Posts

Showing posts from November 10, 2017

Shule iliyotokea mlipuko wa bomu yafungwa

Image
Uongozi wa  Shule ya Msingi  Kihinga umaamua kuifunga kwa muda shule hiyo kwa lengo la kuwajenga kisaikolojia wanafunzi wake baada ya wenzao kupoteza maisha kutokana na mlipuko wa bomu. Akizungumza  Mwananchi leo Novemba 10 ,Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Aidan Makobero amesema   shule hiyo imefungwa kimasomo hadi Jumatatu ili wanafunzi waweze kupata malezi ya  kisaikolojia Aidha amesema kwa shule jirani  ya Nyarukubala iliyo karibu na mpakani na  Burundi mahudhurio yamepungua kutoka wanafunzi 700  na kufikia 100  leo  Novemba 10 “Hata shule nyingine ya Nyarulama nayo wanafunzi wake wamepungua  baada ya tukio la shuleni kwangu na kusalia majumbani wakiogopa kwenda shule wakidai nao wanaweza kukumbwa na tukio  kama la shule jirani’’ amesema  Makobero Pia majeruhi 33 kati ya 42 waliojeruhiwa kwa bomu wameruhusiwa na kurejea makwao baada ya afya zao kuimarika Mganga wa hospitali ya misheni ya Rulenge Dk Mariagoleth Frederick amesema majeruhi hao  ni wanafunzi w

Polisi wamnasa muuza risasi za kivita

Image
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linawashikilia watu wawili kwa mahojiano baada ya kukamatwa na risasi za kivita ambazo wanazimiliki kinyume na sheria. Akitoa taarifa kwa Wanahabari Kamanda Mambosasa amesema kwamba Novemba 6 mwaka huu maeneo ya Serengeti Kigamboni lilipokea taarifa ya kuwepo kwa mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Willy Peter kuwa anafanya biashara ya kuuza risasi mtaani. Amesema kwamba baada ya kupata taarifa hizo Polisi walifanya ufuatiliaji na hatimaye kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na risasi 69 za kivita aina ya FN G3. Kamanda Mambosasa amefafanua kwamba baada ya  mahojiano mtuhumiwa huyo alikiri kuwa risasi hizo alipewa na mtu aliyemtaja kwa jina la Matabu William kwaajili ya kwenda kuziuza na kwamba alimpatia risasi hizo huko nyumbani kwake Kiwalani jijini Dar es salaam. Hata hivyo polisi walifika nyumbani kwa Matabu William Matoke (52) kiwalani ambapo alikiri kufanya biashara hiyo ya risasi na alipopekuliwa katika nyumb

Saada Mkuya amshukia Waziri wa fedha

Image
Waziri wa Fedha wa utawala uliopita wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Saada Mkuya amemshukia Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango kwa kuandaa mpango wa taifa wa maendeleo pasina kuihusisha Zanzibar. Mkuya ambaye ni mbunge wa Welezo visiwani Zanzibar amesema Dk Mpango amekuwa na kawaida ya kutokujibu hoja ambazo zinatolewa na wabunge wa kutoka Zanzibar jambo ambalo limemsikitisha. Akichangia leo Novemba 10 bungeni mjini Dodoma Mpango wa Maendeleo ya Taifa, Mkuya ambaye katika mchango wake alisikitishwa na jinsi Waziri Mpango anavyoitenga Zanzibar licha ya kuwa ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “Nadhani taifa hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaundwa na pande mbili sasa Mheshimiwa Mwenyekiti  (Azzan  Zungu) cha kusikitisha na fedheha kabisa ni kuona hakuna hata eneo moja lililopangiwa mpango angalau tu likaelekezwa katika upande mwingine wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema Mkuya “Hili niliseme wazi mheshimiwa mwenyekiti kupitia kwako

MSHTAKIWA SETHI AIOMBA MAHAKAMA IMRUHUSU KWENDA KUPATIWA MATIBABU YA PUTO LAKE NCHINI AFRIKA KUSINI

Image
Mshtakiwa Harbinder Singh Sethi,ameoimba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumruhusu kwenda kupatiwa matibabu ya puto lake lililoisha muda nchini Afrika Kusini kwa daktari wake maalumu kwa madai ya kwamba Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wamemueleza kuwa hawawezi kufanya upasuaji huo.Maombi hayo yamewasilishwa mahakamani hapo na wakili wake, Joseph Sungwa leo Novemba 10/2017 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, wakati shauri hilo linalomkabili Sethi na James Rugemarila lilipopelekwa kwa kutajwa na Mawakili wa Serikali, Vitalis Peter na Leonard Swai kudai upelelezi haujakamilika. Ili mshtakiwa aweze kuja mahakamani kuudhuria kesi yake na hatimae kuweza kujitetea, tunaomba kama inawezekana aende kumuona daktari wake ambaye anaishi Afrika Kusini kwa matibabu”, alidai Sungwa.Ombi hilo lilipingwa vikali na wakili wa serikali,Swai akidai Muhimbili haijashindwa kumfanyia upasuaji wa puto mshitakiwa huyo, bali anajicheleweshwa mwenyewe kutokana na kutaka uwep

HAMISA MOBETTO AANGUKIA PUA KESI YAKE,MAHAKAMA YAAMUA HAYA LIVE

Image
  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa Watoto imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na Mwanamitindo Hamisa Mobeto dhidi ya Mwanamuzi Naseb Abdull ‘Diamond Platnum’ kuhusu matunzo ya mtoto.Uamuzi huo umetolewa leo mbele ya Hakimu, Devotha Kisoka baada ya kusikiliza hoja za pande mbili ukiwemo wa Diamond ambaye aliwasilisha pingamizi dhidi ya kesi hiyo iliyofunguliwa na Mobeto. Katika uamuzi wake, Hakimu Kisoka alisema anakubaliana na hoja za upande wa mlalamikiwa kwamba kulikuwa na upungufu katika ufunguaji wa kesi hiyo.Kwa mujibu wa pingamizi lililowasilishwa na Diamond mahakama hapo, alidai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi. Hata hivyo, hoja hiyo ilipingwa na Mobeto kupitia jopo la mawakili wake. Mobeto alifungua kesi hiyo mahakamani hapo, pamoja na mambo mengine aliiomba mahakama imuamuru Diamond atoe matunzo ya mtoto waliozaa.Mobeto aliiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi ya Sh.mil 5 ambapo al

Kagasheki amvaa Kigwangalla

Image
Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamisi Kagasheki amemvaa Waziri wa sasa wa sasa wa wizara hiyo Mh. Hamisi Kigwangalla kwa kumtaja kuwa ana mahusiano ya karibu na Mkurugenzi wa OBC ambaye ana kashfa kubwa ya rushwa. Kupitia mtandao wake wa Twitter Balozi Kagasheki alimtaka Mh. Kigwangalla amthibitishie kuhusu ukaribu wake na Mkurugenzi huyo na kuhusu rushwa aliyowahi kupokea ikiwa ni pamoja na kuuza vitalu. Balozi ameandika "Waziri wa Maliasili na Utalii Hamisi Kigwangalla alinukuliwa kutaja "muwekezaji OBC" alivo na kashfa za Rushwa. Alinitaja mimi kuwa karibu na OBC. Napenda athibitishe ukaribu huo, vitalu nilivogawa nikiwa Waziri na rushwa niliyopokea," Balozi Kagasheki Hata hivyo baada ya ujumbe huo ambao ulienda moja kwa moja kwa Waziri Kigwangalla naye alijibu ujumbe huo ambao ulielekezwa kwake na kumuomba Mstaafu huyo wayazungumze nje ya mtandao "Mhe. Balozi Kagasheki , wewe ni kaka yangu na unajua nakuheshimu