Posts

Showing posts from January 2, 2018

Mbunge Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Aitwa Polisi

Image
MBUNGE wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’ na mratibu wa chama hicho Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wameitwa katika Kituo Kikuu cha Polisi mkoani humo huku wakisema hawajui sababu ya wito huo. Wawili hao wamesema wanahisi wito huo unatokana na mkutano wa hadhara alioitisha mbunge huyo katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya. Sugu amesema leo Jumanne kuwa, juzi jioni alipigiwa simu na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) kwamba yeye na Masonga wafike jana ofisini kwa ajili ya mazungumzo lakini alimueleza kuwa itakuwa ni siku ya sikukuu hivyo itakuwa vigumu ngumu kwenda, hivyo walikubaliana wafike leo. “Polisi walinipigia simu juzi jioni wakinitaka mimi na Masonga twende Makao Makuu ya Polisi jana, nikawaambia itakuwa ni sikukuu hivyo tukakubaliana leo asubuhi. Sasa hivi tupo njiani tunaelekea huko kuitika wito. Sijajua sababu, lakini nadhani ni uchochezi,” amesema Sugu. Masonga amesema anaamini sa

Ikulu yatoa neno kuhusu kutokuapishwa kwa Dk. Slaa

Image
Balozi, Dk. Willibrod Slaa. WAKATI zikiwa zimetimia siku 40 baada ya kuteuliwa kuwa balozi, Dk. Willibrod Slaa (pichani), hajaapishwa na kuzua minong’ono hatimaye Ikulu imefunguka na kuweka kila kitu wazi. Itakumbukwa kuwa Rais Dk. John Magufuli alitangaza uteuzi wa Dk. Slaa kushika nafasi ya ubalozi Novemba 23, mwaka jana, lakini tangu wakati huo hajaapishwa. Rais Magufuli amekuwa na utamaduni wa kuteua viongozi na baada ya siku chache wanaapishwa, lakini kwa Dk. Slaa imechukua muda mrefu na kuibua sintofahamu. “Hili ni jambo ambalo siyo la kawaida, tumezoea mtu akiteuliwa kushika wadhifa fulani na rais baada ya siku chache, tunaona au kusikia kuwa ameapishwa, lakini kwa Dk Slaa ni zaidi ya mwezi sasa, kuna sababu zimetolewa? Tujulisheni,” ni moja kati ya simu nyingi za wasomaji wetu waliopiga chumba cha habari kutaka ufafanuzi. Kutokana na hali hiyo, Uwazi liliwasiliana na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ili kujua kwa nini imechukua muda mrefu kumuapisha Dk

SIWEMA AFUNGUKIA KUMUONA MWANAYE KWA NAY

Image
Nay wa Mitego akiwa na watoto wake. MZAZI mweza wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ Siwema Edson amefungukia ishu ya kumuona mwanaye, Cartes kuwa, si kweli kwamba hajawahi kumuona tangu aondoke kwa jamaa huyo. Siwema mwenye maskani yake jijini Mwanza aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, si kweli kwamba hajawahi kuomuona mtoto wake kwani mara nyingi anapokwenda kumuona kwa mama wa mwanamuziki huyo, Nay anakuwa hajui. “Naongea naye kila mara, nimeshakwenda kumuona zaidi ya mara tatu, sema tu baba yake hajui hivyo angekuwa anamuuliza mama yake angempa jibu,”   alisema Siwema.

Uchangudoa wa Zari Waibua Kimbembe!

Image
MAMBO ni moto! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya mfanyabiashara maarufu Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kukiri kuwa yeye ni changudoa mzee, kauli yake imeibua kimbembe. KUPITIA SNAPCHAT Kupitia mtandao wake wa kijamii wa Snapchat, mwishoni mwa wiki iliyopita, Zari alitupia ujumbe akionesha kuwa yeye ni changudoa mzee, lakini mwenye mafanikio akimjibu hasimu wake, mwanamitindo Hamisa Mobeto bila kumtaja. “Bora mimi changudoa mzee niliye na mafanikio na bado ananipenda kuliko kijana wa miaka 20+, mama uliyeachwa mara mbili na tuzo juu,” alisema Zari kupitia Snapchat. Kwa muda mrefu, Zari amekuwa kwenye tifu la aina yake baada ya Mobeto kuzaa na bwana wake, msanii wa Bongo Fleva miezi michache iliyopita. KIBEMBE KILIVYOIBUKA Kitendo cha Zari kutoa kauli hiyo, kimbembe kiliibuka mtandaoni mara baada ya ukurasa wa Instagram wa Global Publisher, kutupia habari hiyo ambapo wafausi wa mtandao huo walianza kurushiana maneno makali huku kila m

WATU 120 WAMEKAMATWA WAKIWEMO MAPADRI NCHINI DRC CONGO

Image
Zaidi ya Makanisa 150 yaliandamana nchini DRC Congo December 31, 2017 wakimtaka Rais Joseph Kabila kuondoka madarakani katika maandamano hayo imetolewa taarifa na Msemaji wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Congo Florence Marchal Katika taarifa iliyotolewa imesema watu saba wameuawa mjini Kinshasa na mmoja katika mkoa wa Kananga, katikati mwa Congo na kuongeza kuwa watu 82 wamekamatwa wakiwemo mapadri, katika mji mkuu Kinshasa, na 41 katika maeneo mengine ya nchi hiyo. Katika hotuba yake ya kumaliza mwaka, Kabila amesisitiza kuwa kutangazwa  kwa ratiba ya uchaguzi wa December 2018, kumefungua njia ya maandalizi ya uchaguzi huo.

Masoud Kipanya awatoa hofu Watanzania

Image
 KUFUATI taarifa kusambaa mitandaoni jioni ya leo Januari 1,2018 kwamba, mchora katuni maarufu Tanzania, Masoud Kipanya amekamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za uchochezi, Kipanya kupitia akaunti yake ya Twitter ameibuka na kuwatoa hofu Watanznia kwa kuandika kauli hii. “Poleni kwa usumbufu na asanteni kwa kujali hali za wengine. Niko salama Alhamdulillah. Namshukuru pia aliyesambaza taarifa. ‘AMESAIDIA’.” Taarifa hizo zinadai kuwa, Masoud Kipanya ambaye pia ni mtangazaji wa Clouds FM, amekamatwa na Polisi baada ya kuchora katuni ambayo ina maudhi ya uchochezi kati ya wananchi na serikali. Aidha katika kauli yake Masoud hajaweka wazi iwapo amekamatwa na amepelekwa kituo kipi cha polisi na kama ameachiwa au bado.