Posts

Showing posts from January 22, 2016

14 Things You Shouldn’t Be Afraid To Tell A Guy In The Bedroom

This summary is not available. Please click here to view the post.

HUU NDO MWONEKANO MPYA WA MSANII LULU BAADA YA KUKATA NYWELE NA KUZIWEKEA RANGI

Image
NA HAYA NDO MANENO ALIYO YAANDIKA MTANDAONI KWAKE Kuna Msemo Unasema "NDEGE WANAOFANANA HURUKA PAMOJA" hii misemo huwa inamaana sana Kwa akili yangu ndogo nilijaribu kuuweka huu Msemo katika Maisha ya kawaida Na nikagundua Una asilimia kubwa ya ukweli Katika Maisha yetu ya mahusiano,urafiki,undugu,ujamaa Na hata ushabiki sio kwamba mambo yanatokeaga Kama miujiza tu,Mfano kwenye urafiki Huwezi kuwa Na Urafiki Na mtu ambaye hamuendani ki mawazo Na mtazamo,mnaweza kutofautiana Muonekano Na kila mtu nje akawa anashangaa lkn ndani yetu mna strong chemistry ambayo inawafanya muwe marafiki,kama Wewe Una character ya umbea Huwezi ukadumu Na rafiki ambaye ana character ya Ucha Mungu...itabidi upate rafiki mwenye character,maono Na mitazamo Kama yako ili kuweza kuruka pamoja Kwenye mahusiano ya Mapenzi iko hvyo pia...mtu anaweza kuwa Na mahusiano Na mtu Na watu nje wasimuelewe imekuwaje ameamua kuwa Na mtu wa aina hyo,pengine NI mtu ambaye hawaendani lbs Kwa Muone

BREAKING NEWS : ZITO KABWE AZIDI KUCHACHAMAA KUHUSU KAMATI ZA BUNGE....SOMA KAULI YAKE LEO

Image
0

MH. MAJALIWA AONGOZA MKUTANO WA WABUNGE

Image
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua mkutano wa wabunge, bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016.  Kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kushoto ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kahilillah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Spika wa Bunge Job Ndugai akizungumza kumkaribisha Mwenyekiti wa Mkutano wa Wabunge, Waziri Mkuu, Kassim Majliwa kufungua mkutano huo bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016. Kulia ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashilillah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)  Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, Nenelwa Mwihambi akitoa mada katika mkutano wa wabunge ulioongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, buneni mjini Dodoma Januari 22, 2016. Watatu kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai na kulia ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashilillah.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu Wabunge, Jenista Mhagama wa Peramiho (kushoto) na January Makamba  wakiteta katika mkutano wa wabunge, bungeni mjini Dodoma Januari 22, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)  Mwanasheria

KAMATI YA KURATIBU MISS TANZANIA YAJITOA KWENYE MASHINDANO

Image
  Mwenyekiti wa Kamati ya kuratibu Miss Tanzania Juma Pinto akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) leo    jijini Dar-es-Salaam juu ya kujitoa kwao kama kamati ya kuratibu Miss Tanzania ambayo ilichagulia na kampuni ya Lino International Agency, kushoto ni Msemaji wa kamati hiyo Joketi Mwegelo na kulia ni Mjumbe wa kamati Gladys Shao . Msemaji wa Kamati ya Kuratibu Miss Tanzania Joketi Mwegelo akitoa maelezo    kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) namna Kamati hiyo ilivyokuwa ikijitahidi kubadili mfumo ili kubadilisha    muonekano wa mashindano ya urembo(Miss Tanzania) kulia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo Juma Pinto.   Waandishi wa habari wakimfuatilia kwa makini Mwenyekiti wa Kamati ya kuratibu mashindano ya Miss Tanzania, Juma Pinto (hayupo pichani) alipokuwa akitoa sababu za kujitoa kwa kamati katika mashindano hayo.   PICHA NA Beatrice Lyimo-Maelezo. Lilian Lundo- Maelezo, Dar es Salaam. Kamati ya kuratibu Miss Tanzania imejitoa rasmi kusimami

SABABU ZA UKAWA KUSUSIA KAMATI ZA BUNGE NA KUMGOMEA SPIKA NDUGAI

Image
Wakati vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge vikitarajiwa kuanza leo kwa uteuzi wa wajumbe, wabunge wa upinzani tayari wameanza kwa kumtikisa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai, baada ya kususia uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo. Dalili za mgawanyiko kwenye kamati hizo zilianza kuonekana juzi, baada ya wabunge hao wa Kambi ya Upinzani kufanya kikao na kuweka msimamo wa kutaka kushirikishwa kwenye uteuzi wa wajumbe. Kambi ya Upinzani ilisema inataka kushirikishwa katika hatua hiyo ikidai kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM), imekuwa ikiwapangia watu wa kuongoza kamati zinazosimamia mapato ya serikali ambazo kikanuni zipo chini yao. Aidha, jana hali ilikuwa ngumu ndani ya kambi ya CCM ambao walifanya vikao tangu asubuhi mpaka jioni kujadili kamati hizo. SABABU ZA UPINZANI KUSUSA Viongozi hao wa kambi ya upinzani walidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakipangiwa watu wa kuongoza Kamati ya Hesabu za Serikali za (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa

JK ATUNUKIWA SHAHADA YA UDAKTARI YA UHUSIANO WA KIMATAIFA

Image
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika ana, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya Kinondoni, Dar es Salaam. (Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog) Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha Rose Migiro akimhudhurisha Shahada ya Heshima ya Udaktari ya Uhusiano wa Kimataifa, Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, katika mahafali ya 30 ya Chuo hicho, yaliyofanyika leo, Alhamisi, Januari 21, 2016, Kampasi ya Kinondon

RAIS DKT MAGUFULI AKIWASALIMIA WANANCHI JIJINI ARUSHA WAKATI AKIELEKEA WILAYANI MONDULI KIKAZI

Image
Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Arusha Mjini wakati akipita Barabarani kuelekea Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli ambako pamoja na mambo mengine kesho tarehe 23 Januari, anatarajiwa kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli kundi la 57/15. Amiri Jeshi Mkuu,Rais Dkt Magufuli akiwasikiliza wananchi kwa makini alipopita maeneno ya Sanawali kuwasalimia wakati akielekea Wilayani Monduli. Baadhi ya Wananchi wa Maeneo ya Sanawali wakishangilia ujio wa Rais John Pombe Joseph Magufuli,alipokuwa akielekea Wilayani Monduli mapema leo asubuhi. Rais Magufuli akiwa amevalia sare za kijeshi amesimamishwa na kuwasalimu wananchi katika maeneo ya SANAWALI, TEKNIKO, NGARENALO, MBAUDA, MAJENGO na KISONGO