Posts

Showing posts from January 25, 2015

Mwanafunzi Ajifungua Ndani ya Daladala

Image
Mwanafunzi mmoja wa Shule ya Sekondari ya Keko amejifungua mtoto akiwa ndani ya daladala maeneo ya Mtoni Kwa Azizi Ally, jijini Dar es Salaam juzi  tarehe 23.   Mwanafunzi huyo ambaye hakuweza kupatikana jina lake mara moja, anasemekana alijifungua mtoto huyo bila ridhaa yake wakati akiwa katika harakati za kuitoa mimba hiyo.   Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, msichana huyo anasemekana alikuwa amekunywa madawa makali kwa lengo la kuitoa mimba hiyo ambayo anadaiwa kuificha  hadi pale alipoumbuka mchana wa siku hiyo.   Haikuweza kufahamika mara moja alikopelekwa mtoto huyo baada ya tukio hilo wala hatua alizochukuliwa binti huyo.

HUYU NDIO MTU ASIYE NA USO, ANAHOFU MTOTO WAKE MTARAJIWA ATAFANANA NA YEYE

Image
Baba mtarajiwa amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya kuishi bila kuwa na uso na kwa namna gani anahofia juu ya hali atakayozaliwa mtoto wake mtarajiwa.Anaitwa Mohammad Latif Khatana, 32, kutoka Kashmir, India, hawezi kuona wala kufanya kazi kutokana na ngozi zilizofunika uso wake. Watu humkimbia barabarani kutokana na hali yake huku wakionekana kuogopeshwa nayo.    Kwa sasa ni mwenye faraja kutokana na ukweli kwamba mke wake ni mjamzito wa miezi saba, ila ana hofu labda huenda mtoto wake anaweza kuzailiwa akiwa anfanana naye. Alisema: “Naingoja kwa hamu hii hali ya kuwa baba na kupata furaha ya maisha. Ila nahofu kila siku na kusali ili mwanangu asije kuzaliwa kama mimi.”   Latif, ambaye anaishi milimani na mke wake mwenye miaka 25 aitwaye Salima, eneo la Tuli Bana, ndani ya Jammu and Kashmir, huwa anatembea mpaka Srinagar mara nne kwa mwaka kwa ajili ya kuomba misaada na ili kupata hela.   Alizaliwa na kinundu kidogo kwenye uso wake ili kimeendelea kuk

DIAMOND THE PLATNUMZ AWARUSHIA BURUNGUTU LA MAMILION MASHABIKI WAKE KWENYE TAMASHA LA TIGO KIBOKO YAO LEADERSCLUB

Image
  Kwa roho nzuri alokuwa nayo Diamond na kwa kutambua mchango wa mashabiki wake aliamua kurudisha fadhila japo kidogo kwa kuwarushia maburungutu ya pesa wakati akiimba kama ahsante kwa mashabiki .. pengine kuna walokuwa hawana nauli za kuwarejesha makwao..wamepata pesa..kuna walokuwa hawajui.maskin ya Mungu kesho wataamkaje..but wamepata kianzio kuna walopata pesa ya kula bata ..etc... side B sasa . kwanza badala ya kupitia mlango husika karuka ukuta(cjaelewa bdo alikua na maana gani)..mashabiki wenu mloweka kuzomea/kurusha chupa baada ya kuona pesa wakasariti badala ya kuzomea wakaishia kuokota na kudaka pesa na mwisho kupiga shangwe tuu.