Posts

Showing posts from April 3, 2016

KIPA WA SIMBA AFUNGIWA MIAKA 10, GEITA GOLD NA POLISI ZASHUSHWA DARAJA

Image
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF),  chini ya Makamu Mwenyekiti wake, Wakil Jerome Msemwa leo imetoa maamuzi ya shauri la upangaji matokeo kwa mechi za Kundi C Ligi Daraja la Kwanza. Akisoma hukumu hiyo baada ya kumaliza kuwahoji viongozi wa klabu na Wenyeviti wa vya vyama vya mikoa husika jana, Wakili Msemwa amesema adhabu hizo zimetolewa kwa kufuata Kanuni za Nidhamu za TFF, na nafasi ya kukata rufaa kwa wahusika juu ya maaamuzi hayo ziko wazi. Klabu za Geita Gold (Geita), JKT Oljoro (Arusha) na Polisi Tabora (Tabora) zimekutwa na hatia ya upangaji wa matokeo na kupewa adhabu ya kushushwa daraja mpaka ligi daraja la pili (SDL) msimu ujao. Upande wa klabu ya JKT Kanembwa FC ya mkoani Kigoma, imeshushwa daraja mpaka kwenye ngazi ya ligi ya mkoa (RCL), baada ya kushika nafasi ya mwisho katika msimamo wa kundi lake, Kundi C. Kamati ya Nidhamu imewafungia maisha kutojihusisha na mpira wa miguu mwamuzi wa mchezo k

BARAKA DA PRINCE NA NAJ WAONYESHEANA MAHABA HADHARANI, CHEKI PICHA HIZI

Image
Couple ambayo inazungumziwa sana kwa sasa kwenye mitandao ya kijamii na hata kwenye media ni ya Baraka Da Prince na Naj, Na hii ni baada ya tetesi kuwa Baraka amekuwa na tabia ya kuwapitia wasanii kimapenzi hadi kutungiwa jina la Zipu Mbovu. Baraka na Naj baada ya kutoka kwenye show ya Friday Night Live ya EATV na EA Radio walienda kujimwaga kwenye kumbi mbali mbali za starehee na ndipo picha hii ikanaswa. Unadhani Baraka na Naj watadumu kwenye mapenzi kutokana na jina walilonalo kwenye tasnia ya muziki?

RAIS DKT. MAGUFULI NA RAILA ODINGA WASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI YA PILI YA PASAKA CHATO MKOANI GEITA.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga wakisali katika kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita. Rais Dkt. Magufuli amesali ibada ya jumapili ya pili ya Pasaka tangu kuchaguliwa kuwa Rais. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Raila Odinga pamoja na Mke wa Raila Bi. Ida Odinga wakifatilia kwa makini mahubiri ya Paroko Padre Henry Mulinganisa katika ibada ya pili ya pasaka Chato Mkoani Geita. Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisali katika kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita. Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisali katika kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita. Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli, Mke wa Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya, Bi. Ida Odinga, Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Raila Odinga pamoja na Rais Dkt. John Magufuli wakifatilia kwa makini mahubiri yaliyokuwa yakitolewa katika kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita. Rai