Posts

Showing posts from February 22, 2017

STAA AGNES GERALD WAYA APANDISHWA MAHAKAMA YA KISUTU,AACHIWA KWA DHAMANA

Image
Mrembo anayepamba video za wasanii nchini, Agnes Gerald Waya maarufu kama Masogange au Deal (28), amepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kutumia dawa za kulevya. Mrembo huyo anayeishi Makongo Juu ambaye alikuwa akitumia muda mwingi kujiziba sura yake kwa mtandio na miwani ya Giza alisomewa tuhuma zake mbele ya Hakimu Mkazi Willbard Mashauri. Hata hivyo, ameachiwa huru baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyowekwa na mahakama. Mahakama ilimtaka Masogange kuwekwa dhamana ya milioni kumi hali kadhalika na wadhamini wake wawili nao walitakiwa kuwekwa kiasi hicho cha fedha. Aidha mahakama imemuamuru kutosafiri nje ya Dar ea Salaam bila ya kupata kibali cha Mahakama. Akisoma hati ya mashtaka, wakili wa serikali, Constantine Kakula amedai kuwa kati ya Februari 7 na 14 mwaka huu katika Eneo na Wilaya isiyojulikana lakini ndani ya jiji la Dar es salaam, Masogange alitumia dawa za kulevya aina ya Heroin (Di

UHALISIA WA MSHAHARA WA MWALIMU BAADA YA MAKATO MAPYA YA 15% YA BODI YA MIKOPOYA ELIMU YA JUU

Image
Baada ya bodi ya mikopo ya E limu ya juu kufanyiwa makato haya ni baadhi ya mchanganuo wa makato kwa mshahara halisi, Baadhi ya makato katika mshahara wa M walimu ni kama inavyoonekana kwenye mabano;-  Mfuko wa hifadhi ya jamii (35,800 sawa na asilimia 5%)  Bima ya afya (21,480 sawa na asilimia 3% )  CWT (14,320 sawa na asilimia 2%) Bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu -HESLB (107,400 sawa na asilimia 15 %)  Income tax  (86,580 sawa na asilimia 12%). Jumla ya Makato tu ni tsh 265,580/=. Mwalimu anayelipwa mshahara wa  tsh 716,000/= anabakiwa na tsh.450,420/= kwa ajili ya kuchangia michango iliyowekwa kwa shuruti na kugharamia maisha yake. *Kila mmoja apige hesabu kutokana na mshahara wake, bila kusahau kuweka makato ya mikopo kutoka kwenye taasisi mbalimbali* Baada ya hapo kinachobaki kipeleke kwenye matumizi yako binafsi:- 1. Maendeleo 2. Chakula 3. Kodi ya pango 4. Umeme 5. Maji 6. Usafiri 7. Mawasiliano 8. Shughuli za kijamii 9. Tegemezi 10.Michango ya mwenge, maabara,

BREAKING NEWZZZ…..TIGO WATOA TAARIFA YA KUMKANA MANJI

Image
G

Ridhiwani Kikwete ajibu shutuma ya kutajwa kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya

Image
Mbunge wa jimbo la Chalinze mkoani Pwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete amekanusha vikali shutuma zilizotolewa dhidi yake kuhusu kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya. Moja ya magazeti ya leo yamechapisha habari inayomtaja mbunge huyo kujihuisha na bishara ya dawa za kulevya ambayo imekuwa ikipigwa vita kila kona ya nchi kutokana na kupoteza nguvu kazi ya taifa. Gazeti hilo limeandika kuwa, jina la Ridhiwani limetajwa katika orodha ya watuhumiwa wa dawa za kulevya na kuwa uchunguzi utafanyika. Pia limesema mbunge huyo ametoa kauli nzito kwa hadhara. Kiongozi huyo kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema kuwa, hafanyi biashara hiyo haramu wala hakuwahi kufikiria kuifanya na kwamba nafsi yake i tayari kufa masikini kuliko kupata utajiri kupitia njia hiyo. Aidha, ameeleza kuwa, anaamini kwamba uchunguzi utafanywa ili kuweza kuweka mambo sawa kwani yeye hana kitu chochote cha kuficha. Amesema kwamba, maneno hayo ya shutuma juu

Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji asema Samatta anauwezo wa kucheza ligi kuu Uingereza

Image
Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji Roberto Martinez amekiri kuwa, mshambuliaji na nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta ana-ubora wa kucheza ligi kuu ya  England maarufu kama EPL. Shaffihdauda ilifanya juhudi za kumtafuta kocha huyo ambaye amewahi kufundisha soka England katika vilabu vya Wigan kabla haijashuka daraja pamoja na Everton kabla ya kupewa majukumu ya kuifundisha timu ya taifa ya Ubelgiji. Juhudi zilifanywa na Mbwana Samatta kuiunganisha shaffihdauda.co.tz na Martinez, hatimaye kocha huyo akatoa ushirikiano. Martinez amesema, Samatta ni mshambuliaji mwenye kiwango kikubwa na uwezo wa kucheza soka kwenye ligi yoyote ikiwemo EPL, pia amesema ameongea na kushauriana vitu vingi na Samagoal. Shaffihdauda.co.tz: Umeshawahi kumshuhudia Samatta akiwa uwanjani akiitumikia klabu yake ya Genk? Martinez: Mimi ni kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji kwa hiyo nafatilia kwa karibu sana ligi za hapa kwa hiyo nimeshamuona mara kadhaa akiwa uwanjani.

WENGI WAJITOKEZA KUMUAGA BLOGGER NA MWANA TBN JENNIFER LIVIGHA (CHINGA ONE) HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR

Image
Pichani ni Mpendwa wetu Jennifer Livigha maarufu aliyekuwa Mmiliki wa Libeneke la CHINGA ONE  na Mwanachama mwanzilishi wa  Tanzania Bloggers Network  (TBN) enzi za uhai wake. Marehemu alizaliwa 25.01.1979 Nachingwea, alifariki nyumbani kwake Kinyerezi 18.02.2017 Jijini Dar es salaam. Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa Ini. Atapumzishwa katika nyumba yake ya milele nyumbani kwao Nachingwea.  Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika Ibada ya kuaga Mwili wa Marehemu Jennifer Livigha aliyekuwa mmiriki wa Blog ya Chinga One katika Hospitali ya Amana.  Waongozaji wa Ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Jennifer  Waombolezaji wakiwemo baadhi ya wana Tanzania Bloggers Network (TBN) ambapo Marehemu Jennifer alikuwa mwanachama  Mmoja ya waombolezaji akitoa historia fupi ya Marehemu Mmoja wa wanafamilia akitoa utaratibu kabla ya kuanza kutoa heshima za Mwisho kwa mpendwa wetu Jennifer  Baadhi ya wanachama wa Tanzania Bloggers Netwo