Posts

Showing posts from June 18, 2016

Wabongo wafungukia simu feki kuzimwa

Image
Stori:  Gladness Mallya, Risasi Jumamosi DAR ES SALAAM: Baada ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ‘TCRA’ kutangaza kuzima simu feki usiku wa Juni 16, mwaka huu, wananchi mbalimbali wa Jiji la Dar, wamefunguka ya moyoni: BARIKI GASTON (MWENGE) “Kuzimwa simu feki kumeniumiza sana na siyo mimi tu wapo wengi hasa wenye hali ya chini japokuwa zina madhara wangetuachia kwa muda mrefu kidogo ili tujipange kwanza.” HIDAYA SAID (MWANANYAMALA) “Serikali ilivyofanya siyo vizuri kwa sababu hali ya maisha ni ngumu, nafanya mama ntilie hapa sina uwezo wa kununua simu orijino, wangetuangalia sisi watu wa vipato vya chini wasingezima ila wangezuia zile zinazoingia nchini lakini hizi tunazomiliki tubaki nazo.” JOSEPH VENANCE (MWENGE) “Suala la simu feki kuzima limetuchanganya sana maana tulishazoea kununua kwa bei rahisi lakini sasa haya ni majanga kwa sababu mpaka upate hela ya kununua simu orijino ni kazi sana lakini inabidi tukubaliane tu hali halisi maana zina madh

Video ya aibu ya Wema yavuja!

Image
Wema Sepetu (kulia) wakati wa hafla hiyo. Stori: Andrew Carlos, Risasi Jumamosi DAR ES SALAAM: Video ya aibu inayomuonesha msanii maarufu wa filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ akicheza kihasara mbele ya mwanaume imevuja, Risasi Jumamosi linayo kibindoni. ‘Klipu’ hiyo ambayo Wema anaonekana akikata mauno huku suruali aliyokuwa amevaa ikimvuka na kuacha wazi sehemu ya makalio yake, ilivujishwa hivi karibuni na mdau mmoja wa burudani ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini. Wema na Igwe wa Pah One wakiyarudi. “Hii video niliichukua siku ya ile eventi ya Christian Bella ya kutimiza miaka 10 pale Escape One. Wakati akicheza na msanii wa Kundi la Pah One aitwaye Igwe, Wema alionekana kama alikuwa amelewa, alikuwa akikata mauno lakini aibu zaidi ilikuwa pale ambapo ile suruali yake ilipomvuka na sehemu ya makalio yake kubaki wazi. “Sidhani kama alikuwa kavaa kufuli, baadhi ya watu waliokuwa wakimkodolea macho walishindwa kuamini kama ni Wema yule wanayemju

Shamsa Ford: Vimini vyangu havimuathiri mtoto

Image
Shamsa Ford Boniphace Ngumije, Risasi Jumamosi DIVA mwenye ‘title’ kubwa Bongo, Shamsa Ford amesema kuwa tangu awe mzazi anajitahidi kuishi maisha ya kistaarabu sana kiasi kwamba hahitaji kuwa na skendo ili kuitunza heshima yake kwa mwanaye wa kiume aitwaye Terry pale ambapo atakuwa kijana. Shamsa na mwanaye. Shamsa alisema hayo wakati akipiga stori mbili-tatu na gazeti hili, alipoulizwa kwa nini anapendelea kuvaa mavazi mafupi alisema kuwa hiyo ni ‘hobby’ yake tangu utotoni, kila mmoja kwenye familia yake anafahamu hilo na wala haihusiani kabisa na malezi ya mtoto. “Mimi nililelewa na mama yangu mkubwa ambaye ameolewa na Mzungu, tangu udogoni alikuwa ananivalisha nguo fupi pamoja na watoto wake. Kwenye familia yetu suala hilo si tatizo wala halihusiani na malezi ya mtoto, ninaimani hata Terry akikua ataliona kuwa ni jambo la kawaida kabisa,” alisema Shamsa.

ALIYEKUWA BEKI WA TP MAZEMBE ATUA SIMBA

Image
Kweli Simba wameamua, tayari beki Janvier Besala Bokungu raia wa DRC, ametua Dar es Salaam kimyakimya ili kumalizana na uongozi wa Msimbazi. Bokungu ni beki wa zamani wa TP Mazembe, kama unakumbuka vizuri ndiye walimchezesha katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba ikakata rufaa kwenye Shirikisho la Soka Afrika (Caf), TP Mazembe wakaondolewa mashindanoni na Simba kupata nafasi ya kucheza na Wydad Casablanca ya Morocco.  “Tayari wametua hapa nchini na wataanza mazungumzo na taratibu nyingine, maana Bokungu alikuwa Esperance ya Tunisia. Mimi ninaamini atasajiliwa Simba maana kiwango chake kipo juu tu,” kilieleza chanzo. Caf, ilitangaza uamuzi wa kuiondoa TP Mazembe Mei 14, 2011 na mechi ikachezwa kwenye uwanja huru wa Petrojet jijini Cairo, Misri, Simba ikatandikwa mabao 3-0, hiyo ilikuwa Mesi 28, 2011.  Bokungu yuko jijini Dar es Salaam pamoja  na kiungo mwingine raia wa DR Congo pia wakisubiri ‘kuonwa’ na makocha au watu maalum kabla ya kusaini mkataba

Mwalimu Afungwa Jela Miaka 90 kwa kuwanajisi wanafunzi

Image
  Mwalimu John Gichia Mugi. Nairobi, Kenya Mwalimu mmoja wa shule ya msingi aliyetambulika kwa jina la John Gichia Mugi mwenye umri wa miaka 23 nchini Kenya amehukumiwa kifungo cha miaka 90 jela kwa kuwanajisi wanafunzi wake wenye umri kati ya miaka 13 hadi 16. Hii ni moja kati ya vifungo vya muda mrefu zaidi kuwahi kutolewa kwa watu wanaowaingilia watoto kijinsia nchini Kenya. Mwalimu John Gichia alishtakiwa kwa kuwabaka wavulana 9 wa shule ya msingi ya Muthiria iliyopo Muran’ga takriban kilomita 120 Magharibi mwa Nairobi nchini humo mnamo Januari na Mei mwaka 2015. Mwalimu huyo atatumikia kifungo cha miaka 10 kwa kila kosa alilotenda yaani kubaka watoto 9, hivyo kufanya jumla ya miaka atakayotumikia jela kufikia 90. Jaji alisema mwalimu walikuwa amesaliti dhamana na imani aliyopewa na wazazi wa wanafunzi hao wachanga ambao alipaswa kuwatunza, inasemekana alikuwa akiwafanyia vitendo hivyo viovu watoto hao baada ya muda wa masomo wa usiku (preps). Wavulana

Mastaa hawa wameachiwa chata, hakijaelewaka!

Image
    Rose Ndauka Mwandishi wetu, Risasi Jumamosi MPANGO au matarajio ya kila mwanadamu ni kuishi katika uchumba, kuolewa kisha kupata watoto! Wapo ambao wamefanikiwa hilo, wapo ambao wamepata kwanza mimba baadaye wakaolewa lakini wapo pia waliopata mimba kabla ya ndoa kisha wakatofautiana na waliowapa, kila mmoja anaishi kivyake. Katika ulimwengu wa mastaa wa kike Bongo, leo nakuletea baadhi ya mastaa ambao wamepata watoto lakini kwa namna moja au nyingine safari yao na waliowapa ujauzito haikufika mbali, ikavunjika. Wapo ambao walipata kabla na wengine baada ya ndoa. Wengi wao huwanadi watoto hao mitandaoni kwa maneno mazuri wakionesha kwamba ndiyo faraja yao baada ya kuachana na wapenzi au waume wao; ROSE NDAUKA Aliingia katika uchumba na Malick Bandawe. Wakafanikiwa kupata mtoto mmoja, uchumba ukayeyuka wakati wawili hao wakiwa katika mchakato wa kuelekea kwenye ndoa. SNURA MUSHI Amefanikiwa kupata watoto wawili; wa kike na wa kiume kwa baba tofauti.

KIKWETE ATEULIWA KUWA BALOZI WA HESHIMA

Image
Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho  Kikwete akipokea barua ya uteuzi kutoka kwa Prof. Kamuzora alipofanya ofisi za CCM Lumumba   Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania awamu ya nne Dkt.Jakaya Mrisho   Kikwete akizungumza na  Prof. Kamuzora alipofanya ofisi za CCM Lumumba

MERCY KITOMARI, MJASIRIAMALI KIJANA ANAYETAKA KUMUONA ‘ROLE MODEL’ WAKE RAIS MAGUFULI

Image
Mjasiriamali kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari wakati akizungumza na Meneja Uendeshaji wa mtandao wa Habari wa  Modewjiblog , Zainul Mzige (hayupo pichani). MJASIRIAMALI kijana na mmiliki wa Nelwa’s Gelato, Mercy Kitomari amesema anatamani kukutana na Rais John Pombe Magufuli kumwelezea haja ya kukutana na wanawake wajasiriamali vijana wamweleze matatizo yao. Amesema Rais baada ya kukutana na makundi mbalimbali ya wafanyabiashara , inafaa akutane na wajasiriamali wanawake vijana ambao wanapita katika magumu mbalimbali . Alisema katika mahojiano hivi karibuni ambayo sehemu yake itachapishwa katika mtandao wa Modewjiblog muda wowote kwamba, rais Magufuli akiwa kama ‘Role Model wake’ katika kujituma, anaweza kuwasikiliza wanawake hao vijana na kusaidia kuwasukuma juu zaidi katika kampeni ya kuiweka Tanzania kuwa nchi ya viwanda. “Nimekuwa nikikutana na wanawake wenzangu ambao wamekata tamaa na wamekuwa wakiniuliza ninawezaje kuendelea,