Posts

Showing posts from October 30, 2013

Kiongozi wa waasi wa M23 ajisalimisha

Image
Kiongozi wa waasi wa M23 Bertrand Bisiimwa ameripotiwa kusalimu amri kwa jeshi la Uganda. Kiongozi huyo wa waasi alivuka na kuingia nchini Uganda kwenye masururu wa magari mawili huku wanajeshi wa Umoja wa Mataifa na wale wa DRC walipofika kilomita tano kuelekea katika kambi yake ya kijeshi Mwandishi wa BBC Ignatius Bahizi amesema baada ya kuongea na afisaa mmoja wa usalama eneo la Bunagana alimthibitisha kujisalimisha kwa Bisiimwa akisema kuwa anahojiwa na maafisa wa usalama katika eneo la Bunagana katika mpaka wa Uganda na Congo DRC. Waasi wa M23 mnamo siku ya Jumatatu walitoroka maeneo yao ya vita ikiwemo eneo la Rumangabo baada ya kukabiliwa na mashambulizi kutoka kwa jeshi la UN na sasa inaarifiwa wametorokea msituni. Majeshi yanayopambana na waasi hao yamefanikiwa kuwashinda waasi hao katika miji waliyokuwa wameiteka na sasa kuna matumaini kuwa jeshi la DRC linaweza sasa kusitisha harakati za kundi hilo ambazo zilianza miezi 20

Mtuhumiwa sugu akamata mkoani Simiyu...Silaha 45 za kivita , 17 za kienyeji na risasi 892 zanaswa

Image
OPERESHENI Maalumu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu kukabiliana na vitendo vya Ujambazi, Ujangiri wa uwindaji haramu pamoja na wahamiaji haramu umefanikisha kukamatwa kwa silaha 45, zikiwemo za Kivita na 17 za kienyeji na risasi 892 na magazine 24 huku watuhumiwa sugu wa ujambazi na ujangiri wakitiwa mbaroni. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Salum Msangi. Akizungumza jana na mbele ya waandishi wa Habari ofisini kwake, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Salum Msangi alisema kuwa opresheni hiyo ilitokana na kuwepo vitendo vya uhalifu katika Wilaya tano za Mkoa huo na kwenye maeneo ya mbalimbai ya Mapori Tengefu ya Uwindaji kwa kipindi cha mwaka moja tangu kuanzishwa kwake Desemba 2012. Silaha zilizokamatwa za kisasa na za kienyeji. Kamanda Msangi alieleza kuwa miongoni mwa silaha hizo 45 na magazine 28 zilikamatwa ni pamoja na SMG 7 risasi 763 na G3 moja ikiwa na risasi zake 35 iliyokuwa ikitumiwa na mwanamke mmoja aliyekamatwa Hollo Mabuga

NAFASI MPYA ZA KAZI BENKI KUU ( B.O.T) ZAIDI YA 50

Accountants, Database Administrator, Business Analyst, Web Developer, Computer System Analyst/Programmer, IT Technician, Senior Enterprise Architect (Information Systems Services), Senior Legal Officer, Economist, Financial Analyst, Bank Examiner, Receptionist, Office Attendant (Kitchen), Artisan (Plumber), Personal Secretary, Security Officer, Risk Analyst, Senior Legal Officer, Drivers, Messenger, Bank Officer, Senior Supplies Officer, Human Resource Officer Applications deadline: 11th November, 2013 EMPLOYMENT OPPORTUNITIES The Bank of Tanzania, an equal opportunity employer and Tanzania’s central bank, is looking for suitably qualified young Tanzanian citizens of high personal integrity to fill the following vacant positions at the Head Office and at its Branches in Mwanza, Mbeya, Arusha, Zanzibar and Training Institute, Mwanza. 1 Position: Accountant III (Domestic Payments and Settlement) - 2 Posts Reports to: Head of Division Contract type: Contract for

Inatisha!! Mganga akutwa na kiganja cha binadamu akimuuzia mteja wake kwa milioni 100 huko Mwanza..

Image
Mtu mmoja jijini Mwanza anadaiwa kukamatwa na kiganja cha mtu akiwa anajiandaa kumuuzia mteja kwa sh million 100. Washukiwa walikamatwa jana karibia na uwanja wa ndege wa Mwanza wakifanya biashara hiyo haramu.... Baada ya upekuzi wa kina, mteja alikuwa ana milioni 100 na mganga alikutwa na kiganja cha binadamu ambacho kilikuwa kibichi kikitoa damu. Kiganja hicho kilikuwa kimevishwa tunguri na nywele za binadamu.

VIONGOZI, WASANII NA WANANCHI WAJITOKEZA KUUAGA MWILI WA MAREHEMU BALOZI ISAAC ABRAHAM SEPETU(BAB​A MZAZI WA WEMA SEPETU) NYUMBANI KWAKE SINZA

Image
Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu enzi za uhai wake Mh. Jaji Warioba akisaini kitabu cha Maombolezo leo mchana nyumbani kwa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa K imataifa Mh. Bernard Membe akisaini kitabu cha maombolezo leo October 29, 2013 nyumbani kwa marehemu Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu Mama Gertrude Mongella akisaini kitabu cha maombolezo kwenye msiba wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu nyumbani kwake Sinza Mori leo October 29, 2013 Mh. Jaji Warioba na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe wakibadilishana mawazo kwenye msiba wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo October 29,2013 Baadhi ya viongozi waliofika msibani kwa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu Watu wa karibu na marehemu waliokuwa wanaishi naye huko Zanzibar wakizungumza jambo kwenye msiba wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo nyumbani kwa