Posts

Showing posts from March 29, 2016

LINAH: NAJUTA KUMUANIKA MPENZI WANGU

Image
  STAA wa Muziki wa Kizazi Kipya, Estelina Sanga ‘Ndege Mnana’ amefunguka ya moyoni kuwa, kamwe hawezi kurudia kosa la kumuanika mpenzi wake kwenye mitandao ya kijamii au kwa watu na kukiri kuwa ndiyo sababu kubwa iliyochangia kuachana na mpenzi wake, William Bugeme. Akizungumza na Showbiz kwa hisia kali msanii huyo anayebamba na Ngoma ya No Stress alisema, hakuwa akijua kama kuanika uhusiano wake kwenye mitandao ya kijamii kutamletea majanga. “Mimi tena kumuonesha mpenzi wangu nimekoma, najutaaa! Maana kwanza wakimjua wengine watajipendekeza na kumchukua na wengine watampelekea maneno ili tugombane  hivyo bora nikae kimya labda wamjue siku ya harusi tu nimejifunza,” alisema Linah.

HUYU NDO Bilionea Mtanzania Anaetaka Kuinunua BENKI ya BARCLAYS Tanzania!

Image
Inabidi ujue Tanzania inao watu wenye pesa zao na wanayo malengo au mipango mikubwa zaidi ya kibiashara ambayo kama ikienda inavyotakiwa wanaweza kuifanya nchi hii kutajwa zaidi kuwa na matajiri miongoni mwa nchi zenye Mabilionea Afrika. Kituo cha Television cha Marekani CNN kilimuhoji Mtanzania huyu na kikaweka kichwa cha habari ‘kutana na Bilionea mwenye umri mdogo Afrika‘ ni Mohammed Dewji ambaye ameajiri watu karibu elfu ishirini na nane kutokana na viwanda na biashara zake. Mbunge huyu wa zamani wa Singida mjini amesema ‘nimekua nikitaka kununua Benki kwa miaka minne mitano iliyopita, sasa hivi nimeamua nataka kuanzisha Benki yangu kabisa japokuwa hii ishu ya Benki ya Barclays Afrika kuuzwa imekuja na nashawishika japo sijajua kama wanataka mnunuzi atakaeichukua Afrika nzima‘ ‘Nimeshawishika kuinunua Barclays upande wa Afrika Mashariki na ninayo pesa tayari, sijajua wanaiuzaje lakini sina mpango wa kuichukua Barclays yote kwa Afrika,

BREAKING NEWZZ.....KUANZIA SASA WASOMI WENYE CHETI ZAIDI YA KIMOJA KUTO PATA KAZI SERIKALINI,NI WALE WALIO RISIT KWA KUTAFUTA CREDIT.

Image
KUNA TAARIFA ZINAENEA KWA KASI MITANDAONI KUHUSU SERIKALI KUTO KUWAPOKEA WASOMI WENYE CHETI ZAIDI YA KIMOJA KATIKA AJIRA..UJUMBE WENYEWE UNAMUHUSISHA WAZIRI SIMBA CHAWENE NA UKISOMEKA HIVI:- Wazir Simba chawene ametoa tamko la serikali kuwa , serikali ya Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania haiko tayari kuajiri wasomi wenye vyeti vya baraza la mitihani kuanzia vyeti viwili na kuendelea,watakaopata ajira yoyote ile ya moja kwa moja serikalini ni wasomi wenye cheti kimoja tu,.Wale waliosoma kwa kuunga unga ,mara kutafta credit,mara kurudia mitihan watafte ajira kwa mashirika binafsi.Serikali inataka kuwaajiri wasomi wenye cheti kimoja tu waliosoma moja k wa moja.System hii itaanza kwenye ajira za walim za mwaka huu 2016 zinazoenda kutangazwa mda c mrefu mwezi wa nne mwanzoni.simba chawene ameyasema hayo akiwa na waandishi wa habar pale jijin Dar leo majira ya asubuh ili kuwajuza watanzania kuwa ni tamko la serikali. Rai kwa weny vyeti vingi,mtakua mnaomba ajira kivy

BREAKING NEWZZ.. ZAIDI YA WAFANYAKAZI 400 KUPOTEZA AJIRA TTCL

Image
Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) ipo kwenye maandalizi ya kupunguza wafanyakazi wasiohitajika kwa sasa kutokana na kasi ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia. TTCL inayotoa huduma za simu na pia kutoa mitandao kwa kampuni zilizo na leseni ya huduma hizo, itapunguza wafanyakazi 400 ili kuongeza ufanisi na hivyo kumudu ushindani katika sekta ya mawasiliano dhidi ya kampuni binafsi. Mapema mwaka jana, Serikali iliamua kununua asilimia 35 ya hisa za TTCL zinazoshikiliwa na kampuni kubwa ya huduma za simu nchini India, Bharti Airtel na baadaye mwezi Mei, 2015 aliyekuwa Naibu Waziri wa Sayansi na Mawasiliano, January Makamba aliliambia Bunge kuwa Serikali iko katika maandalizi ya mwisho ya kumiliki hisa zote za kampuni hiyo kubwa kwa huduma za simu za mezani nchini. Chanzo cha habari kutoka ndani ya kampuni hiyo kinaeleza kuwa kati ya wafanyakazi 1,500 wa TTCL, zaidi ya 400 watapoteza ajira katika mpango huo wa kudhibiti gharama za uendeshaji. “TTCL itaomba fedha ili kuwalipa

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 29/03/2016

Image