Posts

Showing posts from July 22, 2017

Jerry Muro Aiponda Yanga, Adai Kuna Wanafiki

Image
Aliyekuwa msemaji wa Klabu ya Yanga, Jerry Muro amesema kuwa ilikufanikiwa katika utendaji ndani ya uongozi wa mabingwa hao wa kihistoria ni lazima kuangalia ni nani anakuletea ushauri. Muro ameyasema hayo ikiwa ni sikuchache tu zimepita tangu Yanga imtangaze msemaji mpya wa timu hiyo, Dismass Ten aliyochukua nafasi yake. “Yanga kuna majungu watu wanapenda wafanye vitu vyao, kuna wanafiki ambao watakwambia ufanye hiki ukikifanya unaingia chaka. “Wapo Yanga SC watu wenye msaada wa kweli, wazuri sana, wenye akili na wenye mapenzi ya kweli kuhakikisha Yanga inakuwa kama TP Mazembe watu wote hao wapo Yanga. “Unachotakiwa kufanya ni kufungua macho kuangalia ni nani anakuletea ushauri, maana kuna mwingine anakuletea ushauri wakati yeye kashindwa kuongoza nyumba yake kaachana na mkewe ,hajali watoto wake yeye mwenyewe kufua nguo hafui nguo maisha yake yamemshinda,” alisema Jerry Muro aliyekuwa msemaji wa klabu hiyo. Mungu anasema unapojipenda nafsi yako wewe mp

Sanchi Anunua Kiwanja cha Milioni 70!

Image
VIDEO Queen Jane Rimoy ‘Sanchi ’ baada ya kufanya kazi zake za mitindo na upigaji picha amenunua kiwanja cha shilingi milioni 70 kilichopo Mbweni jijini Dar es Salaam . Akizungumza na Risasi Jumamosi , Sanchi alisema kuwa ameamua kununua kiwanja hicho kama moja ya kumbukumbu ya kazi zake alizofanya kwa kipindi cha miaka mitatu. “Unajua mtu akikuona upo kwenye mitandao ya kijamii unaweka picha mbalimbali hajui ni kitu gani unafanya kumbe kila mmoja ana akili yake, mimi najivunia kununua kiwanja hicho tena pembezoni mwa bahari kwani ndiyo ndoto yangu ya muda mrefu,” alisema Sanchi.

Wahuni wa Mwanza Wamng’oa Kucha Kajala

Image
    STAA wa filamu za Kibongo , Kajala Masanja hivi karibuni yalimkuta makubwa jijini Mwanza baada kunyofolewa kucha na wahuni alipokuwa kwenye majukumu ya kazi yake anayoifanya kwa sasa ya kampuni ya mchezo wa kubahatisha. Akipiga stori na Risasi Jumamosi, Kajala alisema kuwa alikuwa kwenye harakati za kazi yake anayoifanya kwa sasa kwenye kampuni hiyo ambapo alikuwa akigawa tisheti ndipo mashabiki wakaanza kumvuta mkono mpaka kumbandua kucha aliyokuwa amebandika mkononi ambayo iliondoka na ukucha wake na kujikuta akipata jeraha na kumwaga damu nyingi. Kajala akipozi. “Yaani mimi nilikuwa sina ili wala lile nagawa matisheti mara wakaanza kunivuta kwa nguvu mpaka wakaitoa kucha yangu, hali hiyo ilinitesa asikwambie mtu jeraha la kucha linauma sana,” alisema Kajala. Aliongeza kuwa, baada ya kucha yake kubanduka alitoa kilio kikubwa kwani alipata maumivu yaliyosababisha ashindwe kuendelea na majukumu yake. “Maumivu niliyopata yalikuwa ni makali mno kias

Kimenuka: Mbasha ‘Amtolea Povu’ Flora

Image
Emmanuel Mbasha. Aliyekuwa mume wa Flora Mbasha ‘Madam Flora’ ambaye pia ni mzazi mwenziye, Emmanuel Mbasha ameibuka gumzo mitandaoni baada ya kuandika ujumbe wa ghadhabu unaodaiwa kuwa huenda ni dhidi ya mtalaka wake. Mbasha aliandika ujumbe huo kama majibu, baada ya hivi karibuni kusambaa kwa taarifa ambazo si za kweli zilizodai kuwa Flora alifanya mahojiano na kituo kimoja cha redio na kutoa maneno ya kashfa dhidi ya Mbasha, akisema uvivu wake kitandani ndiyo chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yao, ambapo Flora alikanusha vikali taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram. Flora Mbasha ‘Madam Flora’. Baada ya taarifa hizi kutua mezani kwa Emmanuel , alipiga kimya kwa muda kutokana na kuwa bize na msiba wa bibi yake, lakini baada ya mazishi, akaingia kwenye mahakama ya mastaa , Instagram na kuandika ujumbe huu. “Sipendi ujinga kabisa kwani hamuwezi kuuza hicho kidaftari chenu mpaka mtafute kiki kwangu?, acheni hizo mnaniingiza kwenye upumbavu wenu i

Katibu wa Habari Ikulu Ajiuzulu Kupinga Uamuzi wa Rais Trump

Image
Rais Trump na Shawn Spicer. Msemaji wa Ikulu ya Marekani, White House, Shawn Spicer , amejiuzulu wadhifa wake kwa madai ya kupinga mabadiliko ya Timu ya Mawasiliano ya Ikulu hiyo. Bw. Spicer ameachia wadhifa huo, kwa sababu hakufurahishwa na uamuzi wa kumteua, Anthony Scaramucci kuwa Mkrugenzi mpya wa Mawasiliano wa Ikulu, Mabadiliko hayo yanafanyika wakati White House ikikabiliwa na uchunguzi kuhusu tuhuma za Urusi kuingilia uchaguzi mkuu wa Marekani wa mwaka jana. Gazeti la New York Times linaarifu kwamba, Bw. Spicer alipinga vikali uteuzi wa Bw. Scaramucci kama Mkurugenzi wa Mawasiliano akidai ni kosa kubwa. Bw. Scaramucci, ameteuliwa kushika wadhifa huo baada ya aliyekuwa akishikilia nafasi hiyo Mike Dubke kujiuzulu Mei mwaka huu.

Mama aliyenaswa bila nguo ‘Airport’ Dar, Mapya yaibuka

Image
ZIKIWA zimepita siku tatu tangu mama mmoja kuzua kizaazaa karibu na eneo la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) kwa kukutwa akiwa barabarani bila nguo, mambo mapya yameanza kuibuka kuhusiana na siri ya kadhia hiyo. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kipunguni Banana, Praxeda Mkandara, ndiye aliyeanza kufichua undani wa kile kilichojiri baada ya kuiambia Nipashe katika mahojiano naye jana kuwa hakika, ni Mungu ndiye ajuaye juu ya uhai wa mama huyo kwa sababu alikuwa katika hatari kubwa ya kuumizwa vibaya na pia hata kuchomwa moto na wananchi walioshtushwa na tukio hilo. Alisema badala ya tuhuma za uchawi zinazoenezwa dhidi ya mama huyo ambaye mtaani kwao ni maarufu, ukweli alioupata kutokana na kauli yake mwenyewe ni kwamba alikuwa amevuliwa nguo na mtu aliyekuwa akidaiana naye siku nyingi na kuachwa eneo hilo. Alisema katika maelezo ya mama huyo, ni kwamba yeye si mchawi na hakuwa akifanya uchawi eneo hilo, bali kuna mtu aliyekuwa akimdai siku nyingi alikutana

Njia 10 Za Kupunguza Magonjwa Ya Mlipuko Wa Kuku

Image
Mlipuko wa magonjwa ni moja ya sababu za hasara kubwa kwa wafugaji na vifo vinavyotokea kwa wakati mmoja. Pindi mfugaji anapokumbwa na janga la vifo vya ndege, kabla ya kufikia mwisho wa mzunguko wa uzalishaji hivyo basi asitarajie kupata faida nzuri mara baada ya mauzo. Hasara itokanayo na vifo inaweza kuepukika au kupunguzwa na kutokea kwa kiasi kidogo. Hili linawezekana, ifuatayo ni namna ya kufanikisha hilo;- 1. Osha vyombo vya maji kila wakati na mwaga maji yaliyobaki. Hakikisha unamwaga maji yaliyosalia mbali na kuosha chombo na sabuni kila siku, weka maji safi yasiyo na dawa na wala usitumie maji ya mto au yale usiyoyajua chanzo chake. Kama utaweka maji dawa basi tumia ‘vitamini’ muhimu kama ‘vitalyte’ ambazo zinasaidia kuua vijidudu. 2. Wape maji kabla ya chakula. Ndege wapo tofauti na binadamu au wanyama wengine. Hakikisha unawapa maji kabla ya chakula hasa kama unatumia maranda, hii ni kuhakikisha hawakanyagani wanapogombania chakula sehemu moja. 3

WATANZANIA WATIKISA TENA TUZO ZA AFRIMMA 2017,DARASSA NA DIAMOND NAO NDANI

Image
Majina ya wasanii wanaowania tuzo za mwaka huu za Afrimma yametajwa. Diamond ameongoza kwenye orodha hiyo kwa kutajwa kwenye vipengele vitano. Rayvanny ametajwa katika vipengele vitatu wakati Darassa na Tuddy Thomas wakitajwa kwenye vipengele viwili. Wengine walitajwa ni Alikiba, Lady Jaydee, Vanessa Mdee, Yamoto Band, Dj D-Ommy, Dayna Nyange na Mose Iyobo. Tuzo hizo zitafanyika October 8 ya mwaka huu mjini Texas. Hii ni orodha kamili ya vipengele hivyo. Best Male West Africa Wizkid – Nigeria Falz – Nigeria Serge Beynaud – Ivory Coast Mr Eazi – Nigeria Toofan – Togo Moh Dediouf – Senegal Davido – Nigeria Stonebwoy – Ghana Tekno – Nigeria Kedejevara DJ (Ivory Coast) Best Female West Africa Tiwa Savage – Nigeria Yemi Alade – Nigeria Efya – Ghana Adiouza – Senegal Becca – Ghana Josey – Ivory Coast Mz Vee – Ghana Simi – Nigeria Best Male East Africa Eddy Kenzo – Uganda Diamond Platnumz – Tanzania Jacky Gosee – Et

CHESTER BENNINGTON AFARIKI DUNIA KWA KUJIUA

Image
Msanii wa muziki kutoka Marekani, Chester Bennington amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 41. Chester alikutwa amefariki dunia akidaiwa kujinyonga mwenyewe nyumbani kwake Palos Verdes Estates mjini Los Angles Muimbaji huyo wa Linkin Park pia alikuwa na urafiki wa ukaribu na Chris Cornell amabye na yeye alijiuwa mwezi Mei mwaka huu kwa kuzidisha madawa. Joe Hahn DJ wa kundi la Linkin Park akielekea msibanit Chanzo cha kifo cha Chester kimeelezwa kuwa marehemu alikuwa akinyanyaswa na mwanaume mmoja hali iliyokuwa ikimpelekea kujiona kama mtoto. Kifo hiko kimetokea wakati kundi la Linkin Park, likijiandaa kwenda kufanya photoshoot mjini Hollywood kwa ajili ya wimbo wao mpya. Marehemu ameacha watoto sita aliokuwa amezaa na wanawake wawili tofauti, pia inaelezwa msanii huyo alikuwa akitumia madawa ya kulevya pamoja na pombe kali.

JPM amkaanga mbunge wa upinzani Kigoma

Image
Dar/Kigoma. Rais John Magufuli ‘amemkaanga’ mbunge wa upinzani wa Jimbo la Buyungu, Kigoma huku akisema kuwa wananchi wa eneo hilo wanateseka kutokana na makosa ambayo waliyafanya wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Akihutubia wananchi wa mkoa huo jana, wakati wa  ziara yake ya kikazi katika Ukanda wa Magharibi, Rais Magufuli alisema maendeleo yanaletwa na chama tawala (CCM) na kwamba wananchi walikosea kuchagua mbunge wa upinzani. Kauli hiyo aliitoa mara baada ya mbunge wa Jimbo la Buyungu, Kasuku Bilago Samson (Chadema) kuelezea kuwa eneo hilo lina uhaba  mkubwa  wa maji. “Kabla sijazungumza chochote naomba mbunge wa hapa awasalimu,” alisema Rais Magufuli ambaye alikuwa wilayani Kakonko kwa ajili ya uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Kibondo-Nyakanazi. Mara baada ya kusimama, mbunge huyo alitumia nafasi hiyo kueleza kero ya maji kwenye jimbo lake. “Naomba niseme tunalo tatizo la maji katika Jimbo la Buyungu hususan Kakonko mjini,” alisema. Licha ya