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam hivi karibuni kwa ajili ya kujua kero na maendeleo mbalimbali ya wafanyakazi wa kampuni hiyo. Naibu Waziri wa Kazi,Vijana na Ajira,Mhe Anthony Mavunde(Mwenye suti katikati)akimsikiliza Mkuu wa kitengo cha rasilimali watu wa Vodacom Tanzania, Conrad Msoma (kushoto) wakati alipotembelea makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam hivi karibuni kwa ajili

BREAKING NEWS : KIMENUKA IRINGA ASUBUHI,VIONGOZI WATUMBULIWA KWA UFISADI

Image
Waziri wa Kilimo, Uvuvi na Mifugo, Mwigulu Nchemba amewasimamisha kazi viongozi wa vyama vya msingi vya tumbaku mkoani Iringa wanaotuhumiwa kushiriki katika ufisadi wa mkopo wa matrekta tisa kupitia mgongo wa vyama vya msingi vya wakulima wa tumbaku na kujimilikisha wenyewe. Nchemba alifikia hatua hiyo jana baada ya wakulima wa tumbaku kulalamikia viongozi wa vyama hivyo na kuwataka wakabidhi ofisi. Awali, mwanachama wa Chama cha Msingi cha Mfyome, Francis Kilatu alisema Benki ya CRDB inawakata fedha zao huku wamiliki wa matrekta hayo wakiwa ni wengine hivyo alimuomba waziri kulishughulikia mara moja.

BREAKING NEWS : WAZIRI MKUU AWATUMBUA VIONGOZI WENGINE RUVUMA,MOTO WAWAKA KILA KONA

Image
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea kiwanda cha kusindika tumbaku cha mkoani Ruvuma na kuwasimamisha kazi viongozi wa  Chama Cha Kikuu Cha Ushirika cha SONAMCU. Akizungumza jana jioni(Jumanne, Januari 5, 2016), katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu Ndogo ya Songea, wakati alipokutana na wakulima wa zao la tumbaku wa Wilaya ya Namtumbo, Wananchama wa Vyama Vya Ushirika vya Mkoa wa Ruvuma, viongozi wa Mkoa pamoja na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Edwin Ngonyani ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini. Waziri Mkuu amesema, Serikali ina dhamira ya kufufua kiwanda cha kusindika tumbaku cha SONAMCU, na lengo la kutembelea kiwanda hicho ni katika utekelezaji wa agizo la Rais John Pombe Magufuli la kufufua viwanda nchini. Waziri Mkuu Majaliwa, ametembelea maeneno mbalimbali ya kiwanda hicho na kukagua mitambo iliyokua ikitumika kusindika tumbaku, kabla kiwanda hicho kuzimwa miaka kadhaa iliyopita baada ya kukosa malighafi za kuend

Rais Obama Adondosha Chozi Hadharani Akitetea Hoja

Image
Rais Barack Obama akitokwa. Rais Barack Obama alitokwa na machozi jana alipokuwa akitetea kufanyiwa mabadiliko kwa sheria za udhibiti wa silaha nchini Marekani ili kupunguza idadi ya watu wanaoshambuliwa na kuuawa kwa risasi nchini humo. Obama aliwaambia Wamarekani kwamba mageuzi anayoyatete  ni kwa manufaa yao wenyewe kwa kuwa yeye huu ni mwaka wake wa mwisho kukaa madarakani na wala hana mpango wa kugombea tena. Rais Obama anataka watu wote wanaouza silaha washurutishwe kuwapekua na kuchunguza historia ya watu wanaowauzia silaha. Kwa sasa, sheria hiyo hugusa tu wauzaji silaha waliosajiliwa. Wauza silaha ambao hawajasajiliwa, hutakiwa kuwauliza tu wateja wao iwapo wamewahi kupatikana na makosa ya uhalifu au kama wana matatizo ya kiakili. Hatua hiyo ya Rais Obama imepingwa vikali na baadhi ya viongozi wakuu wa chama cha Republican wanaosema inaingilia uhuru wa kikatiba wa Wamarekani.