Posts

Showing posts from July 25, 2016

Waziri Mkuu: Nitahamia Dodoma Septemba Mwaka Huu

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  alipokuwa akiwasalimia na kuwashukuru mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma mapema leo asubuhi  waliojitokeza kushuhudia  maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa yaliyofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa, mjini Dodoma. *Asema akishahamia, Mawaziri na Naibu Mawaziri wote wafuatie mara moja WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema atahamia Dodoma ifikapo Septemba, mwaka huu kuonyesha kuwa Serikali imedhamiria kutekeleza ahadi ilizotoa kwa wananchi. Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Jumatatu, Julai 25, 2016) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mkoa wa Dodoma na kuwashukuru kwa ushiriki wao kwenye maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa zilizofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa, mjini Dodoma. “Jana nilimwita Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu na kumwambia akamilishe matengenezo kwenye nyumba yangu kwa sababu ninataka kuhamia Dodoma ifikapo Septemba,” amesema na kushangiliwa na mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma waliohudhuria maadhimisho hayo.

Mtuhumiwa Mauaji ya Mwangosi Akutwa na Hatia.

Image
Daud Mwangosi. Mahakama Kuu Kanda ya Iringa leo imemtia hatiani, Pacificius Cleophace Simon ambaye ni mtuhumiwa wa mauaji ya aliyekuwa  mwandishi wa habari wa Channel Ten na Mwenyekiti  wa Chama cha Waandishi wa  Habari Mkoa  wa  Iringa, Daud Mwangosi kwa kuua bila kukusudia. Mahakama imesema itatoa hukumu ya kesi hiyo keshokutwa Julai 27, mwaka huu. Pacificius anatuhumiwa kumuua Mwangosi katika tukio lilitokea katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi Mkoani Iringa Septemba 2, 2012.

Babu Seya taabani

Image
yaStori: Elvan Stambuli, Wikienda DAR ES SALAAM: Mwanamuziki nguli nchini anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking ‘Babu Seya’ anadaiwa yu taaban ambapo amekimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa matibabu. Mwandishi wetu alimshuhudia Babu Seya akiwa Muhimbili chini ya ulinzi wa askari magereza watatu na wafungwa wengine watano katika Jengo la Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) huku akiwa amedhoofu. Haikuweza kujulikana mara moja ugonjwa uliosababisha Babu Seya ahamishiwe Muhimbili kwa matibabu kwa sababu Jeshi la Magereza lina hospitali yake na mwandishi alipoomba kwa mmoja wa askari magereza ili aweze kumsalimia mwanamuziki huyo, hakupewa ruhusa. Baadhi ya wananchi waliomshuhudia mwanamuziki huyo akiwa Muhimbili na kuingizwa katika chumba cha daktari namba 112 walisema, anavyoonekana ni dhahiri ni mgonjwa kwa sababu hakuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake. “Nguza (Babu Seya) mara nyingi huwa mchangamfu lakini leo ameku

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 25.07.2016

Image

MAGAZETI YA UDAKU LEO TAREHE 25/7/2016

Image