Posts

Showing posts from February 8, 2018

Diamond, Mobeto wamaliza fofauti zoa

Image
Msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond amesema mazungumzo katika kesi yake Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa watoto kati yake na mwanamitindo Hamisa Mobeto,  imekwenda vizuri. “Niseme tu mambo yameenda vizuri na kama mnavyojua mambo ya mahakamani ikitokea ninahitajika nitakuja,” amesema. Diamond alifika mahakamani hapo leo Februari 8, 2018  kusikiliza kesi inayomkabili ya matunzo ya mtoto Prince Abdul iliyofunguliwa na Mobeto. Amesema yeye na Mobeto hawana shida yoyote, ila kuna watu waliokuwa wakizungumza maneno na kumchochea Mobeto. "Tunahitaji kuweka mambo sawa. Tunahitaji kuwa katika mstari kwa sababu vitu vidogo vinaharibu upande wa mama na upande wa baba kwa hiyo tulikuwa tunaweka mambo sawa ili kesho na keshokutwa yasilete sintofahamu baina yetu,” amesema na Diamonda na kuongeza: “Ikitokea kuna mtafaruku baina ya mtoto, kila mtu anakuwa na mawazo yake, kwa hiyo ni lazima kumjenga mtoto na kuhakikisha kuwa mtoto anajengwa na k

ANGALIA WEMA SEPETU ALIVYOFIKA MAHAKAMANI NA WAKILI WAKE,KESI YAKE MAPYA YAIBUKA

Image
Kesi ya mrembo Wema Sepetu ya kukutwa na msokoto wa bangi imesikilizwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Inspekta wa Polisi, Wille ameieleza mahakama kuwa hakuwepo wakati Wema akichukiliwa sampuli ya mkojo kwa Mkemia Mkuu wa serikali. Shahidi huyo aliyaeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati alipoulizwa maswali na Wakili wa Wema, Alberto Msando. Katika ushahidi wake, Inspekta Wille, alidai hakuwahi kupeleka sampuli za mkojo za washtakiwa wenzake Wema ambao ni Angelina Msigwa na Matrida Abbas kwenda kuchunguzwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali. Inspekta Wille alidai kuwa February 8, 2017 alifika katika ofisi za Mkemia Mkuu wa Serikali saa 5 asubuhi na kumkabidhi Mchunguzi Elia Mulima kichupa cha plastiki ambacho ndani kilikuwa na mkojo wa Wema. Wakili Msando alimuuliza Inspekta Wille kama alikuwepo wakati sampuli ya mkojo uliokuwamo ndani ya kichupa cha plastiki unachukuliwa ambapo I alijibu kuwa hakuwapo. Msando alimuhoji

ANGALIA AJIFUNGUA MTOTO KWENYE KORIDO HOSPITALINI

Image
JESICA HOGAN, mama wa watoto sita mkazi wa Riley, Kansas, Marekani, amejifungua mtoto pekee wa kiume katika korido ya hospitali ambayo alikuwa anawahishwa kwenda kujifungua. Mtoto huyo aliyeleta furaha katika familia hiyo ambayo ilikuwa na mabinti mtupu, anaitwa Max, ambaye alizaliwa akiwa salama na mwenye afya njema. Mwanamke huyo aliyejifungulia katika Hospitali ya Via Christi, ya Manhattan, Kansas, alisema alikuwa hana uhakika wa tarehe ya kujifungua, hivyo hakujua ni lini uchungu ungelianza. Alikuwa nyumbani wakati chupa ilipovunjika kunako saa tisa usiku ambapo mumewe, Travis, alimkimbiza hospitali. Mara tu baada ya kuingia katika korido ya hospitali hiyo, Jesica alihisi mtoto alikuwa ameanza kutoka, hivyo akaanza kuvua suruali yake wakati kichwa cha mtoto kilianza kujitokeza. Walianza kusaidia na mumewe hapohapo kwenye korido ambapo alilala chini kabla ya manesi kuja na kumsaidia. “Nilikuwa sifahamu hasa siku halisi ya kujifungua, lakini siku hiyo nilijua im

ANGALIA FARASI AFANYWA MSIMAMIZI HARUSINI,NI VITUKO VYA AJABU

Image
Maharusi wapya walikuwa washitakiwe kufuatia makosa ya kumtembeza farasi bila ruhusa maalum, baada ya Bibi harusi kuamua kumuweka farasi huyo kama mmoja wa wasimamizi wake. Mwanadada Alex Wells, mwenye umri wa miaka 28, alifanya uamizi huo alipokuw akifanya mipango ya harusi yake huko Nottinghamshire, Uingereza ambapo hata mume wake aliafikiana naye. Farasi huyu aliyejulikana kwa jina la Toffee, mwenye umri wa miaka 17 inasemekana pia kwa namna moja au nyingine ndiye aliyeruhusu harusi hiyo kufanyika kwani ni rafiki wa karibu sana wa Bi Harusi. Mume wa Alex, Graham Sales alikiri kukubaliana na hali hiyo kwani hata kwenye maisha ya kawaida ni kama anashindana na farasi huyo ili kupata muda na mkewe. Farsi huyu alikuwa na wakati mzuri wakati wa harusi hiyo kwani aliweza kushiriki katika kupiga picha za pamoja na mambo mengine.    

Breaking News: Tambwe Hizza wa Chadema Afariki Dunia

Image
Kada wa Chadema,  Tambwe Hizza, enzi za uhai wake. KADA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  Tambwe Hizza, amefariki dunia leo asubuhi nyumbani kwake akiwa amelala, msemaji wa chama hicho, Tumaini Makene,  amethibitisha  na kuongeza kwamba mwili wake umepelekwa Hospitali ya Temeke Dar es Salaam asubuhi hii. Kwa mujibu wa Chadema, marehemu Hiza alikuwa kwenye moja ya vikao vya chama hicho hadi jana saa tano usiku wa kuamkia leo. …Akiwa katika moja ya mikutano ya Chadema. Marehemu Tambwe Hizza amefariki akiwa anasumbuliwa na ugonjwa wa pumu na  alikuwa pia mmoja wa waratibu wa kampeni za chama  hicho katika jimbo la Kinindoni Hizza anafahamika sana kwa siasa zake akiwa CUF, baadae alihamia CCM na kuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Propaganda wa CCM na 2015 aliamua kuondoka CCM na kuhamia CHADEMA.

Uwoya, Aunt Ezekiel Wamchokonoa Shonza

Image
Wolper. DAR ES SALAAM: KITENDO cha wasanii wa filamu, Aunt Ezekiel Grayson Gwantwa ‘mama Cookie’ na Irene Pancras Uwoya kutupia picha mtandaoni zikionesha wakiwa wanaogelea huku maeneo nyeti ya miili yao yakiwa wazi, kimetafsiriwa na wadau mbalimbali ni kama ‘kuishika sharubu’ serikali. Mwanzoni mwa wiki hii, picha za wasanii hao wakiwa ndani ya majakuzi sehemu tofauti na kwa nyakati tofauti zimeleta hisia tofauti kwa jamii huku wengine wakienda mbele kwa kusema kitendo hicho ni kukaidi agizo la Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kupitia naibu waziri wake, Juliana Daniel Shonza aliyepiga marufuku picha za utupu mitandaoni. Aunt Ezekiel. Baada ya kuvuja kwa picha hizo, waandishi wetu waliwatafuta wasanii hao kupitia simu zao za mkononi ili kusikia utetezi wao juu ya jambo hilo. “Picha hiyo niko lokesheni (eneo la kuigizia), sasa sioni kama kuna tatizo kuonesha mtandaoni picha ya namna hiyo,” alisema Irene Uwoya. Kwa upande wa Aunt Ezekiel

EWURA Watangaza Bei Mpya Ya Mafuta Kutumika Februari 7, 2018

Image
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei mpya za mafuta zinazoanza kutumika leo Februari 7, 2018 huku bei za petroli, dizeli na mafuta ya taa zikipanda. Taarifa kwa umma iliyotolewa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Nzinyangwa Mchany imesema bei za rejareja zimeongezeka kwa petroli ikiwa ni Sh59 sawa na asilimia 2.70, dizeli Sh46 (sawa na asilimia 2.30), na mafuta ya taa kwa Sh24 (sawa na asilimia 1.17). Amesema bei za jumla nazo zimeongezeka ambazo kwa petroli ni Sh58.57 sawa na asilimia 2.85, dizeli kwa Sh46.48 (sawa na asilimia 2.44) na mafuta ya taa kwa Sh23.75 (sawa na asilimia 1.24). Mchany amesema ongezeko hilo linatokana na bei kuongezeka katika soko la dunia. “Bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli na dizeli yaliyoingizwa nchini kupitia Bandari ya Tanga nazo zimeongezeka ikilinganishwa na toleo lililopita la Januari 3. Bei za mafuta ya taa hazijabadilika kwa sababu hakuna yaliyoingizwa nchini kupitia ba

Mwigulu Avamia Shamba la Bangi, Alichokifanya

Image
WAZIRI wa mambo ya ndani nchini,Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari  sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha. Mwigulu akishirikiana na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Arusha, (RPC)Charles Mkumbo pamoja na vikosi vya askari wa jeshi la polisi mkoani hapo walilazimika kuacha magari yao njiani na kutembea umbali wa kilomita 5 milimani kufika katikati ya msitu huo ambapo wamiliki wa mashamba hayo walitokomea kusikojulikana. Akizungumza na waandishi wa habari  wakati wa zoezi hilo Mwigulu amesema kwamba serikali itaendelea na oparesheni pande zote za nchi na haitasita kuwakamata wahusika wote na kutaifisha magari yatakayotumika kusafirisha bangi. Aidha Waziri Mwigulu amewaambia askari waliokuwa wakishiriki katika zoezi hilo, Mwigulu mbali na kuwapongeza kwa kazi wanayofanya lakini amewaambia kwamba pamoja na kufanikiwa kuteketeza madawa ya kulevya yanayo

Kopa, Msagasumu Kupamba Shindano la Nyonga

Image
WAMAMA wa uswazi na ushuwani leo Alhamisi wanata-rajiwa kuon-eshana matu-mizi ya nyonga kwenye shindano litakalo-fanyika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Akizungumza na gazeti hili, mratibu wa tamasha hilo, Maimartha Jesse alisema shindano hilo litasind-ikizwa na burudani kutoka kwa Mfalme wa Uswazi (Msaga-sumu), Malkia wa Mipasho (Khadija Kopa), Jack Simela na wengineo. Sambamba na wasanii hao Maimartha alisema pia kutakuwa na burudani ya ngoma za Kibao Kata na Baikoko kutoka Tanga. Maimartha alisema upande wa ushereheshaji atakuwa yeye mwenyewe akisaidiana na Sakina Liyoka ambao kama kawaida yao watamwaga ubuyu mwanzo mwisho. Katika burudani zote hizo kiingilio kitakuwa shilingi 5000 tu. RICHARD BUKOS