Posts

Showing posts from January 20, 2016

A - Z YA TIMBWILI LA SHILOLE KIUNO NA NUH MZIWANDA STUDIO

Image
Kimenuka mbaya! Gumzo kubwa mjini ni timbwili ‘hevi’ aliloliangusha Mbongo-Fleva wa kike, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ au Shishi’ ndani ya Studio za Clouds TV mara tu baada ya kumuona aliyekuwa mwandani wake, Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ katika zoezi la kutaka kuwapatanisha baada ya kutemana hivi karibuni hivyo mahojiano yakavurugika na kwamba upatanisho haukufanikiwa. Mara tu baada ya kuchomoka kwenye ‘intavyu’ hiyo, Shilole alitimkia nchini Afrika Kusini (Sauz) lakini alipata nafasi ya kuzungumza na gazeti hili kuelezea kile kilichotokea. Shilole alisema, hakuna siku amewahi kufikia wakati mgumu kama siku hiyo ambapo aliitwa na mmoja wa watangazaji wa Clouds TV, akimuomba wafanye mahojiano na akakubali akijua yatakuwa ni mahojiano ya kawaida yahusuyo muziki na shughuli zake zingine kama msanii wa kawaida. Alisema kuwa kwa upande wake intavyu hiyo ilikuwa ngumu mno kwani hakutarajia na maswali yaliyomhusu Nuh Mziwanda ndiyo maana yakatokea yaliyotokea. “Ile ku

SERIKALI YAKANUSHA UZUSHI UNAOENEZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII KUMHUSU RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Habari MAELEZO Bi Zamaradi Kawawa akitoa ufafanuzi juu ya taarifa za uzushi unaosambazwa katika mitandao ya Kijamii ya ndani na nje ya nchi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimwa Dkt. John Pombe Magufuli amefukuza wageni kutoka nje waliokuwa wanafanya biashara hapa nchini kwa kuwa Serikali yake haitataki wageni wafanye bishara zao nchini ambapo ukweli ni kwamba Serikali haijafukuza wageni wanaofanya biashara zao nchini na haina mpango wa kufanya hivyo kwa wageni wanaoishi nchini kwa vibali vilivyotolewa kisheria na Serikali.kushoto ni Naibu Kamishna na Msemaji wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abbas Irovya na mwisho kushoto ni Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani Isaac Nantanga,Kulia ni Naibu Kamishna wa Idara hiyo Bw.Wilson Bambaganya. Naibu Kamishna na Msemaji wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abbas Irovya akitoa wito kwa Watanzania kuwafichua wale wote wanaoingia na kuishi nchini kinyume cha sheria ili hatua stahiki ziweze kuch

JAJI LUBUVA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA NEC

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kulia) akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo 20 Januari, 2016  katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Jijini Dar es Salaam  wakati alipofungua Mkutano wa Wajumbe wa Baraza hilo uliojadili mambo mengi yakiwemo Afya, rushwa ufanisi kazini na Utawala bora. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Bwana. Ramadhani Kailima. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva (kushoto) akiongea na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa NEC (hawapo pichani) leo 20 Januari, 2016 katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Jijini Dar es Salaam wakati alipofungua Mkutano wa Wajumbe wa Baraza hilo uliojadili mambo mengi yakiwemo Afya, rushwa ufanisi kazini na Utawala bora. Kulia ni Katibu wa Mkoa TUGHE Bwana Gaudensi Kadyango na katikati ni Katibu wa Baraza hilo Bi. Rose Malo. Mkurugenzi wa Uchaguzi Bwana. Ramadhani Kailima akiongea  na Wajumbe wa Baraz

Linah: Mastaa Afrika wananitaka kimapenzi

Image
  Staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Estalina Sanga ‘Linah’. Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Estalina Sanga ‘Linah’ aachane na mchumba wake, amekiri kutakwa kimapenzi na mastaa wa muziki nje ya nchi (Afrika). Akichonga na Amani Linah amesema, mara nyingi amekuwa akisumbuliwa kimapenzi na mastaa wengi wa muziki Afrika lakini hakuwa tayari kuwaweka wazi na wala kutaja kama alishawahi kubanjuka na mmoja wapo kati ya hao. “Ni kweli wapo wengi walionitaka kimapenzi, lakini itabaki kuwa siri yangu kujua ni wangapi na nilimkubalia nani kati ya hao,” alisema Linah.

DKT. KIGWANGALLA AUNDA KIKOSI KAZI KUBORESHA HUDUMA ZA MFUKO WA AFYA YA JAMII (CHF)

Image
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla. Na Rabi Hume, Modewjiblog Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameanzisha kikosi kazi cha watu 24 ambacho kitakuwa na kazi ya kutengeneza mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Katika taarifa ambayo imetolewa na Dkt. Kigwangala imeeleza kuwa kazi ya kuanzisha kikosi kazi hicho ni agizo kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ambaye alimtaka aanzishe kikosi hicho ili washirikiane kuanzisha mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii. “Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu alinipa kazi ya kuunda kikosi kazi maalum na kushirikiana nacho kutengeneza mpango mkakati wa kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF),” alisema Dkt. Kigwangalla. Dkt. Kigwangalla amewa

DIAMOND PLATINUMS ATANGAZA NAFASI YA KAZI

Image
  

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASILI DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Chiku Galawa baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma January 20, 2016 ambako pamoja na mambo mengine anatarajiwa  kuhudhuria vikao vya Bunge. Kulia ni mkewe Mary. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)