Posts

Showing posts from April 20, 2018

NDOA YA KIBA YAACHA VILIO!

Image
DAR ES SALAAM: Wakati mkali wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘AliKiba’ akitarajiwa kuangusha bonge la sherehe baada ya kufunga ndoa nchini Kenya, ndoa hiyo imedaiwa kuacha vilio vikali kwa wanawake ambao waliwahi kushea kitanda na msanii huyo, Ijumaa lina mchapo kamili. Kiba alitarajiwa kufunga ndoa hiyo jana mjini Mombasa nchini Kenya kisha kufuatiwa na bonge la sherehe mjini humo huku sherehe nyingine bab’kubwa ikitarajiwa kufanyika nchini mwishoni mwa mwezi huu. MTU WA KIBA ANENA Mtu wa karibu na AliKiba, amepenyeza habari kuwa, licha ya kwamba wao wanasherehekea harusi ya mkali huyo anayetamba na Wimbo wa Seduce Me, nyuma yake kuna vilio vingi kutoka kwa wanawake ambao walitembea na Kiba kabla. “Kama unavyojua Kiba alishazaa watoto wanne, wale watoto kila mmoja ana mama yake. Sasa mama zao wanalia maana nao walikuwa wana matarajio ya kuolewa,” alisema mtu huyo wa karibu aliyeomba hifadhi ya jina na kuongeza: BIBI HARUSI NJIA PANDA “Kimsingi wamem

Wenger Aondoka Rasmi Arsenal

Image
KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger ameridhia kubwaga manyanga mwishoni mwa msimu huu baada ya majadiliano ya kina na uongozi wa klabu hiyo kongwe duniani. “Baada ya kutafakari kwa kina kufuatia mazungumzo na klabu yangu, u mefika wakati sasa nikae pembeni mwisho wa msimu huu, nina furaha sana kwa muda wote niliokaa hapa klabuni. “Ninawashukuru wafanyakazi wenzangu, wachezaji, wakurugenzi na mashabiki kwa kuifanya klabu hii kuwa spesho, nimeitumikia kwa miaka mingi” amesema Wenger kwenye taarifa yake rasmi leo Ijumaa. LONDON, England.

Breaking News: Masogange Afariki Dunia

Image
Video queen maarufu nchini, Agnes Gerald ‘Masogange’ amefariki dunia hivi punde (leo Aprili 20, 2018) katika Kituo cha Huduma za Afya cha Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar es Salaam baada kuzidiwa ghafla jana na kukimbizwa hospitalini hapo.  Mwili wa marehemu ukiwekwa kwenye gari kupelekwa Muhimbili kuhifadhiwa. Taarifa ambazo hazijathibitishwa, zinadai Masogange alifikishwa Hospitalini hapo akisumbuliwa na homa ya matumbo na tatizo la kupungukiwa na damu. Global Publishers imefika hospitalini hapo na kujionea umati wa watu waliokusanyika wakilia kwa uchungu kumpoteza msanii huyo. Dkt. Kihama Ngoma ameithibitishia Global Publishers na kusema taarifa zaidi zitatolewa baadaye. Tayari mwili wa marehemu Masogange umehaimshwa hospitalini hapo na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kuhifadhiwa. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi, AMEN!.

Mfalme Mswati III Abadili Jina la Nchi Yake

Image
MFALME Mswati wa III wa Swaziland amebadilisha jina rasmi la taifa hilo kutoka Swaziland na kuliita Ufalme wa eSwatini (The Kingdom of Swaziland)  wakati wa maadhimisho ya siku yake ya kuzaliwa ambapo ametimiza miaka 50 na wakati huo huo taifa hilo likiadhimisha miaka 50 ya uhuru wake. Jina hilo jipya, eSwatini, lina maana ya ardhi ya Waswaz na limetumiwa rasmi na Mfalme Mswati wa III kwa miaka mingi. eSwati ni jina ambalo mfalme alilitumia alipokuwa akihutubia katika mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa mwaka 2017 na katika ufunguzi wa bunge la nchini mwake mwaka 2014. Mfalme Mswati ni miongoni mwa wafalme wa mwisho wa duniani waliobaki na ametawala tangu mwaka 1986.  Mswati III kwa sasa ana wake 15 akiwa anaifuata rekodi ya Baba yake aliyekuwa na wake 125. Wanaharakati wa kutetea usawa wa jinsia wanasema mfumo wa utawala wa nchi hiyo ni wa kushangaza na unawabagua wanawake. Mswati III ametoa sababu kuu ya kubadilishwa kwa jina la nchi yake kuwa kila aendapo katika

Siwa ya Bunge yakutwa kwenye Flyover

Image
Baada ya watu wenye silaha kuvamia Bunge la Senate la Nigeria na kuiba siwa juzi, hatimaye imekutwa chini ya Barabara ya Juu ‘flyover’ Jijini Abuja baada ya kuonwa na mwananchi aliyekuwa akipita maeneo hayo. Inadaiwa watu hao waliongozwa na Mbunge Ovie Omo-Agege ambaye amefungiwa kuhudhuria vikao vya Bunge kutokana na tuhuma hizo. Hata hivyo, Msemaji wa Serikali ya Nigeria ameeleza kuwa kitendo hicho ni uhaini na inaashiria kuwa mtuhumiwa, Omo-Agege alikuwa akijaribu kupindua moja ya mihimili ya Serikali ya Nigeria. Siwa ni ishara ya mamlaka ya Bunge hilo na Sheria haziwezi kupitishwa bila kuwepo kwa kifaa hicho. Licha ya kitendo hicho, Bunge liliendelea na kazi yake kwa kutumia Siwa ya ziada iliyokuwepo bungeni hapo ambapo kabla ya hapo Seneta wa Kaduna, Shehu Sani alivua mkanda wake na kuuweka sehemu ya Siwa hiyo. Aidha, Chama tawala, APC kimeita tukio hilo kuwa ni shambulio kwa Demokrasia ya nchi hiyo na kutaka waliohusika kukamatwa. Hadi sasa Seneta Omo-