Posts

Showing posts from August 19, 2018

Uwoya awawashia moto wanaomsakama kuhusu Dogo Janja

Image
Mwanamama wa tasnia ya filamu za Kibongo, Irene Uwoya amejikuta akiwaka baada ya kuhojiwa sababu za kutomposti mumewe, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa zamani. Akizungumza na Risasi Jumamosi, Uwoya ambaye inadaiwa kuwa hayuko sawa na mumewe huyo alidai kuwa siyo lazima kila mara atamposti kwani ana mambo mengi ya kuandika na atafanya hivyo endapo tu imebidi. “Siyo kila mara nitakuwa natumia kurasa zangu kumposti Dogo, nina mambo mengine ya kufanya pia, itakapobidi kufanya hivyo nitafanya,” alisema Uwoya akionekana kuna jambo haliko sawa.  Uwoya alihojiwa hayo baada ya kila mara kuonekana akiposti picha za kuwa ndani ya ndege ambapo wapo waliosema kuwa kwa sasa amekuwa akisafiri na kumuacha mumewe huyo peke yake. “Siyo kweli, mimi sisafiri mara kwa mara, zile ni picha tu nimewahi kusafiri mara moja nilipokua nikienda Mwanza kwenye Miss Lake Zone,” alisema Uwoya

Uwoya awawashia moto wanaomsakama kuhusu Dogo Janja

Image
Mwanamama wa tasnia ya filamu za Kibongo, Irene Uwoya amejikuta akiwaka baada ya kuhojiwa sababu za kutomposti mumewe, Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’ kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa zamani. Akizungumza na Risasi Jumamosi, Uwoya ambaye inadaiwa kuwa hayuko sawa na mumewe huyo alidai kuwa siyo lazima kila mara atamposti kwani ana mambo mengi ya kuandika na atafanya hivyo endapo tu imebidi. “Siyo kila mara nitakuwa natumia kurasa zangu kumposti Dogo, nina mambo mengine ya kufanya pia, itakapobidi kufanya hivyo nitafanya,” alisema Uwoya akionekana kuna jambo haliko sawa.  Uwoya alihojiwa hayo baada ya kila mara kuonekana akiposti picha za kuwa ndani ya ndege ambapo wapo waliosema kuwa kwa sasa amekuwa akisafiri na kumuacha mumewe huyo peke yake. “Siyo kweli, mimi sisafiri mara kwa mara, zile ni picha tu nimewahi kusafiri mara moja nilipokua nikienda Mwanza kwenye Miss Lake Zone,” alisema Uwoya

JPM Apiga Marufuku Wamachinga Kunyanga’nya Bidhaa

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Njia panda ya Bugando mjini Mwanza wakati akiwa njiani kuelekea Chato mkoani Geita. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Sengerema mkoani Mwanza kuelekea Chato mkoani Geita. Rais Dkt. John Magufuli amewapiga marufuku viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza kuwanyang’anya bidhaa wafanyabiashara wadogo na badala yake amewaagiza viongozi wote nchini kujielekeza katika kutatua kero zinazowakabili wananchi. Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo Agosti 18, 2018 alipokuwa anasalimiana na wananchi waliokusanyika mjini Sengerema akiwa njiani kuelekea Chato Mkoani Geita kwa mapumziko, ambapo wananchi hao walidai halmashauri ya Wilaya hiyo imekuwa ikiwanyang’anya matunda aina ya nanasi wakulima na wafanyabiashara wanaouza matunda yao mjini hapo. “Nilishasema viongozi wote niliowateua mimi msishereheke