Posts

Showing posts from May 22, 2016

Madhara Ya Kula Mayai Yasipoiva Vizuri Kwa Afya

Image
Mayai ni moja ya vyakula vyenye viini lishe muhimu kwa ajili ya afya ya mwili wa binadamu. Kwa kawaida mayai kabla ya kuliwa, huandaliwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchemshwa, kukaangwa au kuchanganywa na vyakula vingine kama vipande vya viazi mviringo ambavyo ni maarufu kwa jina la chips. Pia, kuna baadhi ya watu wanaopendelea kula mayai mabichi kama dawa ya tiba mbadala, kwa ajili ya kulainisha sauti na wengine hupendelea kula mayai ya kukaanga ambayo hayakukaushwa vizuri. Ukitembelea migahawa mingi utabaini kuwa watu wanakuwa na mitazamo tofauti na wanavyopenda kula mayai. Mfano kuna wanaoagiza watengenezewe mayai kwa mtindo unaojulikana kama ‘macho ya ng’ombe.’ Ukiagiza namna hiyo, mpishi atataka kuuliza kama ni ‘macho ya ng’ombe’ ya kugeuza. Ina maana kuwa ‘macho ya ngombe’ ya kugeuzwa ni yale yanayoivishwa pande zote lakini yale ambayo siyo ya kugeuza, huwa linaifa nusu. Upande mmoja unabaki ukiwa mbichi, na ndiyo raha ya baadhi ya watu. Hata u

Kauli ya Louis van Gaal baada ya Ubingwa wa Kombe la FA kwa Man United

Image
Baada ya kufanikiwa kutwaa Kombe la FA akiwa na Man United, Louis van Gaal amezungumza kauli ya kujivunia, licha ya kuwa kibarua chake kipo mashakani kuchukuliwa na Jose Mourinho kwa siku za usoni, licha ya kuwa mchana wa May 21 2016 ulianza kwa headlines zisizo njema kwake. Van Gaal ameripotiwa na Metro na AS kuwa atafukuzwa na Man United nafasi yake kuchukuliwa na Jose Mourinho, hiyo ilikuwa ni saa kadhaa kabla ya BBC na Sky Sports kuziongezea nguvu taarifa hizo, kwa kuripoti habari kama hizo katika tovuti zao. Louis van Gaal amekuwa akiandamwa na tetesi zinazohusu hatma ya kibarua chake, aliongea kauli zya kujivunia kama hana hofu na habari zinazoendelea.‘Hii ni furaha kubwa kwa klabu na mashabiki na kwangu pia ambaye nimefanikiwa kushinda taji hili nikiwa katika nchi nne tofauti ni makocha wachache wanaoweza kujivunia hilo, hivyo nina furaha sana na jambo hili”

Kiba, Diamond Kimenuka Hatari!

Image
    Kimenuka! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mafahari wawili wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kudaiwa kutupiana vijembe vya kufa mtu baada ya kuwepo kwa madai ya Kiba kuhujumiwa.       Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. Kwa mujibu wa chanzo makini, ili kuweka hujuma ya kibiashara, hivi karibuni, pamoja na kukanusha mara kadhaa kutokuwa na tatizo na Kiba, Diamond alidaiwa ‘kutengeneza’ kwa makusudi penzi la mwigizaji Jacqueline Wolper Massawe na msanii wa Wasafi Classic Baby (WCB), Rajabu Abdulhan ‘Harmonize’ kisha kuvujisha video ya uhusiano huo mpya siku ambayo Kiba alikuwa akiuachia wimbo wake mpya wa Aje (Jumamosi iliyopita), lengo likiwa kuhamisha upepo mashabiki kutoka kwenye wimbo mpya na kujali mapenzi ya wawili hao. “Ni hujuma ya kibiashara, Diamond na uongozi wake wameamua kumfanyia Kiba ili wimbo wake ukose kiki kwa watu,” kilidai chanzo chetu. Harmonize VIJEMBE VYATAWALA Hata hivyo, kwa muji

TAARIFA KUTOKA KWA FAMILIA YA MAREHEMU WILSON KABWE KUFUATIA UPOTOSHWAJI WA BAADHI YA VYOMBO VYA HABARI

Image
Familia ya Marehemu Wilson Kabwe  imesikitishwa sana na taarifa zilizosambazwa kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuhusu kauli na msimamo wa familia katika shughuli za maazishi ya mpendwa wao Wilson Kabwe. Familia inapenda kuchukua nafasi hii kutamka bayana kwamba, Dk. Zawadi Machuve si msemaji wa familia. Kauli yake iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba:- " Sisi hapa hatukaribishi viongozi, huu ni msimamo wa familia kama wao watafanya utaratibu wao sawa, lakini hatuko kwa ajili ya viongozi" Kauli hiyo ambayo ililenga kutoishirikisha Serikali katika msiba wa mtumishi wake tunaomba ipuuzwe na siyo kauli ya familia. Familia inatambua na inathamini sana mchango mkubwa wa Serikali katika kugharamia matibabu na  huduma  zote za mazishi. Familia inachukua fursa hii kuwakaribisha viongozi wote wa Serikali, ndugu, jamaa na marafiki wanaopenda kushiriki katika shughuli za mazishi ya mpendwa wetu. Imetolewa na: PHILIP MKENGA KABW

JEMBE FESTIVAL YAWAKUNA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA

Image
Msanii kutoka nchini Marekani Neyo akishambulia jukwaa na kuwapagawisha wakazi wa jiji la Mwanza . Neyo akiwa pamoja na Diamond Platnumz jukwaani wakiambulisha wimbo wao mpya mbele ya mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya. Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Ruby akiimba kwenye tamasha la Jembe Festival kwenye uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. Rapa Stamina akiupagawisha umma na mistari iliyo simama kwenye tamasha la Jembe mjini Mwanza. Mr. Blu akirap nyimbo zake zilizompa umaarufu kwenye tamasha la Jembe lililofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Diamond Platnumz na vijana wake wakishambulia jukwaa kwenye tamasha la Jembe lililofanyika kwenye viwanja vya CCM Kirumba mjini Mwanza. Mgeni rasmi wa tamasha la muziki la Jembe , Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM Dk. Sebastian Ndege kwenye chumba maalum nyuma ya jukwaa ,CCM Kirumba . BOFYA HAPA KWA PI