Posts

Showing posts from May 8, 2017

Vilio vya Mastaa kwa Wanafunzi Waliokufa Arusha

Image
M AJONZI yamegubika nchi nzima kufuatia tukio la kihistoria la ajali ya basi lililosababisha vifo vya wanafunzi 33, walimu wawili na dereva iliyotokea Karatu mkoani Arusha. Taarifa zinasema kuwa basi hilo aina Toyota Coaster lililokuwa limebeba wanafunzi, walimu na dereva ambalo ni mali ya Shule ya Lucky Vincent liliacha njia na kutumbukia katika Mto Marera uliyopo kilometa 25 kutoka kwenye geti la Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro. Mbali na ajali hiyo kuwagusa wengi ndani na nje ya nchi, mastaa kutoka kwenye tasnia mbalimbali nchini wameibuka na kuzungumza na Wikenda, wakiweka wazi hisia zao za namna walivyoguswa na ajali hiyo. Wasikie; PROFESA JAY: Mungu azilaze roho za marehemu pema peponi. Kiukweli hili ni pigo kubwa sana kwa taifa letu, natoa pole sana kwa ndugu, jamaa wa marehemu na viongozi wote wa Mkoa wa Arusha kwa msiba huu mkubwa. Kwa mara nyingine tena kama taifa tunapoteza watoto wetu kwa idadi kubwa sana ambao wangeweza kuja kuwa hazina kubwa kwa

LIVE: Yanayojiri Arusha Kuaga Miili ya Wanafunzi Waliofariki kwa Ajali

Image
Makamu wa Rais wa Tanzania,  Samia Suluhu Hassan (kushoto) ,  akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha (kulia), Mrisho Gambo,   baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)  atakapoongoza  wananchi wa Mkoa wa Arusha na Watanzania  kuaga miili ya wanafunzi, na waalimu waliofariki kwenye ajali ya gari juzi Karatu.  Tukio  hilo linafanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha. Jeshi la Wananchi na polisi wakiwa uwanjani katika taratibu za  kupokea miili ya wanafunzi waliofariki. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitoa salam za rambirambi kwa wafiwa na Watanzania wote. Viongozi wa dini,  watakaoendesha ibada  wamewasili mahali pa tukio ikiwa ni pamoja na viongozi wa serikali mkoani, akiwemo Waziri wa Fedha na Mipano Philip Mpango. Pia kuna walimu 30 kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Vikosi vya usalama vikiwa eneo litakalofanyika hafla ya kuwaaga marehemu. Uwanja wa Sheikh Amri Abaid umejaa watu  ambapo viko

Picha za wanafunzi 32 waliofafiki katikia ajali Arusha

Image
Juzi wanafunzi 32 wa darasa la saba, walimu 2 na dereva wa gari la shule ya msingi iitwayo Lucky Vicent ya Arusha walifariki dunia majira ya saa 3 asubuhi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupata ajali katika eneo Rhotia Marera, Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha.