Posts

Showing posts from February 17, 2018

Breaking News: Salum Mwalimu Akamatwa na Polisi

Image
Mgombea ubunge wa Chadema Kinondoni, Salum Mwalimu. MGOMBEA  ubunge wa Chadema Kinondoni, Salum Mwalimu amekamatwa na polisi kituo cha kupigia kura cha Idrisa Kata ya Magomeni. Akizungumza na Global TV Online mchana huu Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene amethibitisha kukamatwa kwa mgombea huyo.

Diamond Platnumz ateswa na maamuzi ya Zari

Image
 Leo February 16,2018 Diamond Platnumz ameonekana kuonyesha hisia zake juu ya maamuzi  ya Zari kuachana nae, kupitia instagram account yake Diamond amekuwa akipost video clips mbalimbali za nyimbo za mapenzi. Kupitia instagram ya Diamond Platnumz amepost kipande cha wimbo wake wa Sikomi na kuandika “Unajua Nyimbo zingine Unaziimba ila Hata we mwenyewe zinakuingia Baadae😟…. Anyways 28 Days Before the Reveal of #AboyFromTandaleAlbum!🔥 #SikoMi Bonus Track on #AboyFromTandale Available on All Digital Platforms now!”

Wananchi Wamkataa Mkuu Wa Wilaya Mbele Ya Waziri Mkuu

Image
WANANCHI wa wilaya ya Kwimba wamemuomba Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aondoke na mkuu wa wilaya hiyo Bw. Mtemi Msafiri baada ya kutoridhishwa na utendaji wake. Wametoa ombi hilo jana (Ijumaa, Februari 16, 2018) walipozuia msafara wa Waziri Mkuu alipowasili katika Ofisi za Halmashauri ya wilaya Kwimba zilizopo Ngudu kwa ajili ya kuzungumza na watumishi akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. Wananchi hao walimkataa mkuu wao wa wilaya Bw. Msafiri kupitia ujumbe wa mabango 17, ambapo Waziri Mkuu amewataka wananchi hao wawe watulivu wakati Serikali inafanyia kazi malalamiko yao. Wananchi hao wanadai kwamba Mkuu huyo wa Wilaya anatabia ya kuamrisha polisi wawakamate kwa kisingizio cha uzururaji na kisha wanawekwa mahabusu, ambapo baada ya muda wanatolewa na kwenda kulima kwenye shamba lake. Waziri Mkuu amesema Serikali inahitaji kila mtumishi atambue majukumu yake na ayatekeleze. “Hakuna atakayeonewa, haki zenu zote tunazitekeleza nanyi mnataki

Mwanamume aliyejibadilisha jinsia 'amnyonyesha mtoto'

Image
Mwanamume aliyejibadilisha jinis na kuwa mwanamke amefanikiwa kumyonyesha mtoto katika kisa cha kwanza cha iana yake kuwahi kushuhudiwa, watafiti wanasema. Mwanmke huyo mwenye umri wa miaka 30 alitaka kumnyonyesha mtoto baada ya mpenzi wake aliyejifungua kusema hataki kumnyonyesha mtoto huyo, hayoni kwa mujibu wa wa jarida la afya la watu waliojibadili jinsia. Alifanikiwa kunyonyesha baada ya kumeza dawa na kukamua maziwa, ripotihiyo inasema kutoka nchini Marekani. Mtaalamu wa Marekani anasema utafiti huo huenda ukachangia visa zaidi vya wanaume walijibadilisha jinsia kuwa wanawake kunyonyesha watoto. Mwanamke huyo aliyekuwa anapokea matibabu ya kubadili homoni zake mwilini kwa muda wa miaka 6, lakini hajafanyiwa upasuaji kubadili sehemu zake za siri, wakati alipowaomba madaktari wamsaidie atimize lengo lake la kumnyonyesha mtoto. Kabla ya mtoto huyo kuzaliwa, madakatari walimpadawa za miezi mitatu unusu kumsaidia kupata maziwa, kwa kawaida dawa hizo hupewa

DIAMOND PLATINUMZ NA RUGE TENA,WATAJWA NA MGOMBEA UBUNGE KINONDONI

Image
Mgombea ubunge jimbo la Kinondoni kupitia tiketi ya CCM, Maulid Mtulia ameahidi kuwatumia Diamond Platnumz na Ruge Mutahaba kunyanyua vipaji katika jimbo hilo ili kuongeza fursa ya ajira.    Mhe. Mtulia amesema hayo leo Ijumaa Februari 16, 2018 katika viwanja vya Biafra wakati akijinadi kwenye kilele cha kampeni ya uchaguzi mdogo wa jimbo hilo. Hata hivyo, Mtulia amewahakikishia wapenzi wote wa soka jimboni humo kuwa ataisaidia timu ya KMC FC iliyopanda daraja kwenda Ligi Kuu kwa hali na mali ifanye vizuri ili kukuza kwa urahisi vijana wengine wenye vipaji. Kwa upande mwingine Mtulia amesema wakazi wa Kinondoni wasihadaike kwa lolote kuchagua viongozi wa vyama vingine kwani yeye anajua matatizo ya vyama hivyo ndio maana aliamua kuhamia CCM akitokea CUF.

Mgombea Ubunge Maulid Mtulia apiga kura yake

Image
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Maulid Mtulia, amepiga kura asubuhi hii ya Feb. 17, 2018 katika kituo cha Friends Corner huko Kata ya Ndugumbi jijini Dar es Salaam.

Makamuzi Ya Mapacha Watatu Si Mchezo

Image
Jose Mara akiwajibika jukwaani. Mpiga besi gitaa wa Mapacha Watatu Vincent Munisi akiwajibika jukwaani. Chaz Baba Kingunge naye akiwajibika. Wanenguaji wakifanya yao. Bendi ya Mapacha Watatu Music Band chini ya Jose Mara usiku wa kuamkia leo ilifanya makamuzi kwenye ukumbi wa Safari Pub, Mtoni Kijichi jijini Dar. Katika onesho hilo Bendi hiyo ilifanya makamuzi ya nguvu ambapo leo Jumamosi itafanya makamuzi Ukumbi wa Meeda uliopo Sinza Mori jijini Dar.