Posts

Showing posts from April 17, 2016

BREAKING NEWS : MSANII TUNDA MAN APATA AJALI MBAYA IRINGA

Image
  Taswira za ajali aliyoipata Tundaman leo. Kama ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii utakua umekutana na taarifa inayomhusisha Tunda Man kupata ajali  akiwa Mkoani iringa Asubuhi ya April 17   Tunda Man. Maelezo ya mwanzo ya   Tunda Man   amesema ‘ Tulikua tunatoka Njombe baada ya kumaliza show yetu na tukasema bora tusilale tuwahi kufika Dar,tumetoka Njombe saa 10 alfajiri mimi nikawa nasikia usingizi nikamwambia mwanangu hebu tuendeshe kidogo,kufika kijiji cha Idetelo kilomita kama 20 au 30 kabla ya kufika Mafinga tukiwa tumelala tukashtuka Gari inaingia porini tukasikia mshindo mkubwa gari imepiga puuuh Dereva hapo hapo akawa amefariki ‘ Tunda Man   anamalizia kwa kusema ‘ Tulikua watu watano kwenye gari aliyekaa mbele na Dereva amevunjika mkono na nyama zimechanika,kuna mtu aliyekua nyuma mapafu yamepasuka,Mimi nipo poa,kwa sasa hivi tuko Mafinga hapa Hospitali ya Wilaya tunaangalia taratibu za kuchukua mwili tuupeleke Kilosa kwa ndugu zake,marehemu

PAPA FRANCIS AWACHUKUA WAKIMBIZI 12 NA KUWAKARIBISHA KUISHI ROMA

Image
Papa Francis leo amewakaribisha wakimbizi 12 wa Syria wakati wakiwasili Jijini Roma baada ya kuwachukua kutoka kwenye kambi ya Lesbos kufuatia ziara yake katika kisiwa hicho cha Ugiriki. Familia tatu za wakimbizi wa Syria walipanda ndege ya Papa Francis punde tu baada ya ziara yake hiyo ya Lesbos kuangazia mgogoro wa kibinadamu unaotokana na wakimbizi.                  Papa Francis akiwakaribisha wakimbizi wa Syria aliowachukua Lesbos Msemaji wa Vatican amesema Papa Francis ameamua kuonyesha ishara ya kuwakaribisha wakimbizi hao kwa kuwachukua kukaa Roma ambao miongoni mwao wamo watoto sita.               Papa Francis akimbusu mtoto mkimbizi wakati wa ziara yake ya Lesbos                          Papa Francis akisalimiana na wakimbizi waliopo Lesbos Ugiriki

WANAUME HUPENDA KUOA MWANAMKE WA TABIA/AINA HII

Image
Habari za wiki hii mpenzi msomaji. Mimi namshukuru Mungu kwa kuweza kunikutanisha na nyinyi kupitia safu hii ambayo pamoja na mambo mengine nazungumzia juu ya mada mbalimbali ambazo zinagusa maisha yetu ya kila siku. Wiki hii nitazungumazia juu ya aina ya wanawake ambao wanaume wengi hupendelea kuoa. Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha. Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri. Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa. Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzur