Posts

Showing posts from August 6, 2013

PICHA ZA NUSU UCHI ZA RIHANNA KATIKA TAMASHA LA CROP OVER 2013

Image
  Taswira juu na chini zinamuonesha Mwanamuziki Robyn Rihanna Fenty 'Rihanna' akijiachia na ndugu, jamaa na marafiki katika tamasha la kila mwaka la 'Crop Over Carnival' lililofanyika nyumbani kwao Barbados.

CCM BADO INA IMANI KUBWA NA TUME YA KATIBA

Image
Nape Nnauye NA MWANDISHI WETU CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) kimesema bado kina imani na Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini, katika mchakato unaoendelea wa kupata katiba mpya. Imesema licha ya CCM kutofautiana kimawazo katika baadhi ya maeneo katika rasimu ya kwanza ya  katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, lakini haina ugomvi na tume hiyo. Hayo yamesemwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.  "Tunawaheshimu sana wajumbe wa tume hii, na kwa kweli tunamatumaini nao sana kuwa watatimiza wajibu wao kwa weledi mkubwa", alisema Nape. Nape alibainisha kwamba  pamoja na maeneo mengine ya rasimu ya kwanza ya katiba ,  CCM ina mawazo tofauti kwenye suala la Muundo wa Muungano ambapo wakati rasimu inapendekeza muundo wa serikali tatu, CCM yenyewe inapende

MTOTO WA USHER RAYMOND ALAZWA ICU MAUTUTI KWA AJALI

Image
Usher 's son  Usher Raymond V  is in the ICU at an Atlanta hospital after a serious accident in the singer's pool Monday, source has learned. Sources tell source, the accident occurred around 6 PM yesterday. Usher was not home at the time. Here's what we know.   The child was playing in the pool with his aunt and saw a toy in the drain.  He dove down to get the toy and his arm got stuck in the drain.  The aunt immediately dove in to rescue him but couldn't get his hand out.  The maid then dove in and tried but was also unsuccessful. The maid screamed for help.  Two men working in the house came out, dove in and freed the boy.  He was given CPR immediately and rushed to the hospital.  Usher arrived and drove in the ambulance with his son. 5-year-old Usher Raymond V is the oldest of Usher's two sons with ex-wife Tameka Raymond. We're told Usher and Tameka are cu

BILIONEA AMTWANGA RISASI MFANYABIASHARA WA MADINI ARUSHA

Image
JIJI la Arusha na Mkoa wa Manyara, hali ya hewa ilishachafuka, wingu zito limefunika kufuatia kuuawa kwa kupigwa risasi, mfanyakazi wa Kampuni ya Tanzanite One, Onesmo William Mushi (pichani). Mtuhumiwa wa mauaji hayo ni bilionea wa madini, mkazi wa Arusha, Joseph Mwakipesile ‘Chusa’ ambaye ni mfanyabiashara anayemiliki migodi, Mererani wilayani Simanjiro, Manyara.NA GLOBAL PUBLISHER ONESMO ALIVYOUAWA Habari zimedai kwamba Onesmo akiwa eneo lake la kazi, mgodini chini, alipigwa risasi mbili kifuani ambazo ziliondoa uhai wake. Tukio hilo lilitokea saa 8 usiku, Julai 20, mwaka huu, chanzo kikitajwa kwamba ni mgogoro wa kugombea madini. Imedaiwa kuwa Onesmo, akiwa na wafanyakazi wenzake wa Tanzanite One ambao wamefahamika kwa jina mojamoja, Kennedy na Leonard, walikutana na wachimbaji wadogowadogo hivyo kutokea mvutano wa kimaslahi. Habari zimedai kwamba miongoni mwa wachimbaji hao wadogo, alikuwepo Chusa ambaye ndiye a

TEKNOLOJIA MPYA KUOKOA MAZAO YANAYOPOTEA

Image
  Na Mahmoud Ahmad,Arusha. Uhifadhi duni na mbovu wa mazao husababisha wakulima kupoteza aslimia 5%ya mazao yao  kuanzia shambani kabla ya kuvunwa na kusafirishwa hadi kwenye masoko Hayo yameelezwa na Msimamizi wa kituo cha kueneza teknolojia ya kilimo kanda ya kaskazini (ATTC)  Ernest Elias alipokuwa akizungumzia teknolojia mpya ya mavuno  ambayo wanayoonyesha katika maonyesho ya nane nane mwaka huu yanayofanyika katika viwanja vya Taso vilivyoko kata ya themi jijini hapa Ernest Elias amesema kuwa teknolojia hiyo mpya ambayo wameionyesha kwa mara ya kwanza katika maonyesho hayo itawasaidia wakulima kuvuna kwa urahisi na kufungasha wakiwa huko huko shambani kwa namna ambayo haitaruhusu upotevu wa mazao hata wakati wa usafirishaji na masokoni pia. Elias alisema kwa wastani  Mkulima akivuna gunia 10 anapoteza gunia 1 kutokana na  ubovu wa uhifadhi  wa mazao na mfumo mzima hadi kumfikia mhitaji sokoni.

KICHANGA CHAZALIWA NA JINSIA MBILI MKOANI RUVUMA

Image
  Mganga mfawidhi wa Hospitali ta Wilaya ya Tunduru Dkt. Joseph Ng'ombo akimuangalia mtoto huyo aliyezaliwa akiwa hana macho, pua na Shavu linalo shika mdomo wa juu, kushoto ni mkunga wa zamu katika Hospital hiyo Rukia Nguo akiwa akiwa amekishika kichanga  Huu ndiyo muunekano wa kichanga hiki usoni. Mkono wa mkunga huyo ukionyesha maungo ya kichanga hicho kilichozaliwa kikiwa na sehemu nyeti mbili ikiwepo ya kiume kwa juu na ya kike kwa chini. ------------------------------ ----------------  Na Steven Augustino, Tunduru MAJONZI na Simanzi zilitawala kwa wanafamilia na Wauguzi katika hosipitali ya Wilaya ya Tunduru baada ya ndugu yao mkazi wa Kijiji cha Kadewele Mjini hapa aliyetambuliwa kwa jina la Rehema Safi (42) kujifungua Mtoto wa ajabu mbaye pamoja miongoni mwa maajabu hayo nipamoja na kuzaliwa akiwa na Jinsia Mbili. Aidha Kichanga hicho ambacho kimezaliwa kikiwa na uzito wa kilo 1.8 pia kimezaliwa kikiwa hak

AJALI MBAYA YATOKEA MBEYA MMOJA AFARIKI PAPO HAPO

Image
GARI AINA YA TOYOTA COROLLA  ILIYOGONGANA NA BASI LA HOOD MENEO YA MSWISWI MBEYA DEREVA WA GARI NDOGO AMEFARIKI PAPO HAPO HATI YA KUSAFIRIA YA MAREHEMU DAVIS HANAMUNDE MZAMBIA MNAMO TAREHE 04.08.2013  MAJIRA YA SAA 06:45HRS HUKO MSWISWI WILAYA YA MBARALI BARABARA YA MBEYA/IRINGA, GARI NO T. 159 AXM AINA YA SCANIA BUS MALI YA KAMPUNI YA   HOOD LIKIENDESHWA NA DEREVA OMARY  SAID, MIAKA 50, MZIGUA, MKAZI WA MABIBO DSM LILIGONGANA NA GARI NO IT.3014 TOYOTA COROLLA LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA DEVIS  ANAMUNDE, MIAKA 28, MZAMBIA MKAZI WA MUNZE LUSAKA NA KUSABABISHA KIFO CHA DEREVA HUYO PAPO HAPO.  MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI WA MAGARI YOTE MAWILI NA DEREVA WA HOOD BUS AMEKAMATWA TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI.  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHANA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYO

"TUTAHAKIKISHA KAGAME HAPONI , NI LAZIMA TUMMALIZE KABLA HAJATOROKA"..... HII NI KAULI YA BAADHI YA ASKARI WETU

Image
Chokochoko  zinazoendelezwa na Rais wa Rwanda, Paul Kagame (pichani) dhidi ya Rais Jakaya Kikwete zimewakasirisha baadhi ya wananchi wakiwemo askari wa Tanzania na wakadai kuwa kiongozi huyo wa Rwanda atakiona cha moto akianza uchokozi. Wakizungumza na gazeti  la UWAZI  mwishoni mwa wiki iliyopita kwa sharti la kutoandikwa majina yao gazetini, baadhi ya askari walisema wanamshangaa Kagame kuitishia Tanzania wakati anajua kuwa hana ubavu wa kupigana nayo.   Askari wengi waliohojiwa, walisema Rwanda haina uzoefu wowote katika vita ya kimataifa ukilinganisha na Tanzania na Kagame akianzisha vita ni yeye atakayekufa kwa sababu vita haina macho.   “Kagame anajua kwamba Rais Kikwete si mgomvi na alimpa ushauri tu kwa kumwambia azungumze na waasi nchini mwake sasa kwa nini anaendelea kufanya chokochoko? Akianza vita itamuua. Kwa nini anamdhalilisha rais wetu?” alisema askari mmoja.     Akaongeza: “Kagame amezoea vita ya wao kwa wao lakini Tanzania tumeshakwenda