Posts

Showing posts from August 28, 2017

BREAKING: Polisi watoa taarifa Kuhusu tukio la mlipuko ofisi za mawakili

Image
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 28/08/2017                TUKIO LA MLIPUKO KWENYE OFISI ZA MAWAKILI WA IMMA Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm mnamo tarehe 26/8/2017 lilitoa taarifa ya awali ya tukio la mlipuko uliotokea katika ofisi za mawakili wa IMMA zilizopo katika eneo la Upanga jijini Dar Es Salaam. Hivyo Jeshi la Polisi linapenda kuufahamisha umma kuwa  uchunguzi wa awali uliofanyika umebaini kwamba usiku wa kuamkia tarehe 26/8/2017 majira kati ya saa 7:00-8:00 watu wasiojulikana utambulisho wao na idadi kamili, walifika katika ofisi za mawakili wa kampuni ya IMMA (IMMA ADVOCATES) wakiwa na magari mawili wakijifanya ni askari na kuwarubuni kisha kuwachukua walinzi wa jengo hilo na kuondoka nao kwenye moja ya gari walilokwenda nalo,ambapo baadaye walinzi hao walikutwa maeneo ya Kawe wakiwa hawajitambui. Aidha, kundi lililobaki liliingia ndani ya Ofisi hizo na kuweka milipuko iliyotengenezwa kienyeji ambayo baada ya watu hao kuondoka ililipuka na kusaba

RAS-Dodoma- Wakumbukeni Idara za Elimu katika PlanRep Mpya.

Image
  Katibu Tawala wa Mkoa wa Dododma  Rehema Madenge akifungua mafunzo ya siku nane kwa wataalamu wa Afya, Mipango na Fedha kutoka Mikoa Mitano chini ya ufadhili wa mradi wa Uimarishaji Mifumo (PS3) Serikali mkoani hapa imesema ili mpango wa PlanRep uweze kufanikiwa kwa ufasaha hakuna budi kuzijumuisha idara za Elimu katika mafunzo yanayoendelea mkoani Dodoma yanayo wajumuisha wataalam wa mipango pamoja na afya kutoka mikoa mitano ya Tanga, Tabora, Manyara, Singida na wenyeji Dodoma kwa ajili ya maandalizi ya bajeti kwakutumia mfumo mpya wa PlanRep na FFARS. Akifungua mafunzo ya siku nane mkoani hapa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bibi Rehema Madenge, amesema moja ya vitu vilivyokuwa vikikwamisha masuala ya bajeti ni pamoja na kutokuwa na takwimu sahihi huku akinyooshea kidole takwimu za idara za elimu. “Ninatamani sana takwimu za elimu ziwe sahihi hasa katika uwasilishaji wa taarifa za mitihani ili ziweze kuendana na idadi ya wanafunzi na fedha zinazo o

JAJI MKUU, POLISI WATOA ONYO MGOMO WA MAWAIKILI NCHI NZIMA

Image
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma. Kaimu  Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Jeshi la Polisi nchini, wamelionya Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS), kutoingilia vyombo vya uchunguzi na upelelezi, vinavyochunguza tukio la mlipuko, uliotokea kwenye ofisi za Kampuni ya Mawakili ya IMMMA usiku wa kuamkia juzi jijini Dar es Salaam. Profesa Juma jana  alisema TLS hawana haki ya kutoa agizo kwa mawakili, kutohudhuria mahakamani na kwenye mabaraza mengine, kwa kuwa kila wakili ana mkataba binafsi na mteja wake. Profesa Juma alisema uhuru wa mahakama ni pamoja na kuheshimu mamlaka nyingine za nchi zinapokuwa zinafanya kazi zake.  Alisema kwa kuwa tukio la kulipuliwa kwa ofisi za Mawakili wa Immma ni tukio la kihalifu, hivyo wanasheria waiache Polisi na vyombo vingine vya upelelezi kufanya kazi yao. “Kama kutatokea wateja watakaolalamika kuwa mawakili wao hawakufika mahakamani siku ya Jumanne na Jumatano, hatua

RAIS MAGUFULI AFANYA ZIARA MAKAO MAKUU YA TAKUKURU

Image
Rais Maguduli akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Valentino Mlowola (Picha na Maktaba). Ulinzi umeimarishwa katika ofisi za makao makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) zilizoko Upanga, jijini Dar es Salaam huku ikielezwa kuwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatembelea ofisi hiyo. Saa 3:17  asubuhi yaleo  Agosti 28 , msafara wenye magari yapatayo 10 uliingia katika ofisi hiyo. Katika kuimarisha ulinzi, barabara zinazoingia kwenye ofisi hiyo nazo zimefungwa. Taarifa zaidi kuhusu alichokizungumza Rais alipotembelea TAKUKURU tutakujuza baadaye. Endelea kufuatilia habari zetu.