Posts

Showing posts from December 18, 2014

MAMBO KUMI (10)YA KUZINGATIA WAKATI WA UJAUZITO KWA AJILI YA AFYA YA MAMA NA MTOTO.

Image
1.Punguza matumizi ya vyakula vyenye “caffeine” Kama vile chai, kahawa na soda za cola huweza kusababisha mimba kuharibika au kutoka. 2. Kula vizuri chakula chenye mlo kamili na aina mbalimbali za matunda ili kujenga afya yako na ya mtoto. 3. Pata muda wa kutosha wa kupumzika ili kutuliza mwili na akili kwa afya yako na ya mtoto. 4. Fanya mazoezi madogo madogo ya viungo kama kutembea, kuogelea na yoga mara kwa mara 5. Kunywa dawa za kuongeza vitamini mwilini “Pregnancy vitamin” endapo huna uwezo wa kula chakula chenye mlo kamili lakini isiwe mbadala wa chakula 6. Acha kuvuta sigara kama ni mtumiaji kwani husababisha madhara kwako na pia mimba kutoka, kuzaa mtoto kabla ya siku kutimia na mtoto kufariki akiwa tumboni. 7. Acha kunywa pombe kwani humfikia mtoto kupitia mirija ya damu na “placenta” kama ukishindwa kabisa punguza kwa kiasi kikubwa. 8. Baada ya kugundua tu una mimba muone mkunga kwaajili ya maelekezo na ratiba ya jinsi ya kuhudhuria kliniki. 9

WANAJESHI 54 WA NIGERIA WAHUKUMIWA VIFO KWA KUSHINDWA KUPAMBANA NA BOKO HARAM

Image
Wanajeshi hao wakiwa mbele ya Mahakama ya Kijeshi jijini Abuja nchini Nigeria.Mahakama ya Kijeshi nchini Nigeria imewahukumu adhabu ya vifo wanajeshi wake 54 waliokataa kupambana na wapiganaji wa Kundi la Boko Haram. Wanajeshi hao walikutwa na hatia ya uasi, kushambulia na uoga. Wanajeshi hao wanashutumiwa kukataa kupigana kurudisha miji mitatu iliyokuwa ikishikiliwa na Boko Haram mwezi Agosti. Mwanasheria wa wanajeshi hao amesema wamehukumiwa vifo kwa kupigwa risasi na kikosi maalum huku wanajeshi wengine watano wakiachia. Vikosi vya Kijeshi vya Nigeria vimedai kuzidiwa silaha na Boko Haram, kwa kuwa hawapatiwi silaha za kutosha kupambana na wanamgambo hao. Boko Haram wanapambana kuunda himaya ya kiislamu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. CHANZO: BBC

JK:AKATISHA ZIARA YA MIZENGO PINDA

Image
Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu. Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow. Waziri mkuu Mizengo Pinda. Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa. Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2

NGUMI ZAPIGWA BUNGENI NCHINI KENYA

Image
Seneta Johnston Muthama aliyejeruhiwa mguuni na kuchaniwa suruali yake wakati wa vurugu bungeni leo. WABUNGE nchini Kenya leo wametofautiana bungeni na kuamua kutupiana makonde huku wengine wakichaniana nguo kufuatia mjadala kuhusu muswada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa Wakenya. Bunge nchini Kenya. Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 kufuatia mtafaruku huo. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha muswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais Kenyatta kuwa sheria. Wabunge wa upinzani waliupinga muswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama wa Bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kutaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa muswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa muswada huo wakisema 'bado mapambano.' Spika wa Bunge hilo, Justin Muturi kuna kipindi alimuru wali

TANZANIAN MIHAYO CHARLES WILL SERVE A MINIMUM OF 31 YEARS IN PRISON FOR MURDERING.

Image
 Photo: Mihayo will serve a minimum of 31 years in prison for murdering his daughters. (AAP: Julian Smith) Photo: Indianna, 3, (left) and Savannah, 4,  A Melbourne man who murdered his two young daughters by smothering them with a pillow has been sentenced to life in jail. Charles Mihayo, 36, smothered his daughters Savannah, 4, and Indianna, 3, at his unit at Watsonia in April. He pleaded guilty to the killings in August and was today sentenced in the Supreme Court to a minimum of 31 years in jail. Prosecutors said Mihayo was locked in a bitter custodial dispute with the girls' mother, his former wife, at the time and had acted out of revenge. The court heard Mihayo sent a text message to his former wife shortly before he killed them suggesting she had "won", and he was giving up his rights to see the girls. He told her he wanted to see them "one last time" and when she took them to see him, he dressed the girls up in new dresses h

ANGALIA DIAMOND NA ZARI WAKILA CHAKULA CHA USIKU

Image
Diamond amefika Uganda na kupokelewa na timu ya Zari kwaajili ya party yake ya#ZariAllWhiteCirocParty inayofanyika @guvnoruganda tarehe 18 December 2014. Hizi picha za chakula cha usiku wakiwa na mwenyeji wao Zari.  

PROF. TIBAIJUKA AKATAA KUJIUZULU

Image
  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka, akiongea na wanahabari hivi punde ndani ya Hyatt Regency Hotel Dar es Salaam amesema haoni sababu ya kujiuzulu kutokana na sakata la akaunti ya Escrow. Aongeza kuwa watu wanaona suala la kujiuzulu kama fasheni ila yeye hayupo katika fasheni hiyo.