Posts

Showing posts from March 18, 2018

Naibu Waziri Mavunde Kalazwa Morogoro

Image
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavundeakiwa kalala kitandani Hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro akisumbuliwa na homa kali. Mavunde amesema alipelekwa hospitalini hapo usiku wa kuamkia Jumapili baada ya kujisikia vibaya na saivi anaendelea kupatiwa matibabu

MTOTO ALIYECHOMWA SINDANO KIMAKOSA NA MADAKTARI KICHWANI,CHAANZA KUOZA

Image
Leo stori ninayokusogezea ni kuhusu matukio ya kutokuwa makini katika idara ya afya hasa kwa madaktari yanazidi kuzua wasiwasi kwa wananchi nchini Kenya, tukio lililotokea siku za hivi karibuni ni la mtoto kuchomwa dawa isiyofaa na kumfanya aanze kuoza kichwa. Tukio hili limefanyika katika hospitali ya Malava General Hospital katika jimbo la Kakamega na linatokea huku kukiwa na kesi dhidi ya Madaktari wa hospital ya Kenyatta inaendelea baada ya Daktari kumfanyia upasuaji mgonjwa asiyestahili. Mtoto huyo aliyejulikana kwa jina Clinton Luchivya alikuwa amepelekwa katika hospitali hiyo baada ya kuwa mgonjwa na madaktari kumchoma kichwani baada ya kukosa mshipa wa kumwekea dawa. Kulingana na mama wa mtoto huyo, mwanae alikuwa na ugonjwa wa Malaria kabla ya kupokea matibabu katika hospitali hiyo. Alisema kuwa mwanae alikuwa ameanza kubadilika badilika kabla ya kufahamu kuwa kichwa chake kinaoza.
Image
Huku Drama za Diamond na Wema Zikinoga, Kule Zari Bata Batani – Picha 7 WAKATI Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz akiendeleza drama ya mapenzi na aliyekuwa girl friend wake, Wema Sepetu kupitia mitandao ya kijamii, mzazi mwenzake na mwanamuziki huyo, Zari The Bosy Lady ameendelea kura raha katika Hoteli ya Sun City nchini Afrika Kusini anakoishi. Zari kupitia ukurasa wake wa Instagram ametupia picha saba akila bata katika hoteli hiyo kuonyesha kuwa haumizwi na kile anachokifanya x wake huyo mitandaoni kwa kujiweka karibu na Wema, kupost picha na maneno yanayoonyesha kuwa wamerudisha uhusiano wao. Zari baada ya kuweka picha hizo hakuandika maneno mengi bali ameweka caption hii;  Sun City typa weekend. Kuanzia jana Ijumaa kumekuwa na drama mitandaoni zikionyesha Wema na Diamond kama tayari wamesharudiana baada ya Wema kutupia picha na kipande cha video mpya ya Diamond, African Beauty na kumfagilia boy friend wake huyo wa kitambo. Wema aliandika  “I’m inlove

Mzee Mkapa Ataka Mjadala wa Kitaifa

Image
RAIS Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini William Mkapa amesema ipo haja ya kuitishwa mjadala wa kitaifa wa kujadili hali ya elimu nchini kufuatia shule za serikali kuendelea kufanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya kitaifa. Mkapa ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma amesema hayo mkoani Dodoma wakati wa tukio la kumuingiza kazini Makamu Mkuu mpya wa chuo kikuu hicho cha Dodoma Profesa Egid Mubofu na kumuaga Makamu Mkuu wa chuo hicho aliyemaliza muda wake Profesa Idrisa Kikula. Mzee Mkapa amesema mjadala huo unatakiwa kuhusisha makundi yote ya jamii bila kujali kama ni ya sekta binafsi ama ya umma sambamba na watu wa kawaida siyo wasomi pekee ambapo kupitia njia hiyo anaamini suluhu ya kudumu itapatikana. Hata hivyo, Serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imefanya juhudi kubwa kuondoa ada kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha nne pamoja kuongeza madawati, nyumba za walimu, madarasa, vitabu, kulipa stahiki za walimu