Posts

Showing posts from January 13, 2016

Edward Mordrake; Binadamu Mwenye Sura Mbili.

Image
Edward Mordrake NI vigumu kuamini!  Edward Mordrake ni Mwingereza mashuhuri wa karne ya 19 ambaye alijinyakulia tuzo za Nobel. Mordrake aliyetokea kwenye ukoo mashuhuri na wenye hadhi kubwa nchini humo, alitambulishwa zaidi kwa sura zake mbili, moja ikiwa kwenye uso wake wa kawaida na nyingine nyuma ya uso (kwenye kisogo). Cha kushangaza zaidi inasemekana kuwa sura yake ya kisogoni haikuweza kula wala kuongea chochote na hata ikijaribu kuongea maneno yalikuwa hayasikiki lakini iliweza kulia, kucheka na kusikia kila neno. Sura yake ya mbele ya uso imeelezwa kuwa ilikuwa ni nzuri na ya kuvutia  (handsome). Watu waliomuona na kuzungumza naye, wanamsifu Mordrake kwa uzuri wa sura yake ya usoni na tabasamu lake, lakini balaa lipo kwenye sura yake ya kisogoni ambayo ni ya kutisha na  inayofanana na sura ya “bibi kizee mchawi”. Simulizi za wafanyakazi wa jumba la kifahari alimoishi Mordrake, zinatolewa kwa siri, ambapo zinaeleza hali ya maisha ya huzuni ya kijana huyo

Taswira za sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikagua gwaride la Vikosi vya Ulinzi liliandaliwa rasmi katika kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,zilizofanyika jana katika Uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi wakati wa kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Salim Ahmed Salim. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein mara alipowasili katika kilele cha sherehe za m

Wema Hamjui Mwenye Mimba

Image
Wema Sepetu ‘Madam’ Na Mwandishi Wetu, Risasi DAR ES SALAAM: Habari zinazosambaa kwa kasi ya ajabu kama moto wa kifuu zinaeleza kuwa, mtoto mzuri ndani ya Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ mbali na taarifa za kuwa mjamzito, hadi sasa bado yupo kwenye wakati mgumu kuweza kutegua kitendawili cha nani mmiliki halali wa kiumbe kilichopo tumboni mwake, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili. Hivi karibuni, magazeti tofauti ya Global Publishers ndiyo yalikuwa ya kwanza kuripoti kuhusu uwepo wa mimba ya mlimbwende huyo asiyechuja Bongo, ambapo awali, vyanzo mbalimbali vilieleza kuwa mhusika ni mbunge mmoja machachari ambaye ndiye anayemuweka Wema mjini kwa sasa.   Kitumbo cha Wema Sepetu MAJIBU YA WEMA ALIPOBANWA Kwenye habari ya awali iliyoripotiwa na gazeti la Ijumaa, Wema alipotafutwa kusomewa mashitaka yake kuwa ana ujauzito wa mbunge huyo, kupitia simu ya shosti wake, Aunt Ezekiel, staa huyo hakutaka kufunguka sana kuhusu mbunge huyo zaidi ya kusema; “ndiyo

PICHA ZA HALFA FUPI YA KUMPONGEZA MBWANA SAMATTA HYATT REGENCY

Image
 Serikali immempatia zawadi ya kiwanja na pesa ambazo thamani yake haijajulikana mchezaji bora wa Afrika Mbwana Samatta, Hayo yalisemwa jana na Mgeni Rasmi katika halfa hiyo Waziri William Lukuvi. Sherehe hizo zilifanyika  kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar.  Waziri wa Michezo Nape Nnauye akiwa na wazazi wa Mbwana Samatta  Mwakilishi wa Vodacom akitoa neno  Mchezaji Thomas Ulimwengu akifurahia jambo na mdau.  Mbwana Samatta akimpa zawadi ya jezi Waziri Lukuvi

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 13.01.2016

Image
MAGAZETI YA UDAKU LEO   MAGAZETI YA MICHEZO NA BURUDANI