Posts

Showing posts from March 18, 2016

Jinsi ya Kuangalia kama Simu ni Feki

Image
  Hivi karibuni zilisambaa taarifa kwamba simu feki zote nchini Tanzania zitazimwa ifikapo mwezi Juni mwaka 2016, makala hii itakuonesha jinsi ya kuangalia kama simu yako ni feki ama la. Hatukuweza kuthibisha moja kwa moja kwamba kweli simu zitazimwa mwezi Juni lakini tumejiridhisha kuwa kutakuwa na hatua dhidi ya wanaomiliki simu feki pindi itakapofika tarehe hiyo. Zifuatazo ni hatua unazoweza kuzitumia kuangalia kama simu yako ni fake, hakuna mahitaji makubwa kufanya hili ila tu unahitaji simu yako unayoitumia na unayotaka kuiangalia. Jinsi  ya angalia IMEI namba Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba ambapo kama simu yako au kifaa chako kina laini mbili basi kutakuwa na IMEI namba mbili Namba hii pia unaweza kuipata katika boksi la simu ama nyuma ya ya simu hiyo baada ya kutoa betri, utaijua kwa kuwa huwa ni tarakimu 15. Nakili namba hizo pembeni. Mfano wa IMEI namba iliyopatikana kwa kupiga *#06#

Pichaz za jaliyojiri kwenye usiku wa Birthday ya Linah,

Image
March 17 ni tarehe waliozaliwa watu wengi dunia lakini kutoka kiwanda cha   Bongoflevani mrembo anayemiliki hitsongs nyingi ikiwepo ‘ Malkia wa Nguvu’ ,   Linah   amesherekea siku yake ya kuzaliwa march 17 na kuudhuriwa na mastaa mbalimbali. Linah na Bilnass Neddy Music Queen Darleen na Kajala Queen Darleen, Kajala, Mwijako na Mwasiti Linah na Mdogo wake Linah na Bilnass Linah na Kajala Linah na Director Khalifani Linahna Recho Linah na Perfect Linah na Simple Linah, Mwijako na Mwasiti Linah na G Model Dj Tass, Linah na Bilnass Perfect, Bilnass na Kajala

BAADA YA WAFUASI 42 WA CUF KUKAMATWA ,MSHAURI WA MAALIM SEIF NAYE AKAMATWA NA POLISI ZANZIBAR

Image
Jeshi la Polisi linamshikilia mwanasiasa Mansoor Yussuf Himid kwa mahojiano kuhusiana na kulipuliwa kwa maskani ya CCM, Kisonge Michenzani mjini Unguja. Mansoor, ambaye ni mshauri wa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad alipigiwa simu jana jioni na polisi kwa ajili ya mahojiano katika kituo cha Madema. Kukamatwa kwa Mansoor kumekuja siku chache baada ya Jeshi hilo kuwakamata wafuasi wengine 42 akiwamo Kaimu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma, Hamad Masoud akituhumiwa kutoa taarifa kwamba kuna watu wamekimbilia porini na wengine wamekwenda Mombasa. Wafuasi hao 42 ambao bado wanashikiliwa ni kutokana na kuhusishwa na tukio la kulipuliwa nyumba ya Kamishina wa Polisi, Hamdan Omar Makame. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam jana alithibitisha kukamatwa kwa Mansoor na kwamba ni kutokana na hali ya matukio ya milipuko na mambo mengine, hivyo wanahitaji kupata maelezo ya kina kabla ya kumwachia. Alis

WAZIRI NAPE NNAUYE KUZINDUA MSIMU MPYA WA MASHINDANO YA UREMBO YA MISS TANZANIA 2016 JIJINI DAR

Image
Pichani kulia ni Mkurugenzi wa Lino International Agency LTD,Hashim Lundenga akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani),katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO),kuhusiana na msimu mpya wa mashindano ya Urembo ya Miss Tanzania kwa mwaka 2016.Lundenga amesema kuwa msimu huo mpya unatarajiwa kuzinduliwa rasmi siku ya jumamosi Machi 19,2016 katika hotel ya Ramada Resort iliyopo eneo la Kunduchi jijini Dar.Katika uzinduzi huo utakaokuwa wa aina yake Mgeni rasmi amepangwa kuwa ni Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo Mh.Nape Moses Nnauye.Kati ni Mshindi wa Miss Tanzania 2014-2015 Liliani Kamazima pamoja na Mkuu wa Itifaki wa kamati ya Miss Tanzania Albert Makoye. Lundega akifafanua jambo kwa umakini mbele ya Wanahabari (hawapo pichani). Lundenga amesema kuwa katika uzinduzi wa msimu huo mpya,utawakutanisha wadau mbalimbali wa tasnia ya Urembo wakiwemo Wabunifu wa Mavazi,Mawakala wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa

ZIARA YAWAZIRI MKUU, CHATO NA KATORO - GEITA.

Image
  Waizri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mtambo wa kukamu mafuta ya alizeti  wanaushirika wa Chato akiwa katika ziara ya mkoa wa Geita Machi 17, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa  Ushirika huo Elias Kaswahili.     Wasani wa Katoro Geita wakicheza ngoma ya Kisukuma mara baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo  Machi 17, 2016.   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa hadhara katika mji wa Katoro , Geita Machi 17, 2016.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)