Posts

Showing posts from May 27, 2018

Waziri Jafo atoa agizo hili

Image
WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa  na Serikali za  Mitaa (TAMISEMI),  Selemani Jafo, ameagiza  kufikia  mwezi Desemba mwaka huu taasisi zote za serikali katika halmashauri ya  jiji la Dodoma zinatakiwa kupata  hati miliki ya maeneo yao. Aidha,  ametoa muda wa mwezi mmoja kukamilishwa kwa ujenzi wa kituo cha afya cha Hombolo jijini  hapa ambacho kimeonekana kuwa ujenzi wake upo nyuma ikilinganishwa na vituo vingine 208 vinavyokarabatiwa nchini. Jafo alitoa maagizo hayo juzi mara baada ya kupokea taarifa ya ujenzi wa kituo cha afya Hombolo iliyotolewa na Mganga wa kituo hicho kilichopatiwa fedha kiasi cha Sh. milioni 500 na serikali kwa ajili ya ukarabati. Katika taarifa hiyo ya ujenzi moja ya changamoto iliyotolewa na Mganga wa kituo hicho,  Dk.Hosea Lotto alisema kituo hicho hakina hati miliki.Dk. Lotto alisema pamoja na majengo ya kituo cha afya Hombolo kuwepo toka mwaka 1968,  lakini mpaka hivi sasa  hawana hati miliki kutoka mamlaka husika. Kutok