Posts

Showing posts from December 6, 2016

Ajali ya Lori na Hiace Yaua Watu 9 na Kujeruhi 18, Iringa

Image
   IRINGA: Watu tisa wamefariki dunia na wengine 18 kujeruhiwa kufuatia ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Ifunda mkoani Iringa jana Desemba 5, 2016 baada ya lori kugongana na gari dogo la abiria aina ya Toyota Hiace.   Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amesema dereva wa lori lililopata ajali lililokuwa likitokea Mbeya kuelekea Dar es Salaam, alishindwa kufunga breki na kuigonga Hiace iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara.   “Lori limeharibika kabisa na Hiace pia imeharibika vibaya,” alisema RC Masenza.   “Lori hilo liliposhindwa kufunga breki liliigonga Hiace ambayo ilikuwa na abiria na kwenda mbele na kisha kugonga watembea kwa miguu.”  RC Masenza alisema katika ajali hiyo iliyotokea jana jioni, madereva wa magari hayo wote wamejeruhiwa na wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Iringa pamoja na majeruhi wengine. “Dereva mmoja yupo chumba cha upasuaji kwa kuwa mguu wake umevunjika na mwingine yupo wodini,” alisema RC Masenza.

Zari Kujifungua Soon, Apelekwa Hospitali Sauz, Diamond na Mama Yake Waungana Naye

Image
   HABARI ya town kwa sasa ni kuhusu kujifungua kwa mpenzi wa mwanamuziki nguli wa Bongo Fleva nchini Diamond Platnumz, Zarinah Hassan a.k.a Mama Tiffah. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond anayetarajia kupata mtoto wa kiume ametupia video inayomuonesha Zari akiwasili katika hospitali ambayo haikutajwa jina iliyopo nchini Afrika Kusini ikionyesha dhahiri kwamba yupo tayari kujifungua mtoto wa pili wa nguli huyo wa Bongo Fleva ambapo aliandika ni Jina gani vile mmesema nimpe? Zari alikuwa kwenye kiti cha kubebea wagonjwa “Wheel Chair” wakati akifikishwa hospitalini hapo huku pembeni akiwepo mama mkwe wake, Sandra Kassim ambaye ni mama mzazi wa Diamond pamoja na wahudumu wa hospitali hiyo. Mapema leo, staa huyo aliweka picha yake akiambatana na mama yake mzazi wakiwa kwenye ndege wakielekea Afrika Kusini kwa ajili ya kuwa karibu na Zari huku akiandika maneno yafuatayo; Na mama Chibu D Chibu De … flying to our new Second home, South africa For my

PICHA: SAFARI YA MWISHO YA FIDEL CASTRO WA CUBA

Image
Mwili wake wa aliyekuwa Rais wa Cuba umechomwa moto hadi kuwa majivu kama alivyotaka, katika sherehe ya kibinafsi, na majivu yake yamezungushwa katika msafara maalumu kote nchini kabla ya kuzikwa katika Makaburi ya Mji wa Santiago leo Desemba 4, 2016. Cuba inaadhimisha siku tisa za maombolezo kufuatia kufariki kwa Fidel Castro akiwa na umri wa miaka 90. Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwekwa garini tayari kwa kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini kabla ya kuzikwa katika Makaburi ya Mji wa Santiago Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Gari maalumu likiwa na Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Wananchi wakijipanga kuaga Kasiki lenye majivu ya Fidel Castro yakiwa garini kuzungushwa katika msafara maalumu kote nchini Cuba.