Posts

Showing posts from April 22, 2017

Ngoma, Bossou kuikosa Prisons

Image
MSHAMBULIAJI Donald Ngoma na Vincent Bossou watakosekana katika kikosi cha Yanga kinachotarajiwa kuivaa Tanzania Prisons kutoka Mbeya katika mechi ya hatua ya ya robo ya fainali ya mashindano ya Kombe la FA itakayofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Akizungumza na gazeti hili jana, Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi, alisema kuwa maandalizi ya mchezo huo yamekamilika na wataingia uwanjani huku wakiwaheshimu wapinzani wao kutokana na uzoefu waliokuwa nao kwenye ligi na mashindano mbalimbali. Mwambusi alisema kuwa wamejiandaa na ushindani na changamoto kutoka kwa Prisons ambayo wachezaji wake wamekaa pamoja muda mrefu. 'Hatutawadharau Prisons, mpira hauna historia, tusubiri tuone dakika 90, ila tutamkosa Vincent ambaye ni mgonjwa aliumia jana (juzi) na leo (jana) amekwenda hospitali, Ngoma ndio hatokuwapo kabisa, aliumia tangu tulipokuwa safarii, tunasema mchezo wa kesho utakuwa mgumu zaidi, " alisema Mwambusi. Aliongeza kuw

Gabo Afunguka Kuonja Penzi la Wema Sepetu

Image
  Staa wa Bongo Movie, Salim Ahmed ‘Gambo’ na Madame Wema Sepetu KUFUATIA uwepo wa madai kuwa amelionja penzi la mwigizaji Wema Sepetu, mkali anayekimbiza kwa sasa katika soko la sinema kwa Bongo, Salim Ahmed ‘Gambo’ amebanwa na Risasi na kufungukia uhusiano wake na Wema Sepetu. Awali, mwanahabari wetu alihakikishiwa na msanii mmoja (jina tunalihifadhi) kuwa kabla ya kuvuja kwa picha za sinema za Wema na Gabo za filamu hivi karibuni, wawili hao waliwahi kuanguka dhambini miaka kadhaa iliyopita. “Kwani unafiri ukaribu wa Wema na Gabo ni filamu tu? Kuna zaidi ya filamu, walishawahi kutoka miaka ya nyuma na ndio maana umeona hivi karibuni imekuwa rahisi tu kwao kufanya tena kazi pamoja,” alisema msanii huyo. Baada ya kupata ubuyu huo, mwanahabari wetu alimtafuta Wema ili kuweza kumsikia anazungumziaje ishu hiyoi lakini bahati mbaya mrembo huyo hakuweza kupokea simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, pia hakujibu. Alipoulizwa Gabo kuhusiana na madai hayo, alisem

Watumishi 52,436 kuajiriwa

Image
SERIKALI inakusudia kuajiri watumishi wapya wa umma 52,436 katika mwaka ujao wa fedha. Aidha, madaktari wapya 258 waliokuwa waende kufanya kazi nchini Kenya, lakini wakakwama kutokana na kuwekewa pingamizi la kimahakama na wenzao wao huko na hivyo Rais, Dk John Magufuli kuamuru waajiriwe mara moja nchini, watarajiwa kuanza kazi keshokutwa Jumatatu. Hayo yalisemwa bungeni juzi usiku na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki alipokuwa anatoa ufafanuzi wa lini Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada nyingine, kama ilivyoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Lupembe (CCM). “Azma ya serikali, kwanza kabisa hatuwezi kuajiri wananchi wote, tumekuwa tukisikia hapa wahitimu hawana ajira, wengine wanaendesha bodaboda… tunapopanga idadi ya watumishi wa kuajiriwa, tunaangalia mambo mengi, kuanzia mahitaji, vipaumbele hadi uwezo wa kibajeti. “Tayari tumeshaanza kutoa vibali vya ajira zaidi

Atembezwa Nusu UCHI Na Kisha Kulazimishwa Kula Kinyesi kwa Kosa la Kumtukana Mama Yake

Image
Wanawake wa kijiji cha Kisungamile kilichopo katika Kata ya Matai wilayani Kalambo katika mkoa wa Rukwa wamemwadhibu Vitus Nyami (26) kwa kumtembeza nusu uchi na kulazimisha kula kinyesi cha ng’ombe kwa kosa la kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni. Aidha wanawake hao walitumia mfuko wa ‘salphate’ kufunika sehemu za siri za kijana huyo kisha wakaanza kumtembeza mitaani kijijini  humo huku wakiimba nyimbo za kabila la Kifipa wakilaani tabia ya kijana huyo ya kumtukana mama yake mzazi matusi ya nguoni kila kukicha . Walidai kukasirishwa na tabia ya kijana huyo wa kiume kumtukana mzazi wake wa kike matusi ya nguoni, hivyo walilazimika kumfunga kamba na kumtembeza mitaani kijijini humo akiwa nusu uchi. Mwenyekiti wa kijiji cha Kisungamile, Didas Musa alikiri kutokea kwa mkasa huo juzi ambapo mtuhumiwa huyo alitembezwa mitaani kwa saa sita kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 6:00 mchana. Akifafanua alisema kuwa licha ya adhabu hiyo ya kutem

Ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie

Image
1. CHOKOCHOKO Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano. Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa. Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani. Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye. Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali. Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala. 2. KUTORIDHIKA Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawar

Faida za kula parachichi kiafya

Image
Tunda hili lina virutubisho vingi na muhimu kwa afya zetu, na inaelezwa kuwa tunda hili huenda likawa ni mbadala wa vyakula kama nyama nyeupe kwa jinsi lilivyo na malighafi zote zilizo muhimu ndani yake. Zifuatazo ndizo faida  za tunda hili; Tunda hili linapotengenezwa kama kinywaji (juis) husaidia kuondoa maumivu ya tumbo na kuponya vidonda vya tumbo pamoja na kurekebisha udhaifu mwingine tumboni. Parachichi huweza kumpatia mtu uwezo mzuri wa kuona, huku majani yake yakielezwa kuongeza damu na kusheheni vitamin A, B, C na E. Parachichi linauwezo wa kukuza nywele kwa haraka zaidi na kuifanya ngozi ya mwili kuwa katika unyororo. Unachotakiwa kufanya ni; Hakikisha ya kwamba unakata vijipande vidogo vidogo kisha paka katika nywele zako au ngozi yako, acha baada ya dk kumi na tani kisha na nawa uso wako kwa maji ya uvuguvugu. Tunda hili husaidia wanawake katika kuifanya hedhi iende vizuri kila mw

Watumishi 52,436 kuajiriwa

Image
SERIKALI inakusudia kuajiri watumishi wapya wa umma 52,436 katika mwaka ujao wa fedha. Aidha, madaktari wapya 258 waliokuwa waende kufanya kazi nchini Kenya, lakini wakakwama kutokana na kuwekewa pingamizi la kimahakama na wenzao wao huko na hivyo Rais, Dk John Magufuli kuamuru waajiriwe mara moja nchini, watarajiwa kuanza kazi keshokutwa Jumatatu. Hayo yalisemwa bungeni juzi usiku na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki alipokuwa anatoa ufafanuzi wa lini Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa kada nyingine, kama ilivyoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Anna Lupembe (CCM). “Azma ya serikali, kwanza kabisa hatuwezi kuajiri wananchi wote, tumekuwa tukisikia hapa wahitimu hawana ajira, wengine wanaendesha bodaboda… tunapopanga idadi ya watumishi wa kuajiriwa, tunaangalia mambo mengi, kuanzia mahitaji, vipaumbele hadi uwezo wa kibajeti. “Tayari tumeshaanza kutoa vibali vya ajira zaidi