Posts

Showing posts from November 28, 2016

Machafuko Yanayoendelea Kwenye Kasri ya Mfalme Uganda, Mwandishi wa KTN Akamatwa

Image
Mwandishi wa habari wa runinga ya KTN ya nchini Kenya, Joy Doreen Biira amekamatwa na kuzuiliwa na maafisa wa usalama nchini Uganda jana Jumapili usiku. Vyombo vya habari zinasema Bi Biira alikamatwa pamoja na wengine watano kwa tuhuma za kupiga picha na video kuhusu operesheni ya maafisa wa usalama katika kasri la mfalme wa Rwenzururu na kuzichapisha kwenye mitandao ya kijamii. Wanahabari na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu wametoa wito kwa serikali kumwachilia huru. Hash Tag #FreeJoyDoreen (Mwachilie huru Doreen) kinavuma katika mtandao wa Twitter nchini Kenya. Wanajeshi na polisi walivamia kasri hilo la Mfalme Charles Wesley Mumbere Jumapili. Walinzi wake 46 waliuawa kwa mujibu wa polisi, na wengine 139 wakakamatwa. Mfalme huyo alikamatwa pia na kuzuiliwa makao makuu ya polisi ya wilaya ya Kasese kabla ya kuhamishiwa mjini Kampala. Gazeti la linalomilikiwa na Kampuni binafsi ya Monitor nchini humo linasema mfalme huyo anatarajiwa kukutana

Hatima ya Dhamana ya Godbless Lema Kujulikana Leo

Image
ARUSHA: Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema, leo, anatarajia kujua hatima ya dhamana ya kesi ya uchochezi inayomkabili. Lema anashikiliwa katika mahabusu ya Magereza ya Kisongo mjini Arusha. Wakili wake, Peter Kibatala amesema walikata rufaa chini ya hati ya dharura kuomba Mahakama isikilize kesi hiyo mapema. Amesema waliamua kufuata maelekezo ya Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Sekela Mosha ya kuwataka kukata rufaa. Katibu wa mbunge huyo, Innocent Kisanyage amesema rufaa hiyo itasikilizwa leo saa tatu asubuhi baada ya kukamilisha mambo yanayotakiwa. Lema alirudishwa mahabusu kutokana na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kukataa kupokea ombi lake la kufanya marejeo ya uamuzi wa kunyimwa dhamana. Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mosha alisema uamuzi uliofanywa na Mahakama ya Hakimu Mkazi umeegemea kifungu cha Sheria cha Makosa ya Jinai CPA 148, hivyo kilimtaka mshtakiwa kukata rufaa siyo kuomba Mahakama hiyo kufanye reje

Kiwanda cha Dangote Chasitisha Uzalishaji wa Saruji Mtwara Kutokana na Gharama Kuwa Juu

Image
MTWARA: Kiwanda cha Saruji cha Dangote huko Mtwara kimesitisha uzalishaji kutokana na gharama kuelemewa na gharama za uendeshaji hivyo kuwaacha watumiaji wake njia panda. Hayo yalisemwa na mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho Harpeet Duggal Walisema wapo na mazungumzo na serikali kuona namna ya kutatua changamoto hiyo Mwezi uliopita mkurugenzi huyo alilalamika uamuzi wa serikali kupiga marufuku kiwanda chake kuingiza makaa ya mawe kutoka Afrika Kusini na kutakiwa kutumia ya Liganga ambayo alidai yapo chini ya kiwango na bei ghali. Pia alilalamikia shirika la maendeleo ya petroli TPDC kwa kushindwa kuwauzia gesi kwa bei rahisi wakati inazalishwa mkoani Mtwara Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alidai madai yao ya gharama kuwa juu ni ya uzushi. CREDIT: NIPASHE