Baba Diamond Ashinda Njaa
NA WAANDISHI WETU, Risasi Jumamosi DAR ES SALAAM: Wakati mwanaye staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul āDiamondā, mama yake mzazi, Sanura Kassim āSandraā, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan āZari The Boss Ladyā na mwanaye Tiffah wakiteketeza kiasi cha fedha kinachokadiriwa kufikia shilingi Mil.100 barani Ulaya walikokwenda kula bata, baba mzazi wa msanii huyo, Abdul Juma anadaiwa kushinda njaa kutokana na ugumu wa maisha, twende na Risasi Jumamosi. Baba mzazi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul āDiamondā, Mzee Abdul Juma. Diamond na familia yake hiyo sambamba na madansa wake, waliondoka nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kwenda Frankfurt, Ujerumani ambapo pamoja na kufanya ziara ya kimuziki katika nchi tofauti balani Ulaya, staa huyo aliitumia ziara hiyo kuponda raha. Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul āDiamondā, mzazi mwenzake, Zarinah Hassan āZari The Boss Ladyā pamoja na mtoto wao Tiffah wakila ābataā Ulaya. TUJIUNGE NA CHANZO Chanzo makini k...