Posts

Showing posts from December 19, 2013

ANGALIA PICHA EMMANUEL OKWI AWASILI DAR,APATA MAPOKEZI MAKUBWA

Image

RAIS JAKAYA KIKWETE AELEKEA NCHINI MAREKANI KUFANYIWA UCHUNGUZI WA AFYA YAKE.

Image
 Rais Jakaya Kikwete ----   THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA     DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini jioni ya jana, Jumatano, Desemba 18, 2013, kwenda Marekani kufanyiwa uchunguzi wa afya yake. Kwa mujibu wa ratiba ya shughuli za uchunguzi wa afya yake na kwa kutilia maanani siku za kusafiri kwenda Marekani na kurudi nchini, Rais Kikwete anatarajiwa kurejea nchini Alhamisi ya wiki ijayo, Desemba 26, 2013. Imetolewa na : Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu . Dar es Salaam . 19 Desemba, 2013

PICHAZ..AFANDE AACHA LINDO NA KWENDA KUSAKA BODABODA...!FUATILIA ZAIDI HAPA..

Image
Afande akiwa amemdhibiti dereva wa bodaboda. Wasamaria wema wakijaribu kumbembeleza afande. Afande akiwa amecharuka hataki kusikia cha mtu. Afande kakomaa. Afande aliyekuwa akilinda Benki ya NMB iliyopo Mtaa wa Samora karibu na Idara ya Habari 'Maelezo' jijini Dar, leo mchana aliacha lindo lake na kuanza kukamata bodaboda zilizokuwa zikivunja sheria za usalama barabarani kama anavyoonekana pichani akimdhibiti mwendesha bodaboda.

KAMA UKIMFANYIA MPENZI/MWENZI WAKO MAMBO HAYA KAMWE HAWEZI KUKUACHA KABISA

Image
Habari yako ndugu msomaji? Natumaini u mzima na mwenye afya njema. 1. KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye. 2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako. 3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali 4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasir

TAARIFA KUTOKA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA KUHUSU NDEGE ILIYOTUA KWA DHARURA KATIKA KIWANJA CHA ARUSHA

Image

RAY C ANATAFUTA BWANA .... HIVI HAPA VIGEZO VYAKE

Image
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ameibuka na kusema kuwa anahitaji mume anayemzidi umri kwa miaka kumi. Akizungumza hivi karibuni kwenye kituo kimoja maarufu cha runinga, Ray C alisema anahitaji mwanaume mtu mzima anayemzidi miaka kumi, anayejitambua na asiwe mwanamuziki kwani anaamini akiwa na mtu kama huyo uhusiano wao utakuwa mzuri kuliko ule wa awali uliokuwa wa machungu. “Ninamtaka mwanaume anayenizidi miaka kumi kwani kwa sasa nina miaka 31 japokuwa kwa sasa nafanya kazi kwanza ili nirudi kwenye levo yangu na nitakuwa juu zaidi ya zamani kwa sababu najitambua japokuwa nina hamu sana ya mtoto lakini yote namwachia Mungu. “Nashukuru sasa hivi niko vizuri nakumbuka  meneja wangu wa kwanza alinikataza nisiwe na uhusiano na mwanamuziki lakini ndiyo hivyo nikajikuta niko na Lord Eyes ambaye alianza kunichanganyia cha Arusha (bangi) bila mimi kujua na kujikuta ninaharibikiwa lakini nimeshamsamehe na ninamuombea heri katika maisha yake,” alisema R

BABY MADAHA AZIDI KUTAFUTA KIKI KUPITIA KWA DIAMOND

Image
Baby Joseph Madaha akipozi na Nasibu Abdul ‘Diamond’. MWIGIZAJI na mwanamuziki Bongo, Baby Joseph Madaha amemchana Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa kumwambia awatishie watoto wa Tandale kwani hana ubavu wa kuchuana naye. Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz'. Akizungumza na paparazi wetu, Baby alifunguka kuwa anamshangaa Diamond kujibu kuhusu jinsi alivyomchana wiki kadhaa zilizopita gazetini na kusema yeye hamuwezi kwani alimtangulia kuchomoka kistaa. “….akiwa bado ana-struggle kupata mkwanja awatishie watoto wenzake wa Tandale, mimi nishazindua brand yangu ya manukato na mikoba ya zawadi, bidhaa ambazo zinaingia sokoni rasmi Desemba 31, awatishe haohao watoto wenzake, mimi siyo saizi yake,” alisema Baby.  Baby Joseph Madaha. Diamond alipotafutwa, simu yake iliita bila kupokelewa.

BAADA YA KUMUUA, LULU AMSHUKURU KANUMBA

Image
Na Waandishi Wetu SURA ya mauzo katika sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ ametoa ya moyoni kuwa kama siyo kuwekwa nyuma ya nondo za Mahabusu ya Segerea, Dar basi yangemkuta mazito. Marehemu Steven Kanumba ‘The Great’. Lulu alikaa Gereza la Segerea kwa takribani miezi kumi baada ya kutokea kifo cha aliyekuwa mwandani wake, marehemu Steven Kanumba ‘The Great’ aliyefariki dunia Aprili 7, 2012. Nyota huyo wa Filamu ya Foolish Age alifunguka mambo ya kushangaza hivi karibuni juu ya tukio hilo kupitia Kipindi cha Take-One, kinachorushwa  na Clouds TV. TATIZO FOOLISH AGE Lulu alikuwa akizungumzia filamu yake hiyo ya Foolish Age ambapo alisema sinema hiyo inawasihi wasichana ambao wanapitia kipindi cha balehe ambacho ni hatari sana kwao. “Kwa kweli kipindi cha foolish age ni cha hatari sana, nilicheza filamu hiyo ili kuwaasa wasichana wenzangu. “Asikwambie mtu, mimi mwenyewe nilikokuwa nikielekea si kuzuri kabisa. KAMA SIYO KANUMBA “Ukweli ni kwamba

WATU WAWILI WANAODHANIWA NI MAJAMBAZI WAULIWA KWENYE KIJIJI CHA MANGA, MKOANI SINGIDA.

Image
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,SACP Geofrey Kamwela, akionyesha bunduki ya kijeshi aina ya SMG no.34555 iliyokuwa ikitumiwa na watu wawili wanaodhaniwa kuwa majamabazi katika kijiji cha Manga manispaa ya Singida. WATU wawili wakazi wa manispaa ya Singida ambao majina yao bado hayajajulikana,wakiwa kwenye Jokofu la kuhifadhia maiti baada ya kuuawa wakati wa majibishano ya risasi na polisi . JESHI  la Polisi mkoani Singida limewauwa watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wa kurushiana rasasi. Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida, SACP, Geofrey Kamwela amesema tukio hilo limetokea desemba tisa mwaka huu saa 12:00 jioni, huko katika kijiji cha Manga nje kidogo ya mji wa Singida. Amesema watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa na bunduki moja ya kijeshi aina ya SMG, walifika kijijini hapo kwa lengo la kufanya uhalifu. Kamanda Kamwela, amesema wat

CHENI APANIA KUMUAIBISHA RAY

Image
UAMUZI wa kujitosa kuwania nafasi ya uenyekiti wa kundi la mastaa la Bongo Muvi kwa mwigizaji Mahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’, umempa wakati mgumu mwenyekiti anayemaliza muda wake wa kuliongoza kundi hilo, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa hofu ya kuidondosha nafasi hiyo tamu. Mahsein Awadhi ‘Dk. Cheni’. Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa  wasanii wakubwa wa kundi hilo alisema tangu Dk. Cheni atangaze nia ya kuwania nafasi hiyo, Ray amekosa raha kutokana na ubora wa sera ambazo Dk. Cheni amekuwa akizinadi kwa wapiga kura. Vincent Kigosi ‘Ray’. “Ni kweli nagombea lakini si kwa ajili ya kumkomoa mtu, kiongozi atachaguliwa kwa kuchuja ubora wa sera zake, hayo wanayosema kuwa nitampindua kutokana na sera zangu, wana haki ya kusema,” alisema Dk. Cheni.

WOLPER, ZAMARADI NDANI YA BIFU ZITO

Image
Jacqueline Wolper. Na Shakoor Jongo STAA wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper amemrushia maneno ya lawama Mtangazaji wa Kipindi cha Take One, Zamaradi Mketema kuwa ni mnafki na adui yake mkubwa katika maisha. Zamaradi Mketema. Akizungumza na Amani juzikati, Wolper alisema amegundua kuwa mtangazaji huyo amekuwa akimfuatilia kwa karibu sana maisha yake kwa mtindo wa chanya (negative), akamuomba amuache. “Nilibadili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu, Zamaradi akanifuatilia, juzijuzi nimerudi kundini (kwenye Ukristo) kwa kusikiliza maneno ya wazazi wangu, akanifuatilia tena. “Huko nyuma kupitia kipindi chake alikubali nidhalilishwe na waigizaji wenzangu kwa faida yake (hakutaka kufafanua), iliniuma sana. Leo (hivi karibuni)  kaniweka hewani (kwenye redio) bila ya ridhaa yangu. Naomba niseme kuwa naanza kugundua azma yake kwangu ni nini, aniache na maisha yangu,” alilalama Wolper. Baada ya Wolper kulalamika sana, Amani lilimtafuta Zamaradi kwa njia ya simu y

PICHA ZA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU WAKIFANYA YAO ZAVUJA

Image
Baadhi ya madenti wa vyuo vikuu mbalimbali jijini Dar es Salaam, wameoza kwa matukio machafu ya ngono. Katika uchunguzi wa muda mrefu, Inaonyesha kuwa kuna kamtindo ka wanafunzi kufanya mapenzi ndani ya hostel zao huku wakijirekodi na kupiga picha chafu na za aibu na wengine hata kuuza miili yao ili kukidhi hali ngumu ya maisha iliyopo vyuoni Data zilizokamilika zilionesha kuwa wanafunzi hao waliojulikana kwa jina mojamoja ni Maya mwenye umri wa miaka 19, anayesoma katika chuo maarufu cha mahesabu, Raya anayebukua masomo ya Information Technology (IT) na mwingine ambaye jina lake na chuo anachosoma havikupatikana. Habari zilidai kuwa Raya na rafiki zake watatu wamekuwa wakijihusisha na vitendo haramu vya ngono rejareja na mwanaume mmoja wakiwa katika hosteli hiyo kwa kigezo cha mshiko ‘mnene’ wanaochuma kwa jamaa huyo. Hata hivyo, ripoti ya uchunguzi wetu haikufanikiwa kuwanasa wakimhudumia mwanaume huyo kwa mpigo, isipokuwa ilifuma picha ambazo kila

MANCHESTER UNITED WAICHAPA STOKE GOLI 2 SASA KUWAVAA SUNDERLAND

Image
Strike: Ashley Young (left) scored Manchester United's first goal against Stoke City Some Stoke players, it must be said, didn’t really want to go off.  They aren’t really like that in Staffordshire. Nevertheless it was hard to question Clattenburg’s decision, given that the elements were, at that time, making it rather difficult to see — and stand up, straight.  In fact the weather that battered the Britannia during the first half was pretty much the most exciting event of the opening 35 minutes.  With United fielding a strong team — an indication perhaps of Moyes desire to win a trophy of some description in his debut season at O ld Trafford — there was no reason why we shouldn’t have h ad an entertaining game against  opposition that have started to find their feet under Mark Hughes. Wayne Rooney — injured in training on Tuesday — may not have been present and fellow  stri