Posts

Showing posts from November 28, 2017

Vurugu Zatanda Kenyatta Akiapishwa, Polisi Wafunga Mtaa Kuzuia Mkutano wa NASA

Image
Polisi wakiimarisha ulinzi eneo hilo. MTAA wa Jacaranda jijini Nairobi, Kenya, leo umefungwa na polisi ili kuzuia mkutano wa umoja wa vyama vya upinzani nchini humo, National Super Alliance (NASA) uliopangwa kwa ajili ya kuwakumbuka wafuasi wake 27 waliouawa wakati wa maandamano ya kupinga uchaguzi wa marudio uliofanyika zaidi ya wiki moja iliyopita. Mataili yakiwa yamechomwa moto. Mkutano huo ulipangwa kufanyika leo ambapo Rais Uhuru Kenyatta ameapishwa kwa kipindi cha pili katika uwanja wa michezo wa Kasarani. Chumba vya kutunzia maiti katika jiji hilo pia kimefungwa na polisi ambapo watu hawatakiwi kufika hapo. Hali ilivyokuwa eneo la tukio. Polisi waliokuwa na zana zote za kuzuia fujo wamekuwa wakirusha mabomu ya machozi sehemu nyingi yakiwemo maeneo ya wafuasi wa NASA ambao wamefunga barabara kadhaa jijini humo. Wafuasi wa NASA wakipambana na polisi. Mpinzani mkuu nchini humo, Raila Odinga, amepinga mipango ya kumwapisha katika nafasi ya urais, a

DIAMOND PLATINUMZ AIBUA MAPYA,AWASHA MOTO UPYA,WEMA SEPETU,ZARI THE BOSS LADY NA HAMISA KUMEKUCHA KUPITIA WIMBO WAKE MPYA- "SIKOMI"

Image
Wakati msanii wa muziki wa Bongo Flava, Diamond Platnumz ameachia ngoma mbili kwa wakati moja ambazo ni Sikomi na Niache, ngoma ya kwanza imekuwa na nguvu na mapokeo makubwa kutokana na ujumbe uliyomo ndani yake.Katika ngoma hiyo ‘Sikomi’ Diamond amezungumzia maisha yake ya kimahusiano na wanawake maarufu kama Wema Sepetu, Penny na baby mama wake, Zari The Boss Lady.Wimbo huo wenye dakika 3:58 Diamond anaeleza baada ya kupambana kwa kipindi kirefu hadi kuja kutoka kimuziki aliamini pengine maisha yake ya kimahusiano yangekuwa vizuri kitu ambacho anakiri hakijamtokea tangu pale alipokutana na mrembo kutoka Bongo Movie. Licha ya kutomtaja mrembo huyo bila shaka anamzungumzia Wema Sepetu kwani ndiye mrembo pekee wa Bongo Movie aliyeanza kudate naye na couple yake kuwa na nguvu zaidi.Hata hivyo katika verse ya pili ya ngoma hiyo ndipo ameweka wazi kuwa anayemzungumzia ni Wema Sepetu kwa kueleza licha ya kumpenda sana lakini bado aliusumbua moyo wake. MOYO ALIUPATI

Mmiliki wa shule ashitakiwa kwa mauaji

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Moshi imewasomea shitaka la mauaji watu watatu wanaotuhumiwa kumuua kijana Humphrey Makundi aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo Moshi. Watuhumiwa hao ni mmiliki wa shule ya Scolastica, Edward Shayo mwenye miaka 63, mlinzi wa shule hiyo Hamis Chacha mwenye miaka 28 na Laban Nabiswa mwenye miaka 37. Upande wa Jamhuri katika shitaka hilo lililofika mbele ya Hakimu Mkazi, Julieti Mawore umewakilishwa na Mwanasheria Kassim Nassiri akisaidiana na Wakili wa kujitegemea, Faygrace Sadallah. Akisoma maelezo ya hati ya mashitaka mbele ya mahakama hiyo, Nassiri alieleza kuwa mnamo Novemba 6 mwaka huu mshitakiwa wa kwanza, Hamis Chacha wa pili Edward Shayo na wa tatu Laban Nabiswa, walimuua kwa kukusudia mtu aitwaye Humphrey Makundi. Aidha washitakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikliza shitaka la mauaji huku akiwataka kusubiri kufany

Biblia ya Jomo Kenyatta Yatumiwa Kumwapisha Uhuru Kenyatta

Image
Mzee Jomo Kenyatta akiapishwa kuwa Rais wa Kwanza wa Kenya mwaka 1964. KATIKA hafla ya kuapishwa kwa Rais wa Kenya na Makamu wake, imeelezwa kuwa, nakala ya Biblia iliyotumiwa kumwapisha Rais Uhuru Kenyatta ni ile iliyotumiwa kumwapisha kwa Rais wa kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta ambaye ni baba’ke rais wa sasa wakati nakala ya Katiba ni iliyotiwa saini wakati wa kurasmishwa kwa Katiba ya sasa mwaka 2010 uwanjani Uhuru Park. Biblia hiyo ilitumika mwaka 1964 kumwapisha Jomo Kenyatta, 2013 kumwapisha Uhuru kenyatta na leo Novemba 28, 2017 kumwapisha Uhuru Kenyatta katika Uwanja wa Kasarani. Uhuru Kenyatta akiapishwa kuwa Rais wa Kenya mwaka 2013. Msajili Mkuu wa Mahakama, Anne Amadi amemwapisha Uhuru Kenyatta kuwa Rais wa Kenya kwa mhula wa miaka mingine mitano ijayo na William Ruto kuwa Makamu wake. Rais Kenyatta: “Nitatekeleza majukumu yangu, na wajibu wangu katika Ofisi ya rais wa Kenya, na kwamba nitatenda haki kwa wote kwa mujibu wa Katiba hii kama il

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU AMWAKILISHA JPM KUAPISHWA KWA KENYATTA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo asubuhi tarehe 28 Novemba, 2017 amewasili Mjini Nairobi nchini Kenya ambako anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli katika sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta. Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba amepokelewa na Mhe. Balozi Robinson Njeru Githae wa Kenya na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Dkt. Pindi Chana. Sherehe za kuapishwa kwa Mhe. Rais Uhuru Kenyatta zinafanyika katika uwanja wa Moi Kasarani Mjini Nairobi. Gerson Msigwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU Nairobi 28 Novemba, 2017. Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akitia saini kitabu cha wageni baada ya kuwasili Nairobi, kumwakilisha Rais Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa Rais

Kauli ya zitto Kabwe baada ya Rias Magufuli kutohudhuria kuapishwa kwa Kenyatta

Image
Zitto Kabwe amefunguka na kusema kitendo cha Makamu wa Rais Mhe. Samia kupokelewa na Balozi Kenya ni ishara kuwa mahusiano ya Tanzania na Kenya hayapo vizuri na kudai Rais Magufuli kutokwenda kwenye sherehe za kuapishwa Kenyatta inaweza kueleweka. Zitto Kabwe amesema hayo kupitia mtandao wake wa twitter na kusema kitendo cha Rais Magufuli kutohudhuria kwenye sherehe za kuapishwa kwa Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta inaweza kueleweka kwani kiongozi huyo hakuweza kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame. "Makamu wetu wa Rais kupokelewa na Balozi ( sio hata Waziri wa Mashauri ya Kigeni au Waziri mwengine) ni dalili kuwa mahusiano yetu yanalega lega. Rais kutokwenda Kenya inaweza kueleweka maana hata Rwanda hakwenda kwenye uapishaji wa Paul Kagame" aliandika Zitto Kabwe.

ANGALIA PICHA MAGARI YALIYO FICHWA PORINI NA ALIYEKUWA RAIS WA GAMBIA

Image
Rais wa The Gambia Yahya Jammeh alilazimika kuyaficha magari yake ya kifahari yapatayo 13 katika msitu wa Kanilai, baada ya kubanwa sana kuhusu ufujaji wa fedha……..Magari hayo (Yakiwemo Rolls Royce 2 na Mercedece Benz 3) yaligunduliwa na jeshi la ECOWAS