Posts

Showing posts from April 12, 2018

Zuckerberg Akiri Kosa Lake Na Kuomba Radhi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg. Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg ametoa maelezo katika Bunge la Marekani- Congress kwa mara ya kwanza Jumanne, akijibu wasiwasi ulioelezwa na wabunge juu ya kushindwa kwa mtandao wa jamii maarufu kulinda taarifa zao. Taarifa hizo za siri ni za watumiaji wanaofikia milioni 87 ulimwenguni zilizotumiwa na kampuni yenye kujishughulisha na siasa- Cambridge Analytica iliyokuwa na mafungamano na Trump. Mahojiano hayo yanaendelea Jumatano wakati Zuckerberg atakapokutana katika raundi ya pili kujibu maswali mbele ya jopo la Wabunge wa Marekani. Mkurugenzi huyo Mark Zuckerberg amekiri kuwa :”Hilo lilikuwa kosa kubwa na ni kosa langu mimi mwenyewe na naomba radhi. Nilianzisha matandao wa Facebook, niliusimamia na nina wajibika kwa kitu chochote kinachotokea.” Wachambuzi wanasema ni kosa ambalo liliruhusu kampuni ya kisiasa ya Cambridge Analytica kupata taarifa kwa kupitia programu iliyotengenezwa na k

JPM AMBADILISHA BODIGADI WAKE, AWAPANDISHA VYEO 28

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ameridhia na kuwapandisha vyeo maofisa 28 wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kuanzia leo Aprili 12, 2018 huku akimbadilisha Msaidizi wake Kanali Mbaraka Mkeremy ambaye amempandisha cheo na atapangiwa kazi nyingine jeshini. Aidha, Rais pia amekukubali kumpandisha cheo kutoka Luteni Kanali kuwa kanali D.P.M Murung a na kuwa mpambe wa Rais akichukua nafasi ya Kanali Mkeremy. Akitoa taarifa ya uteuzi huo, Mkuu wa Majeshi, Jenelari Venancy Mabeyo amesema maofisa walioteuliwa wanakwenda kuimarisha safu za utendaji kazi kijeshi na kwamba maofisa wote hao watavalishwa vyeo vyao Ijumaa hii katika makamo makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es salaam. Katika uteuzi huo Rais Magufuli amewapandisha vyeo maofisa wa ngazi mbalimbali Jeshini ikiwa ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma Kanali M E Gaguti ambaye sasa anapanda cheo na kuwa Brigedia Jenelari na kurejeshwa Jeshini.

ATCL Yaondolewa International Air Transport Association kwa Madeni

Image
SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL) limeondolewa katika Mfumo wa Malipo wa Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga (International Air Transport Association – IATA) kutokana na kukabiliwa na madeni na sasa iimetiliana saini ya makubaliano ya miaka mitano na Kampuni ya Ndege ya HAHN Air ili kuuza tiketi za Air Tanzania. Akizungumza na wanahabari Mjini Zanzibar, Mkurugenzi wa ATCL. Mhandisi Ladislaus Ernest Matindi, amesema wamelazimika kuingia kwenye makubalianao na kampuni hiyo ili wasikose baadhi ya huduma za malipo ya tiketi. “Tuna madeni, sikumbuki yalifikia kiasi gani lakini ni madeni makubwa ambayo yalilazimisha kusimamishwa uanachama au kufungiwa huduma hizi mpaka tutakapokuwa tumelipa hayo madeni. “Kubwa zaidi ilikuwa ni sisi kuwa katika mfumo wa Shirikisho wa Mashirika ya Ndege Dunia IATA ambayo ndiyo mfumo wa uuzaji na utawanyaji wa tiketi kwa kuwa mabadilishano ya pesa au kupeleka pesa kutoka shirika moja kwenda lingine hufanyika kwa kutumia huo

RAIS MAGUFULI AFUNGUKA ANAVYOIKUMBUKA SIKU YA MWISHO YA SOKOINE

Image
  IKIWA leo ni Kumbukumbu ya Kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine aliyefariki dunia Aprili 12, 1984 kwa ajali ya gari, eneo la Dakawa nje Kidogo ya Mji wa Morogoro, Rais Dkt. John Magufuli amefunguka na kueleza alivyomfahamu kiongozi huyo enzi za uhai wake na mchango wake katika Taifa letu. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli amesema; “Katika siku kama ya leo tarehe 12 Aprili 1984 nikiwa Mpwapwa JKT nikitumikia jeshi langu “Oparesheni Nguvukazi” tukatangaziwa kifo cha marehemu Edward Moringe Sokoine, ilikuwa siku ya majonzi shujaa huyu niliyemjua na kumshabikia ikawa siku yake ya mwisho.   “Wakati tunapoazimisha siku kama hii ya kifo chake, watanzania tuige mfano wake kwani alikuwa msema kweli, asiyeogopa, mpiga vita rushwa,ufisadi, unyonyaji,mzalendo wa kweli na aliyechukia rasilimali za watanzania kuibwa. “Marehem Sokoine hatasahaulika katika historia ya Tanzania, ni wito wangu kwa

Lowassa asema hatapoteza muda kwenda kupimwa DNA

Image
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema hamtambui mwanamke aliyejitambulisha juzi kama binti yake aliyetelekezwa na kwamba hatapoteza muda kwenda kupimwa vinasaba (DNA), kama msichana huyo alivyotaka. Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam kwa njia ya simu, Lowassa ambaye kwa sasa ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), alisema kuwa kinachofanyika kwenye zoezi hilo ni siasa. Msichana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Fatuma alijitokeza hadharani juzi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kudai kutelekezwa na Lowassa ambaye alisema ni baba yake, kwa kuambiwa na mama yake mzazi. "Wewe unamwamini kweli huyo msichana? Angekuwa mwanangu kweli ningeshamchukua muda mrefu, kwanza wala simjui naona siasa zinaingizwa hapo," alisema. Alipoulizwa kama yuko tayari kupimwa DNA ili ukweli ujulikane, Lowassa alijibu "Kupima DNA huo ni upuuzi. Yaani nipoteze muda wangu kwenda kufanya  upuuzi huo? Siko tayari."

RAIS MAGUFULI: MZEE KIKWETE WATANZANIA ‘TUNAKUMISI’

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya (JKMF) Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuizindua. PICHA NA IKULU RAIS Dk. John Magufuli amesema kwa kazi kubwa ambayo imefanywa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete kwenye uongozi wake kuna mambo makubwa ya maendeleo katika nchi yetu huku akitanguliza uzalendo mkubwa Watanzania wanamkumbuka na wataendelea kukumbuka ‘kummisi’ watake wasitake. Pia ametumia nafasi hiyo kutoa shukrani zake za dhati kwa Rais mstaafu Kikwete kwani ndio amesababisha awe Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano huku akitumia nafasi hiyo kuahidi kuwa atahakikisha Serikali yake itashirikana na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete inayofahamika kwa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF)ambayo ameizindua rasmi leo Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipigiwa makofi mara baada ya kumaliza kuso

MMILIKI WA MABASI YA HBS NA SABENA AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI

Image
Mfanyabiashara Sultan Ahmed au maarufu Chapa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya mabasi ya HBS na Sabena anadaiwa kujiua kwa kujipiga risasi ambayo iliingilia mdomoni kisha kutokea kisogoni leo Jumatano Aprili 11,2018 majira ya saa tatu asubuhi. Taarifa za tukio hilo zinadai kwamba, Sultanambaye ni mwenye asili ya Kiarabu pía ni mmiliki wa kituo kikubwa cha uuzaji wa mafuta ya petroli wilayani Sikonge amejipiga risasi akiwa nyumbani kwake wilayani Sikonge mkoani Tabora huku chanzo cha uamuzi huo wa kujitwanga risasi kikiwa hakijajulikana. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora SACP Wilbroad Mutafungwa amethibitisha tukio hilo na kwamba wanafanya uchunguzi juu ya mauaji hayo.