HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YAJIDHATITI KUIMARISHA MAWASILIANO NA WANANCHI

2
Kiongozi wa ujumbe kutoka Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano  Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO  Bi. Gaudensia  Simwanza akisisistiza jambo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi.  Changwa Mkwazu      wakati wa ziara ya ujumbe huo katika halmashauri hiyo uliolenga kuona utendaji kazi wa Maafisa  Habari na Mawasiliano na namna wanavyokabiliana na changamoto mbalimbali ili kuweza kuisemea Serikali kimkakati.
3
Kiongozi wa ujumbe kutoka Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano  Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO Bi. Gaudensia Simwanza akisisitiza jambo kwa Afisa Habari na Mawasiliano wa Halmashuri ya Wilaya ya Masasi Bi mara baada ya ziara ya ujumbe huo katika Halmashuri hiyo.
4
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya  ujumbe  wa viongozi wa Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO wakati walipotembelea Halmashuri ya Wilaya hiyo ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha Maafisa habari na Mawasiliano kutekeleza majukumu yao kwa weledi na pia kuweka mikakati ya pamoja ya kutatua changamoto zinazowakabili maafisa habari  katika Sekretarieti za Mikoa na Halmashuri.
5
Mwakilishi wa Idara ya Habari MAELEZO Bw. Casmir Ndambalilo akiagana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu mara baada ya ziara ya ujumbe kutoka Chama cha maafisa Habari na Mawasiliano  Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO.
Na Frank Mvungi- MAELEZO
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi. Changwa Mkwazu    Amesema kuwa Dhamira ya Halmashauri hiyo ni kuendelea kuimarisha Mawasiliano na wananchi kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.
Akizungumza na ujumbe wa Viongozi kutoka chama cha maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO)  na Idara ya Habari MAELEZO uliomtembelea Ofisini kwake Bi. Mkwazu amesema kuwa Halmashuri hiyo inatambua umuhimu wa wananchi kupata taarifa za miradi ya maendeleo kwa wakati kupitia vyombo vya habari.
“ Afisa Habari wetu anashiriki kikamilifu katika jukumu hili la kuwajulisha wananchi kuhusu miradi ya maendeleo inayoteklezwa na mikakati yetu ni kumuwezesha zaidi kadiri rasilimali zitakavyopatikana kwa kumpatia vitendea kazi bora ili atekeleze jukumu hili kwa ufanisi “ Alisisitiza Bi. Mkwazu
Akifafanua amesema kuwa mawasiliano ni nyenzo muhimu katika kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuwa wanapata elimu kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo kilimo.
Aliongeza kuwa suala la mawasiliano katika Halmashauri hiyo ni kipaumbele kwa kuwa ndiyo chachu ya maendeleo katika Halmashauri hiyo.
Kwa upande wake Kiongozi wa Ujumbe huo Bi Gaudensia Simwanza amesema kuwa ni wakati muafaka kwa maafisa habari na mawasiliano Serikalini kuwa na mawasiliano ya kimkakati na kuangalia namna bora ya kuwasiliana na wananchi kuhusu yale yanayoteklezwa na Serikali katika maeneo yao.
“ Ni muhimu kwa afisa habari kuonesha umuhimu wa mawasiliano kwa kutekleza majukumu yake kwa weledi” alisisitiza Simwanza.
Ziara ya Viongozi wa chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari MAELEZO inalenga kuimarisha utendaji wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini katika Mikoa na Halmashuri hapa nchini.

Comments

Popular posts from this blog