Posts

Showing posts from July 27, 2013

HIKI NDO CHOO CHA DHAHABU KILICHO NUNULIWA NA KANYE WEST NA MKEWE .

Image
Kwenye nyumba ya Kanye West Na Kim Kardashian yenye thamani ya dola Milioni 11 za Kimarekani kuna vitu vyenye thamani kubwa kama vitanda, jiko na makoche, ila kilicho make headline zaidi ni vyoo vyao vyenye thamani ya dola Milioni 1 za KiMarekani. Kwa mujibu wa HipHopWired.com , West na Kardashian wamenunua vyoo vinne vya Gold vyenye thamani ya dola milioni moja. Bonyeza Read More Uone Picha Zaidi     SOURCE-sammisago.com

SIMBA USO KWA USO NA COASTAL UNION KESHO TANGA

Image
Wekundu wa Msimbazi Simba, “Taifa Kubwa” muda huu wapo Mjini Tanga kwa ajili ya mechi ya kujipima uwezo dhidi ya wenyeji wa dimba la Mkwakwani, wagosi wa Kaya Coastal Union hapo kesho. Akizungumza kwa njia ya simu, kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kiwhelo “Julio” amesema wachezaji wote  wapo salama na wapo safarini kuelekea Tanga ambapo kesho majira ya saa 10 jioni wanatarajia kucheza mechi moja kali ya kujipima ubavu  dhidi ya vijana wa Hemed Morocco, huku kivutio kikubwa kikiwa ni wachezaji wa zamani wa Simba ambao kwa sasa wapo Coastal, beki kisiki, Juma Said Nyoso na kiungo fundi, Haruna Moshi Shaaban Mnyamwezi “Boban”. Boban na Nyoso walitemwa enzi za kocha Mfaransa, Patrick Liewig baada ya kutolewa ligi ya mabingwa barani Afrika na LIbolo ya Angola kwa tuhuma za utovu wa nidhamu pamoja na akina Ramadhan Suleiman Chombo “ Redondo”, Ferlix  Mumba Sunzu, David Luhende, Juma

HARUNA CHANONGO - SINA AKAUNTI FACEBOOK - ANAYETUMIA JINA LANGU KWENYE MTANDAO HUO NI FEKI

Image
   Winga wa timu ya taifa ya Tanzania anayekipiga klabu ya Simba Haruna Chanongo amasema amesikitshwa mno na kitendo cha mtu asiyefahamika kutumia jina lake na picha kwenye mtandao wa Facebook. Akizungumza na mtandao huu kutoka Kampala alipo na timu ya taifa ya Tanzania inayojiandaa kucheza mechi ya pili kuwania nafasi ya kucheza kombe la CHAN, amesema yeye binafsi hana akaunti kwenye mtandao wa kijamii wa FACEBOOK lakini anashangaa amekuwa akipokea malalamiko kutoka kwa watu wa karibu kuhusu suala la akaunti hiyo. "Kiukweli mie sina akaunti Facebook, sasa nashangaa muda mwingine napata malalamiko kutoka kwa watu wangu wa karibu na hata mashabiki kuhusu mambo ya ajabu huyo aliyofungua hiyo akaunti anayafanya. Ninachotaka kuweka wazi mie sina akaunti Facebook hivyo watu wote wafahamu kuhusu hilo," alimaliza Chanango amepa kwamba leo akipata nafasi atajitahidi kwa hali na ma

MWALIMU NA MWANASIASA MKONGWE JOHN SHILATU AZIKWA KATIKA MAKABURI YA KINONDONI

Image
 Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu John Shilatu likiingizwa kwenye gari kutoka mochwari.  Jeneza lenye mwili wa Marehemu Shilatu likiwa mbele ya kadamnasa wakati wa Ibada  Jeneza lenye mwili wa Marehemu Shilatu likipelekwa eneo atakalozikiwa maeneo ya makaburi ya kinondoni jijini Dar es Salaam. SOMA ZAIDI.... »

RAIS KIKWETE AKIWA ZIARANI NGARA MKOA WA KAGERA

Image
  Rais Kikwete akihutubia kijiji cha Rulenge   Rais Kikwete akihutubia umati Ngara   Rais Kikwete akihutubia umati Ngara   Rais Kikwete akisalimia wananchi Rulenge Rais Kikwete akiwasili Ngara

IRINE CHEPTAI WA KENYA AANGUKA NA KUZIMIA BAADA YA KUMALIZA MBIO ZA MITA 3,000

Image
Daktari wa kwanza kabisa kumkimbilia Irine Cheptai akihaha kuuzindua moyo wake baada ya kuzimia, alipokuwa akimaliza mbio za mita 3,000 kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini London jana. Jopo la Madaktari wakihangaika kumpatia huduma ya kwanza Irine Cheptai, alianguka na kuzimia wakati akimaliza mbio za mita 3,000 kwenye Uwanja wa Olimpiki. Cheptai akiwa ametungikiwa mtungi wa hewa ya oksijeni, baada ya kuanguka na kuzimia kutokana na shambulio la moyo. Hata hivyo alikuja kurejewa na fahamu zake akiwa hospitali. Cheptai (wa pili kulia) akikimbia mbio za mita 3,000 kwenye Uwanja wa Olimpiki jijini London. LONDON, England Cheptai, binti wa miaka 21, alimaliza mbio akiwa nafasi ya 11, katika muda bora zaidi katika rekodi yake binafsi, alipotumia dakika 8:56.20, lakini akaanguka ghafla na kupoteza fahamu baada tu ya kuvuka mstari wa kumalizia MKIMBIAJI wa mbio ndefu wa kimataifa wa Kenya, Irine Chebet Cheptai jan

ANGALIA PICHA ZA KILICHOJIRI KATIKA USAHILI WA BONGO STAR SEARCH DAR

Image

SINTAH : “WATANZANIA HAWAPENDI KUAMBIWA UKWELI”

Image
Mwigizaji maarufu kwenye bongo movie Christine Manongi a.k.a Sintah amefunguka na kusema kwamba “watanzania hawapendi kuambiwa ukweli”. Sintah aliendelea kwa kusema kwamba “vijana wengi wa sasa wanapenda kuishi maisha ya kuigiza na kupelekea kupoteza muda mwingi kwenye mambo yasiyo na msingi.” Hivi karibuni Sintah alipinga kauli ya mwigizaji na mwanamuziki Shilole kutaka kufanya kazi na Jenifer Lopez ambao ilipelekea wasanii hao wawili kuangia katika beef.

SERIKALI YATANGAZA MISHAHARA MIPYA KWA WATUMISHI WA UMMA

Image
Madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimuudumia mgonjwa hospitalini hapo. Wafanyakazi wa sekta ya afya ni miongoni wa walio ongezewa mishahara na serikari katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14. Picha na Maktaba.  SERIKALI imetangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma itakayoanza kutumika mwezi huu, huku kima cha chini kikiongezwa kwa asilimia 41.18 kutoka Sh 170,000 hadi Sh240,000. Vilevile, mishahara ya watumishi wengine wa umma imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41.  Waraka namba moja kwa watumishi wa umma uliotolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utum ishi wa Umma, George Yambesi Julai 2 mwaka huu, unaeleza kuwa marekebisho hayo ya mishahara yatahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa. Wengine watakaonufaika na marekebisho hayo ni watumishi walioshikizwa kwenye taasisi za umma na watumishi ambao watakuwa kwenye likizo inayoambatana na kuacha kazi, kustaafu kazi au kumaliza mikat

JUMUIYA YA KIISLAM (ZADEO)-ZANZIBAR YAFANYA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI

Image
Rais wa Jumuiya Kiislamu (ZADEO) Sheikh, Haji Ameir Haji, akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma za kuwatapeli mahujaji, huko katika ukumbi wa watu wenye ulemavu Kikwajuni weles Mjini Zanzibar. Waandishi wa habari mbalimbali wakiandika habari kwa kina zilizotolewa na Sheikh, Haji Ameir Haji juu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake, huko katika ukumbi wa watu wenye ulemavu Kikwajuni weles Mjini Zanzibar. Mwandishi wa habari, Yahya Saleh wa chuchu Fm akimuuliza suali Rais wa Jumuiya Kiislamu (ZADEO) Sheikh, Haji Ameir Haji, katika mkutano wake na waandishi wa habari, huko katika ukumbi wa watu wenye ulemavu Kikwajuni weles Mjini Zanzibar.   Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.

HATIMAYE KAJALA NAYE AAMUA KWENDA SOUTH AFRIKA..Angalia PICHA AKIWA HUKO

Image
Juzi mwigizaji wa bongo movie Kajala aliondokoka nchini kuelekea Afrika ya kusini kwa ajili ya safari binasfi ambayo pamoja na mambo mengine alitembelea shue ya uigizaji ya AFDA (AFDA the South African School of Motion Picture Medium and Live Performance) iliyopo nchini humo.

RAY C ATANGAZA KURUDI UPYA KWENYE GAME LA MUZIKI.....

Image
Mabibi na mabwana mko tayari kwa ujio mwingine wa Ray- C. Malkia wa kiuno bila mfupa Rehema Chalamila aka Ray-C ametangaza ujio wake rasmi baada ya kuwa chimbo kwa kipindi kirefu toka apate matatizo miezi kadhaa iliyopita. Ni baada ya siku chache kupita toka Ray-C atamke kuwa anapenda sauti ya ‘dogo lake’ Recho na kuwa atakuja kufanya naye kazi, leo amethibitisha kuwa mwezi Agosti ndio anarudi rasmi kutoka chimboni. Kupitia akaunti ya Instagram Ray-C aliweka picha ya gazeti moja lililoandika ‘Ray-C kuonekana hadharani mwezi Agosti’, na baada ya followers wake kutaka ufafanuzi ndipo alifunguka kwa kusema “For Sure it’s bout time nw nimewapa muda sana watoto sasa mdada is coming back”. Ray C aliwauliza marafiki zake wa Instagram kama wapo tayari kwa ‘come back’ yake, wengi wameonekana kutamani muda ufike waweze kumuona tena Ray-C akirudi katika muziki. Hizi ni baadhi ya comments kutoka kwa mashabiki wake.

BREAKING NEWZZZ.....HII NDO BARUA YA WAFUNGWA WA KITANZANIA waliokamatwa na madawa ya kulevya Hong Kong..WAWATAJA WAHUSIKA MH.MBUNGE NAYE ATAJWA

Image
Barua kwa lugha ya Kiswahili Barua kwa lugha ya Kiingereza.