Posts

Showing posts from May 29, 2013

MWAKILISHI WA BIG BROTHER TANZANIA BI. FEZA AZIDI KUCHANJA MBUGA

Image
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwenye   mitandao  mbalimbali nchini Tanzania, mrembo huyu, mwanamuziki Feza Kessy, ndiye atakayeiwakilisha Tanzania katika Big Brother Africa 2013 (BBA “The Chase.” Well, hizi ni baadhi ya picha zake. Tunaenda vizuri, bahati inaonekana kutuangukia watanzania kwani mshiriki Feza jana ameukwaa ukuu wa kaya ama kwa lugha ya ki-big brother ‘Head of House’. Ilikuwaje? Baba mwenye nyumba, biggie, alitoa task ambayo washiriki walitakiwa kuelekea bustanini na kuchagua box, ambaye angechukua box la ushindi ndo huyo angekuwa mkuu wa kaya. Kama zali, bahati hiyo ilimuangika mrembo Feza. Washiriki wenzie akiwemo mtanzania Nando, walimkumbatia kwa furaha kama ishara ya kumpongeza. Iko hivi, ukichaguliwa kuwa mkuu wa kaya, unauwezo wa kumuokoa mtu ambaye anakuwa amependekezwa atoke katika wiki hiyo. Usipofanya hivyo basi wewe mwenyewe unawekwa kikaangoni. Feza alitumia nafasi hiyo kumuokoa Elikem ambaye ni mshiriki kutoka Ghana na

CHANZO CHA KIFO CHA MSANII ALBERT MANGWEA AKIWA UKO MADIBA....................

Image
Ngwea akiwa na msanii Mwenzake M to the P jana south africa. Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo.  Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear  na   M to the P  ambaye walikuwa room moja  wamekutwa wamezima   baada  ya  kuzidhisha  madawa  ya  kulevya... Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini. Akiongea na mwandishi wetu  muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka. Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka na  kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka n

R.I.P ALBERT MANGWEA

Image
Habari  zilizotufikia  ni  kwamba  msanii  Albert Mangwair  amefariki  dunia akiwa  Afrika  kusini Chanzo  cha  kifo  hicho  bado  hakijafahamika  lakini  taarifa  za  awali  zinadai  kuwa  msanii  huyo  hakuamka  tangu  alipolala . Kwa habari zaidi tutawajulisha kadri ya uwezo.   BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE