Posts

Showing posts from May 9, 2016

EXCLUSIVE: Rachel Kizunguzungu amrudia Mungu… ni baada ya yote aliyofanya na kupitia.

Image
Mwimbaji Rachel ambaye ujazo wa jina lake uliongezeka baada ya kujiunga na nyumba ya vipaji Tanzania ( THT ) na kuanza kuachia nyimbo zake, amekaa kwenye Excluvie na mtangazaji wa Amplifaya ya CloudsFM Millard Ayo na kueleza kilichotokea mpaka akakwama na kukaa kwenye nchi ya watu kwa zaidi ya miezi saba, ishu yake ya kuvuta bangi na mengine. KUHUSU KUMRUDIA MUNGU:   Ni kweli nimemrudia Mungu, ni maamuzi ambayo nimeyafanya mwenyewe baada ya kuona vitu ni vilevile, dunia ni ileile na watu ni walewale ndio maana nikaona sio vibaya nikaja na upande mwingine lakini hii haimaanishi kwamba nitakua nafanya muziki wa Injini, nitaendelea na bongofleva lakini muda mwingi nitautumia kanisani. KUHUSU OMAN: ‘Ni kweli nimekaa nchini Oman kwa zaidi ya miezi saba, nilikwenda kwa ajili ya kufanya shows tu lakini nikapata tatizo kwenye VISA yangu, nilifanya show za kuandaa mwenyewe ikafanikiwa mwanzoni lakini baadae hali ikabadilika, nilikua na VISA ya miezi mitatu na nikae

WEMA SEPETU AFUNGUKA JUU YA MCHEZAJI HARUNA NIYONZIMA

Image
Ibrahim Mussa, Dar es Salaa BAADA ya Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Sagrada Esperanca ya Angola, msanii wa filamu nchini, Wema Sepetu, amefunguka kuwa hajui ni kwa nini amekuwa akimpenda kiungo wa timu hiyo, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima. Katika mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Afrika uliopigwa juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, Championi Jumatatu lilimshuhudia msanii huyo ambaye pia alikuwa Miss Tanzanani mwaka 2006, akiwa amekaa Jukwaa la VIP A kwa ajili ya kutoa sapoti kwa timu yake hiyo. Akizungumza na Championi Jumatatu, Wema alisema kuwa upendo wake kwa kiungo huyo ni mkubwa mno kiasi kwamba hajui kwa nini inakuwa hivyo, lakini akaongeza kuwa inawezekana kuwa ni kutokana na uwezo wake anaouonyesha uwanjani ambapo katika mchezo huyo aliwapa wakati mgumu viungo wa Esperanca. “Mimi ni shabiki wa Yanga damu kabisa, tangu nazaliwa na utabiri wangu umeenda vizuri, maana nilisema kabla ya mchezo kuwa tutashinda na imekuwa kweli, ushindi huo n

RAIS DKT MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI YA KUPAA KWA BWANA KATIKA PAROKIA YA TOLEO LA BWANA JIMBO LA ARUSHA

Image
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia waumini aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.  Sehemu ya waumini wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alipokuwa akiwsalimia  aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia na wanakwaya  aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimia baadhi ya watawa aliposhiriki ibada ya Jumapili ya Kupaa kwa Bwana katika Parokia ya Toleo la Bwana jimbo la Arusha leo Mei 8, 2016.    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Maguful

WAZIRI WA MAGUFULI AKWAA KISIKI JIMBONI KWAKE,APEWA MAJI MACHAFU ANYWE.

Image
Kijiji cha Nala na vitongoji vyake juzi walimpelekea maji machafu Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Anthony Mavunde wakimtaka ayanywe kwa kuwa ndiyo wanayotumia. Mavunde alikutana na mkasa huo muda mfupi alipoingia kwenye kijiji hicho umbali wa kilomita tisa nyakati za jioni, ambako wakazi wa eneo hilo walikuwa wakimsubiri tangu asubuhi. Mama mmoja aliyekuwa eneo hilo, alifika na chupa ya maji akimtaka Naibu Waziri ayaonje mbele yao, kwani nao ni binadamu kama yeye na wanayatumia, lakini Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini, Paul Luhamo alimzuia kuyanywa.Pamoja na taarifa ya kijiji iliyotolewa na Ofisa Mtendaji wa Kata, Mathias Ndologa, wakazi hao walilipuka na kupiga kelele wakiipinga taarifa hiyo kwamba iligusa kwa juu matatizo yao, lakini ikaacha jambo kubwa la maji. Kwenye risala yake, Ndologa alikuwa ameelezea suala la maji, umeme, miundombinu na upungufu wa madawati, lakini kelele zilizidi kutoka kw