Posts

Showing posts from April 12, 2017

MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE AUSHANGAA UKIMYA WA MWIGULU NCHEMBA

Image
Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete anamshangaa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuendelea kukaa kimya juu ya matatizo ya kiusalama kwa wananchi yanayoendelea nchini wakati yeye ndio kiongozi mwenye dhamana ya kulitatua hilo. Akiongea bungeni Jumanne hii, mbunge huyo amesema, “Kumekuwa na malalamiko mengi sana, tumeshuhudia malalamiko mengine yanahitaji majawabu kama siyo majibu ya haraka ili kuondoa hizi sintofahamu walizonazo wananchi.” “Niwaombe sana hakuna sababu ya mtu kama Mhe. Waziri Mwigulu kuendelea kukaa kimya wakati wananchi wanalalamika juu ya hali yakiusalama katika maisha yao,” ameongeza. “Mimi binafsi niishauri serikali yangu kwamba unapojibu jambo lolote lile unatoa hali ya wasiwasi,” amesisitiza.

ISHU YA ROMA YAMFANYA DAVINA AMUUNGE MKONO WEMA SEPETU

Image
Halima Yahya ‘Davina’. BAADA ya supastaa wa filamu Wema Sepetu kuwashutumu wenzake wa Bongo Muvi kwa kutosapoti harakati za kupiga kelele kufuatia kupotea kwa Mwanamuziki wa Hip Hop, Ibrahimu Mussa ‘R.O.M.A’ kwa siku tatu na kusababisha kutoleana maneno makali mtandaoni na muigizaji mwenzake Vincent Kigosi ‘Ray’, Halima Yahya ‘Davina’ amemuunga mkono mrembo huyo wa zamani wa Tanzania akisema wapo wasanii ambao hawawasapoti wenzao wanapokuwa kwenye matatizo. Wema Sepetu. Akistorisha na Risasi Vibes, Davina alisema waraka alioandika na Wema kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba wasanii wa filamu hawana ushirikiano na wenzao hasa wanapokuwa katika matatizo ni kweli ingawa siyo wote. “Wema alichosema kipo Bongo Muvi, kuna watu hawana ushirikiano na wenzao, mimi huwa nawasapoti sana wenzangu, hata yeye alipokuwa Sentro nilikwenda kumuona, kwenye suala la ROMA karibu asilimia 50 ya wasanii waliposti katika kurasa zao,” alisema na kuwataka wasanii kushirik

BREAKING NEWS: Askofu Gwajima aachiwa huru na Mahakama. 0

Image
Mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuchia huru Mchungaji wa kanisa LA Ufufuo na Uzima Askofu Josephat Gwajima kufuatia kosa la Kutoa Lugha ya Matusi Dhidi ya Muadhama Polycap Kardinal Pengo mnamo mwaka 2015. Chini ya chini ya Hakimu mfawidhi Cyprian Mkeha Mahakama imeamuchia Askofu Gwajima kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya 225 ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.