Man United Vs Liverpool, Salah Aundiwa Tume Manchester Utd
Kiungo mshambuliaji wa Liverpool, MoĀhamed Salah (kulia) Paul Labile Pogba. MANCHESTER United inatarajiwa kuwa mweĀnyeji wa Liverpool, keĀsho Jumamosi kwenye Uwanja wa Old Trafford, mchezo huo ni mkubwa na unasubiriĀwa kwa hamu. Kuelekea mtanange huo, gumzo kubwa ni juu ya uwezo wa kiungo mshambuliaji wa Liverpool, MoĀhamed Salah ambapo mashabiki wa UnitĀed wameanza kupata hofu kuhusu mchezaji ambaye atamzuia. Kawaida Salah amekuwa akipangwa kushambulia akitokea kulia, kwa aina ya ulinzi wa United beki wa kushoto amĀbaye atatakiwa kukutana naye ni Ashley Young au Luke Shaw, sasa hapo ndipo patamu, imeibuka hoja juu ya nani mweĀnye uwezo kati yao anayeweza kumficha Salah. Mchezo uliopita timu hizo zilipokuĀtanaa ulimalizika kwa suluhu, huku MarĀteo Darmian akipangwa kucheza beki wa kushoto, kwa sasa beki huyo siyo chaguo la kwanza la Kocha Jose MourĀinho. Kutokana na ubora wa Salah kufunĀga, mashabiki wa United kutoka mataifa mbalimbali wamepaza sauti wa...