Posts

Showing posts from November 9, 2017

Mchakato Katiba Mpya, Watolewa Majibu na Waziri Mkuu

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amesema kuwa Changamoto za jamii ni nyingi kuliko mahitaji ya Katiba hivyo suala la katiba sio kipaumbele cha serikali kwa sasa. Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo Bungeni wakati wa kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu, ambapo alijibu swali la Mbunge wa Temeke Abdallah Mtolea lililohoji kuwa ‘Serikali ya awamu ya tano imetimiza miaka miwili lakini hakuna jitihada zozote zilizofanywa katika kuendeleza mchakato wa katiba ulioachwa na Serikali ya awamu ya nne. Akijibu swali hilo Waziri Mkuu amefafanua, “Katiba mpya inahitaji gharama kubwa na sisi tumeanza na kutatua changamoto za jamii kwanza, ikiwemo mahitaji ya maji, changamoto za elimu, na sekta ya Afya”. Amesema Waziri Mkuu Waziri Majaliwa ameongeza kuwa Katiba ni muongozo tu na wakati ukifika serikali yake imemaliza changamoto basi wataanza mchakato huo. “Kila bajeti ina vipaumb

Breaking News: Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi mwingine Tunduru

Image
 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 November 2017 ametengua uteuzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Bwa. Abdallah Hussein Mussa kwa kushindwa kumudu majukumu yake.