Posts

Showing posts from May 28, 2014

Mrembo Anaswa Kavaa Nguo za Marehemu Adamu Kuambiana, Afunguka Yote

Image
Stori: Hamida Hassan na Gladness Mallya AMA kweli duniani kuna sarakasi! Takribani siku kumi tangu alipofariki dunia aliyekuwa ‘kichwa’ kwenye filamu za Kibongo, Adam Phillip Kuambiana (38), mrembo aliyejitambulisha kwa jina Mary Njombe amenaswa na nguo za staa huyo wakati mali za marehemu hazijagawanywa. Kwa mujibu wa vyanzo vyetu makini, Mary ambaye ni mkazi wa Magomeni Hospitali, Dar amekuwa akipigilia pamba za marehemu hasa baada ya jamaa huyo kutangulia mbele ya haki. “Jamani njooni huku Magomeni Hospitali hapa mtaa wa pili kuna mwanamke anatinga nguo za marehemu Kuambiana,” kilisema chanzo chetu. Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu walifanya msako eneo hilo hadi wakamnasa Mary. Katika mahojiano na gazeti hili, Mary alisema kuwa alikuwa mchumba wa Kuambiana na alichobahatika kubaki nacho ni nguo ambazo alimpatia mara ya mwisho amfulie (zinaonekana pichani). Mary alisema kuwa yeye na Kuambiana walifahamiana tangu mwaka 2006 ambapo alikuwa aki

Mlela Kuoa Mwanamke Aliyemzidi Umri

Image
STAA wa filamu Bongo, Yusuf Mlela ametoa kioja cha aina yake baada ya kufunguka kuwa akifika hatua ya kuingia kwenye ndoa anataka mwanamke atakayemzidi umri. Tofauti na vijana wengine ambao wanapenda kuoa wake wadogo kwao, Mlela alisema anaamini mwanamke akimzidi umri ndoa itadumu na maisha yao yatakuwa mazuri kwani atakuwa tayari ameshakomaa kiakili na atakuwa na uwezo mkubwa wa kuiendesha familia. “Nahitaji mwanamke anayenizidi umri na sitaki nimzidi mimi naamini huyo tutaelewana na ndoa itadumu, sitaki mwanamke ninayemzidi umri mimi maana itakuwa shida kwani sijapangilia hivyo,” alisema Mlela. Na Gladness Mallya

Hata Wema Atembee Peku Posta, Hawezi kumfikia Vanessa Mdee kwa Hili.

Image
Ukiongelea watu maarufu hapa town, ni wazi kwamba Wema ndiye maarufu zaidi kuliko celebrity yeyote yule wa kike hapa bongo, cause kila rika linamjua Wema Sepetu, na haswa vijana wengi wa kike hutokea kumpenda sana Diva huyu, ila tukienda kwa level zakimataifa hapo kidogo ndio utata unapokuja haswa ukilinganisha na presenter maarufu hapa town na mwanamuziki mkali wa Come Over yaani Vanessa Mdee. Haina budi tukubaliane na ukweli kwamba, yuko famous zaidi ki-international zaidi kuliko mtu mwingine anavyodhani kwa mtazamo wa haraka haraka hapa Bongo. Vanessa ni moja ya msanii wa kike ambaye mbali tu na umaarufu wake huo kimataifa bali, ana ule muonekano wa ki-star, kitu ambacho ni nadra sana kukipata kwa wasanii wengi hapa Bongo, ila tukirudi kwa Wema Sepetu ambaye ndiye ana-run industry ya watu maarufu hapa Bongo , upande wa wanawake, ukilinganisha na Vanessa Mdee bado jibu utapata kuwa Vanessa ndie anayekimbiza kwa upande wa muonekano wakistar na umaarufu wa kimataifa

MAMBO 6 AMBAYO WANAUME HAWAPENDI KUFANYIWA NA WENZI WAO

Image
Haya niliyapata kutoka kwa mshauri wa masuala ya mahusiano, ndoa na vijana Frederick Kyara. Hizi ni baadhi tu nakuwekea hapa japo kuna vitu pia wanawake hawavipendi kutoka kwa wenzi wao wanaume. Nayo ni haya hapa, ungana nami kujadili jambo hili ambalo kwangu nimeona ni changamoto au niseme sikujua.  1. Wanaume hawapendi kuambiwa cha kufanya na wenzi wao Mwanamke unapotaka mwanaume afanye jambo usimwambie alifanye bali fanya kama una mpa ushauri.  Mfano ..... hivi kwa nini tusiweke balbu hapa kwenye korido maana kuna giza kweli. Badala ya hivi wewe ...... huoni hapa kwenye korido kuna giza balbu imeungua mwezi sasa hujabadilisha kwa nini? Weka balbu bwana. Atafanya au asifanye kabisa kwa sababu umemwambia cha kufanya.  2. Wanaume hawapendi mwenzi mwenye makelele, mlalamishi Yeye ni kulalamika kuanzia Jumatatu hadi Jumapili. Japo wanawake nao wanasema kuna wanaume walalamishii balaaa. Na wenye gubu wanasusa kula mpaka kuongea wanawanunia wake zao mmmmh!   3

CHEKI PICHA MAMBO YALIVYOKUWA KWENYE PARTY YA WASANII WA BONGO MOVIE DAR LIVE FULL BURUDANI

Image
Kundi la Scorpion Girls likiongozwa na Isabela Mpanda (katikati) likiporomosha burudani wakati wa  Tamasha la Usiku wa Mastaa wa Filamu lililofanyika Dar Live usiku wa kuamkia leo . Mrembo Jacqueline Wolper akiwapa 'hi' mashabiki. Jacob Steven 'JB' akionyesha umahiri wake wa kusakata rhumba wakati wa tamasha hilo. Steve Nyerere naye akionyesha manjonjo yake stejini. Mastaa wa filamu wakiwa jukwaani kuwasalimia mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live. Snura Mushi akiwapagawisha mashabiki. Msanii Afande Sele akiwarusha mashabiki ndani ya Dar Live. Tundaman akiwachizisha mashabiki. ...akizidi kuwapa raha mashabiki. Kingwendu akifanya vitu vyake. Richie naye akionyesha ufundi jukwaani. Dk. Cheni na mwanadada wakienda sambamba. Shamsa Ford akisema na mshabiki. Bi. Mwenda akiwa kapagawa na shangwe za Dar Live. Mrisho Mpoto akiwapa raha mashabiki. Afande Sele akiwapa 'hi' mashabiki. Mgeni rasmi katika tamasha hilo ambaye pia ni Me

UTATA MTUPU KESI YA AUNT EZEKIEL ...!SOMA ZAIDI HAPA..

Image
MSANII  wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel amesema hivi karibuni aligongana uso kwa uso na Ivon Bigilwa ambaye anadaiwa kumchana kwa chupa mkononi na kesi hiyo inaendelea katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam.   Msanii  wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel akliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar. Aunty alisema hayo juzi Jumatatu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mbele ya hakimu Agustina Mbando, akikanusha taarifa ya wadhamini wa Ivon, Christopher Mwaseba na Anthon Mwaseba walioiambia mahakama kuwa mtuhumiwa alikuwa nyumbani akimuuguza mama yake.   Ivon Bigilwa aliyemchana Aunt kwa chupa. Msanii huyo alisema wadhamini hao wanaidanganya mahakama kwa kuwa hivi karibuni alikuwa nchini China na aligongana naye uso kwa uso. Kutokana na hilo, Hakimu Mbando aliwaonya wadhamini hao kwa kuidanganya mahakama na kuwataka wampeleke mtuhumiwa huyo mbele ya mahakama hiyo Juni 10, mwaka h

BOTI YAZAMA NA KUUA WATU WATANO ZIWA VICTORIA

Image
Watu watano wamekufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama   ndani ya Ziwa Victoria.Kamanda wa Polisi wa Mkoawa Kagera, George   Mayungaalisema ajali hiyo ilitokea Mei 23 mwaka huu saa 8 usiku. Boti   ya Mv Kitoko II waliyokuwa wakisafiria kutoka Bugombe kupitia Kasenye   kwenda Mganza wilayani Chato, ilizimika ghafla ikiwa katikati ya   ziwa.Alisema boti hiyo inayomilikiwa na Mama Chacha aishiye Muganza ,   ilikuwa na abiria hao watano,ambao wote walikufa maji. Maiti   aliyepatikana ni mfanyabiashara raia wa Rwanda, Jane Mlekatete (36)   ambaye mwili wake ulikutwa ukielea. Wengine waliozama ambao   hawajapatikana ni Chikola Filbert (22) mkazi wa Muganza, Mapinduzi   Daud ( 38 )mkazi wa Mwanza, Ashana Suzy waliotambuliwa kwa jina moja   moja, wote wakazi wa Kasenyi na Mavombe (23) ambaye ni mkazi wa   Muganza.Alisema chanzo cha ajali hiyo ni boti kubeba mzigo mkubwa. Kwa   mujibu wa Kamanda, ilikuwa imebeba magunia 210.Chanzo kingine cha   ajal

ANGALIA PICHA MWANAMKE ACHANWA NA VIWEMBE KWA WIVU

Image
Stella Mbinga akiwa na majeraha ya viwembe. INASIKITISHA sana! Stela Mbinga ambaye ni mke wa mtu, mkazi wa Tegeta - Kontena jijini Dar amepata balaa kubwa baada ya kuchanwachanwa uso wake kwa viwembe na jirani yake aliyefahamika kwa jina la Zakia Mohamed. Habari kutoka eneo la tukio zinasema kuwa, Zakia na Stella kwa muda mrefu wamekuwa wakiishi maisha ya uhasama na kuringishiana hali iliyojenga chuki miongoni mwao.“Hawa huwa wanashindana kimaisha. Huyu akifanya hivi, mwingine anafanya vile. Cha kushangaza huwa wanatishiana hadi mambo ya vyakula, kwamba nani anakula vizuri zaidi ya mwenzake. “Sasa juzi Stella alikuwa amekaa kibarazani wanazungumza na shoga yake, Zakia alipita akawakuta wanacheka, hata alipokuwa chumbani wakaendelea na vicheko vyao, akahisi wanamsema na kumcheka yeye, alipotoka akamvaa Stella, kumbe alikuwa na kiwembe, akaanza kumchana bila huruma,” alisema mmoja wa majirani wa wanawake hao. Wasamaria wema walimpeleka Stella Kituo cha

MWANAMKE ALIYEHUKUMIWA KIFO AJIFUNGUA.

Image
Mwanamke aliyeasi dini nchini Sudan na kupata adhabu ya kifo amejifungua mtoto mvulana akiwa jela mjini Khartoum kwa mujibu wa wakili wake. Meriam Yehya Ibrahim Ishag, aliolewa na mwanamume mkristo jambo lililopelekea mwanamke huyo kuhukumiwa kifo mapema mwezi huu baada ya kukataa kusilimu tena. Ataruhusiwa kumnyonyesha mtoto wake kwa miaka miwili kabla ya hukumu kutekelezwa. Meriam aliyezaliwa na wazazi waisilamu, alihukumiwa na mahakama ya ya kiisilamu. Bi Ibrahim alihukumiwa kifo kwa kosa la zinaa kwa sababu ameolewa na mwanamume mkristo wa kutoka Sudan Kusini na kwamba ndoa yao haikubaliki chini ya sheria ya kiisilamu ambayo inasema kuwa mwanamke muisilamu hawezi kuolewa na mwanamume mkristo. Kwa kosa hilo, jaji alimuhukumu adhabu ya mijeledi miamoja, adhabub ambayo itatekelezwa pindi mama huyo atakapopata nafuu kutokana na kujifungua. Bi Ibrahim alilelewa kwa njia ya kikristo , dini ya mamake kwa sababu babake aliyekuwa muisilamu hakuwepo katika