Posts

Showing posts from January 7, 2014

MWENYEKITI WA CHADEMA TEMEKE ALIYEPIGWA NA KUUMIZWA USIKU WA KUAMKIA LEO AHAMISHIWA MUHIMBILI KWA MATIBABU ZAID

Image
  MWENYEKITI WA CHADEMA WILAYA YA TEMEKE JOSEPH YONA AHAMISHIWA MOI MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Temeke na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Joseph Yona (33), aliyepigwa na watu wasiojulikana kisha kutupwa kwenye eneo la Ununio Kawe jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo, ametolewa wodini katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuhamishiwa katika Kitengo cha Mifupa Muhimbili. ShareThis Copy and Paste

MWANAMKE (MTANZANIA) ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE WA MWALIMU NYERERE

Image
 PICHA KUTOKA MAKTABA MWANAMKE wa Mtanzania, Salama Omari Mzale , amekamatwa jana- katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam akisafirisha dawa za kulevya kwenda nchini China. Hadi leo saa nane mchana amekwishatoa kete 27 kwa njia ya haja kubwa.   Mwanamke huyo mkazi wa Mbagala Kongowe, anaendelea kutoa kete hizo katika vyoo vya Uwanja wa Ndege.   Hadi saa 1 jioni (mida ya Tanzania); mwanamke huyu amekwishashusha kete 63

MWANAMUZIKI WA NYIMBO ZA INJILI ATENGENEZA VIDEO YAKE YA MUZIKI HUKU AKIWA MTUPU KAMA ALIVYOZALIWA NOOMA KWELIKWELI..! CHEKI HAPA MAPICHA 50 YA AIBU TUPU

Image
''Maheeda'' Sijui alikusudia nini Dada huyu?..

MH. ZITTO KABWE AIBUKA KIDEDEA KATIKA KESI YAKE DHIDI YA CHADEMA

Image
Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Zitto Kabwe ameshinda kesi yake aliyoifungua akiitaka Kamati Kuu ya Chadema kutojadili Uanachama wake hadi kesi ya msingi aliyoifungua itakaposikilizwa.

JACKIE CLIEF AKUMBWA NA MAZITO ZAIDI, CHINA ... FULL DATA ZIPO HAPA Stori:

Image
HABARI mpya za supastaa modo wa Bongo aliyedaiwa kukamatwa na madawa ya kulevya ‘unga’ Macau, China, Jacqueline Patrick ‘Jack’(pichani) zinazidi kumuumiza mrembo huyo. Jacqueline Patrick ‘Jack’. Mrembo huyo alikamatwa Desemba 19, mwaka jana katika Uwanja wa Ndege wa Macau akitokea Bangkok, Thailand akiwa na kete 57 (kilo 1.1) za unga aina ya heroin tumboni zikiwa na thamani ya shilingi milioni 300.  TAARIFA MBICHI Taarifa mbichi kabisa zinadai kwamba, Jack amepewa mwaka mmoja na nusu (siku 447) ajifunze lugha inayozungumzwa na watu wa Macau (Kireno) ambayo ndiyo itakayotumika mahakamani wakati kesi yake itakapoanza kuunguruma. Dawa za kulevya alizokutwa nazo Jack Patrick. Sheria ya kisiwa hicho inasema kuwa mshitakiwa yeyote atakayefikishwa kortini, kesi yake haitasikilizwa mpaka majaji wakubali kwamba anajua lugha hiyo na si kinyume na hapo. Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, mwalimu maalum anayejua Lugha za Kiingereza na Kireno ndiye atakayemfundisha Jack mpaka at

KATIKA ILE SKENDO YA LUCCI NA JOKATE KUTOKA KIMAPENZI..!! HUU NDIO MCHAPO MZIMA KUHUSU WAO..!!

Image
Sehemu ya video ya wimbo wa "dada kaka" iliyozua utata kuhusu mahusiano ya wawili hawa.. Mtu wangu wa nguvu unaweza kujiuliza huyu shemeji yetu alikuwa na hali gani kipindi kifupi kilichopita wakati Kaka Dada,Lucci Jokate ndiyo headline kila sehemu. Lucci anaongezea,”Unajua ukishakuwa kwenye mapenzi na mtu anayejitambua na anafahamu kazi yako. Basi atafahamu kabisa entertainment inahitaji vitu tofauti ili kufanikisha. So mimi na yeye tuliongea kwamba muda huu tunaitoa kazi ya kaka dada na plan nzima alikuwa anaijua. So hakukuwa na tatizo lolote” Kama unataka kujua upande wa pili wa Lizzyblazzer, Lucci anatuelezea kuhusu mchumba wake,”Lisa ni director wa kampuni yetu mimi na yeye inaitwa  Tsere. Kazi tunayofanya ni creative and marketing, pia anafanya kazi ya HR kwenye hii kampuni”   Oky, so kumaliza mawazo mengi ambayo watu walikuwa nayo kuhusu Jokate na Lucci. Kaka Dada ni kaka na dada kweli, ule ulikuwa wimbo tu. Tunasubili Jokate na yeye atuwek

BINADAMU SASA TUMEZIDI KWA MATUKIO YA AJABU NA YA AIBU: TAZAMA PICHA BINTI AKIVUNJA AMRI YA SITA NA NGURUWE BAFUNI!!!! CHEKI HAPA

Image

KIKAO CHA KAMATI MAALUM YA CCM (NEC) ZANZIBAR CHAFANYIKA

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinnduzi,pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Wazee wa Chama cha Mapinduzi alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja jana, kuhudhuria katika Kikao cha Kamati Maalum ya CCM (NEC) kilichofanyika jana,(kushoto) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] Wajumbe wa Kikao cha Kamati Maalum ya CCM (NEC) wakipitia mada mbali mbali zilizoingizwa katika makbrasha waliyopewa katika kikao kilichofanyika jana katika ukumbi Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] Wajumbe wa Kikao cha Kamati Maalum ya CCM (NEC) wakifahamishana jambo wakati wa kikao cha siku moja cha  Kamati Maalum ya CCM (NEC) kilichofanyika jana katika ukumbi wa Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] Wajumbe wa Kikao cha Kamati Maalum ya CCM (NEC) wakimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyek

Alichokisema Diamond kuhusu yeye na Wema Sepetu na movie yao 2014.

Image
Diamond alidondoka kwenye Exclusive interview ya XXL ya Clouds FM na kuyajibu maswali ya Raymond Mshana ambae ndio alikua anaifanya XXL kwa siku hii ya January 6 2014. Kwenye show ya Xmas Diamond alifanya show yake kwa ajili ya watoto Leaders Dar es salaam ambapo baadae vyombo vya habari vilimkariri akitangaza kwamba Wema Sepetu ndio mpenzi wake wa sasa. Kwenye XXL Diamond amekwepa kulijibu hilo swali ila akamzungumzia Wema na uwepo wake pamoja na movie yake ambayo wamecheza pamoja na inatarajiwa kutoka mwaka huuhuu wa 2014. Maelezo zaidi kuhusu alichosema yako kwenye hii video ya dakika tatu hapa chini www.millardayo.com