Posts

Showing posts from September 28, 2016

Rais Magufuli: Tumejipanga Kununua Ndege Mpya Kubwa Mbili

Image
Ndege mbili aina ya Bomberdia zilizozinduliwa jijini Dar es Salaam leo. Vikundi vya ngoma vikitumbuiza katika uzinduzi wa ndege mbili  aina ya Bomberdia jijini Dar es Salaam leo RAIS John Magufuli amesema serikali yake imejipanga kununua ndege nyingine mbili ambapo moja itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 160 na nyingine abiria 242. Hayo ameyasema leo wakati akizindua  ndege mbili za serikali kwenye hafla iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere uliopo jijini Dar es Saalam. Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mama Janeth Magufuli; Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Profesa Makame Mbawara; Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam Paul Makonda;  Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Saalam Isaya Mwita na viongozi wengine mbalimbali. Vilevile rais aliwananga watu wote wanaobeza ununuzi wa ndege hizo na kuziita zina kasi ndogo ya Bajaj akawataka wawe na moyo wa kupenda vitu vyao wenyewe. Pia amewahakikishia Watanzania kwa ujumla kwamba ndege hizo ni mpy

AUNTEZEKEL AFUNGUKA KUHUSU : WEMA SEPETU ATAJIJUA KISA KUWA KARIBU NA ZARI

Image
  KAMA ni noma na iwe noma! Mwigizaji Aunt Ezekiel amesema kama kitendo cha yeye kuwa karibu na mpenzi wa Nasibu Abdul ‘Diamond’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kama kitapokelewa vibaya na shosti wake muigizaji Wema Sepetu ‘Madam’, hatajali, atajijua mwenyewe maana hana jinsi. Kauli hiyo imekuja ikiwa ni baada ya Aunt kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya mpenzi huyo wa Diamond, iliyofanyika visiwani Zanzibar na picha za Aunt akiwa ameshikilia tumbo la Zari kuvuja mitandaoni. Baada ya picha hizo kuvuja, watu mbalimbali walianza kuchangia kwenye mitandao ya kijamii kwa kusema kitendo hicho hakitamfurahisha Madam huku wengine wakimpongeza Aunt kwa kuonesha anamsapoti kwanza ‘ubavu’ wake halafu marafiki baadaye. Mara baada ya kuona maoni hayo mitandaoni, R i s a s i Mchanganyiko, lilimvutia waya Aunt na kutaka k u m u u l i z a k w a m b a haoni kitendo hicho kinaweza k u p o k e l e w a tofauti na Madam ndipo mrembo huyo alipofunguka: “Mim

Mahakama Kuu Yaikana Kampuni Iliyomtoa Mbowe

Image
Vitu vya Mbowe baada ya kutolewa nje na Kampuni ya Fosters Auctioneers and General Traders kwenye jengo la Shirika la Taifa la Nyumba (NHC). Mahakama Kuu imekana kuitambua kampuni ya Fosters Auctioneers and General Traders iliyohusika kuondoa vitu vya kampuni za Freeman Mbowe kwenye jengo la Shirika la Taifa la Nyumba (NHC). Hayo yalibainishwa jana na kiongozi wa jopo la mawakili wanaomtetea Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti wa Chadema, Peter Kibatala wakati wa usikilizwaji wa maombi yaliyofunguliwa na mlalamikaji huyo kupitia kampuni ya Mbowe Hotels Ltd dhidi ya NHC na kampuni hiyo ya udalali. Wakati wa usikilizwaji wa maombi hayo jana, pamoja na mambo mengine Mbowe aliiomba Mahakama iliamuru NHC na kampuni hiyo wamrejeshe katika jengo hilo pamoja na vifaa na mali zake zinazoshikiliwa na kampuni hiyo. Wakili Kibatala aliieleza Mahakama kuwa mteja wake aliondolewa katika jengo hilo kinyume na sheria. Alidai dalali aliyetumiwa na NHC kuziondoa kampuni za Mb

RC Makonda Amshukuru Wolper

Image
Picha inayomuonesha Wolper akiwa amevaa fulana hiyo. DAR ES SAALAM: Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam, mheshimiwa Paul Makonda amemshukuru mwanadada Jaqueline Massawe ‘Wolper’ ambaye ni muigizaji anayefanya vizuri kwenye tansia ya Bongo Muvi nchini. Mkuu huyo wa Mkoa amemshukuru muigizaji huyo kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya Wolper kuweka picha kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa amevaa fulana nyeupe yenye ujumbe wa kuhamasisha kampeni ya upandaji miti jijini Dar es Saalam itakayofanyika Oktoba Mosi, 2016. Kampeni hiyo inayokwenda kwa jina la ‘Mti Wangu’ inasimamiwa na Mkuu wa Mkoa mh. Paul Makonda. Mkuu wa Mkoa ameandika ujumbe huu kwenye akaunti hiyo unaosomeka: “Huwezi kujuwa umeugusa Kwa kiasi gani moyo wangu. Wewe na watu wote wanao support campaign ya MTI WANGU. Niwashukuru sana sana. “Endeleeni kuiunga Mkono serikali kwani miti tunayoipanda inafaida kubwa sana kwetu sisi Wananchi.”

Deni La Bil. 7 Lamziba Mdomo Madam Rita.

Image
Mjasiriamali, Ritha Paulsen ‘Madam Rita’. Na Mwandishi Wetu, RISASI mchanganyiko DAR ES SALAAM: Habari zilizozagaa wiki iliyopita kuhusu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuidai shilingi bilioni 7 Kampuni ya Benchmark Production inayomilikiwa na mjasiriamali, Ritha Paulsen ‘Madam Rita’, zimesababisha mwanamama huyo kuziba mdomo wake kwa kukataa kuzungumzia sakata hilo. Ritha Paulsen ‘Madam Rita’ akiwa katika pozi. Gazeti hili lilimtafuta mdau huyo mkubwa wa burudani ambaye pia huendesha shindano la kila mwaka la Bongo Star Search (BSS) kutaka kusikia maoni yake kuhusiana na habari hizo zilizotikisa wiki iliyopita, lakini akawa na jibu fupi; “No comment kwa sasa, nitatoa taarifa hivi karibuni juu ya jambo hilo, lakini siyo leo, muda muafaka ukifika nitafanya hivyo,” alisema Madam Rita. Wiki iliyopita, TRA ilitoa muda wa siku 14 kwa kampuni hiyo kuwa imelipa deni hilo linalotajwa kuwa ni la kuanzia mwaka 2009, kupitia kwa meneja msaidizi wa madeni wa mamlaka