Posts

Showing posts from October 5, 2013

Maiti ya mtoto yachunwa ngozi masaaa machache kabla ya kuzikwa

Image
MAMIA ya wananchi mjini Bunda, wamefurika kushuhudia mwili wa mtoto wa miezi 10 aliyefariki kwa ugonjwa wa malaria na baadaye watu wasiofahamika kuchuna ngozi ya kichwa chake. Tukio hilo ambalo limehusishwa na imani za ushirikiana, lilitokea usiku wa kuamkia juzi katika mtaa wa Nyasura ‘B’ Tarafa ya Serengeti katika mamlaka ya mji mdogo wa Bunda, wilayani hapa. Ofisa tarafa, Justine Rukaka, alisema kuwa mtoto huyo alifariki usiku katika hospitali ya wilaya ya Bunda, baada ya kuugua malaria na mwili wake ukapelekwa nyumbani kwao kwa ajili ya mazishi. Rukaka alisema kuwa kesho yake asubuhi wakati wananchi wanaandaa shughuli za mazishi, walishangaa kuona ngozi ya kichwa chake ikiwa imechunwa na watu wasiofahamika. “Wakati shughuli za mazishi zinaandaliwa ndipo walipogundua kuwa ngozi ya kichwa chake imechunwa kwa kile kinachodaiwa kwamba ni imani za ushirikina,” alisema. Aliongeza kuwa kufuatia hali hiyo, wazazi wa mtoto huyo, wanafam

RIHANNA FULLL MIBANGI UFUKWENI

Image
Rihanna Aka Riri a Bad Girl Ameonakena akiwa Mapumziko huko Thailand akijinafasi beach mbali mbali huku kama kawaida yake akijiliwaza na Mjani aka Bangi...Hii sio mara ya kwanza kwa yeye kuonekana akivuta Bangi ...

HUU NI MUONEKANO WA STUDIO MPYA ANAYOIMILIKI PROF. JAY

Image
Mwanalizombe Studios Ni Recording Lebel Inayomilikiwa na Rapper Profesa Jay, Studio ipo msasani na Ameamua kuipa Jina la Mwanalizomba kwasababu Jay Ni mtu wa Ruvuma na Mwanalizombe maana yake ni Mwana Ruvuma na kufanya hivyo ameonyesha mapenzi ya mkoa wake wa Ruvuma. Producer kwenye studio hii ni Duke Touchez. Profesa ameshindwa kusema amewekeza kiasi gani cha fedha kwenye studio hio ila fahamu kuwa vifaa vilinunuliwa kwa wakati tofauti na ni vifaa vya hali ya juu sana. source: Sammisago.com

MWANAFUNZI WA MIAKA 13 AJIFUNGUA MTOTO WA MIEZI 6 AKIWA SEBULENI BILA KUJIJUA....

Image
  MSICHANA aliyejitambulisha kwa jina la Salma Hemedi (13) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ubungo Plaza, Dar amejifungua maiti ya kichanga cha miezi 6 bila mwenyewe kujijua. Tukio hilo lilitokea Septemba 25, mwaka huu maeneo ya Ubungo National Housing jijini Dar ambapo asubuhi ya siku hiyo, Salma alilalamikia maumivu ya tumbo lake kiasi cha mama yake aliyejitambulisha kwa jina la Rahma Shabani kwenda kuomba msaada wa kitabibu. Mwanamke huyo alieleza kwamba baada ya kurudi ndani alikomuacha mwanaye, alimkuta akiwa amejifungua kichanga sebuleni, kitu ambacho hakukitarajia kwa kuwa alizoea kumnunulia vifaa vya kujisitiri wakati wa hedhi kila alipomlalamikia maumivu ya tumbo akijua yupo kwenye siku zake. Akiwa na manesi walioongozana naye, walimsaidia Salma huku kila mtu akiwa amepigwa na butwaa kwa kilichotokea kwani hakuna aliyekuwa anajua kama Salma alikuwa na ujauzito. Akiongea na waandishi wetu, Salma alisema alipewa ujauzito na mwanaume aliyemtaja kwa jina

KABURI LA MTOTO ALIYEFUFUKA LAFUKULIWA CHINI YA ULINZI MKALI...!! WAKUTA MAAJABU MATUPU KABURINI

Image
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida kaburi ambalo alizikwa mtoto Shabani Maulidi (15), ambaye anadaiwa kufariki dunia miaka mitatu iliyopita na kuonekana akiwa hai hivi karibuni, jana lilifukuliwa na viungo vya mwili wake kukutwa ndani. Kazi hiyo iliyofanyika chini ya ulinzi mkali wa polisi pamoja na Mtafiti wa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mwanza, Lucas Ndungulu, ilizua taharuki kwa umati wa watu waliokuwa eneo hilo, baada ya nyumba ya jirani lilipo kaburi hilo, Masanja Marwa, kubomoka ghafla wakati ufukuaji huo ukiendelea, huku mwanamke mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja naye akianguka na kuzirai. Kwa sasa mtoto huyo ambaye alionekana hai, amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kwa uangalizi wa kitaalamu. Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, Ndungulu alisema kuwa wameamua kufukua kaburi hilo ili kupata sehemu ya viungo vya mwili kwa ajili ya vipimo. “Lengo la kufukua kaburi hili ni kutaka tupate kiungo chochote cha mw