Posts

Showing posts from September 12, 2017

BREAKING NEWZ: Mchekeshaji MC Pilipili amepata ajali

Image
Taarifa zilizoifikia muda huu kuhusiana na mchekeshaji MC Pilipili amepata ajali ya gari akiwa katikati ya  Nyasamba na Bubiki mkoani  Shinyanga . MC Pilipili amepata ajali akiwa kwenye garia aina ya Prado na kukimbizwa hospitali, kwa matukio na habari zaidi zinafuatilia kwa ukaribu ili kuweza kukuletea habaria kamili.

ANGALI PICHA WEMA SEPETU AKIWA MAHAKAMANI KWENYE KESI YAKE,SHAHIDI AFICHUA ALIPOIKUTA BANGI

Image
                    Wema Sepetu akitoka nje ya Mahakama ya Hakimu MKaziKisutu Dar. Wema na mama yake wakielekea kupanda gari. SHAHIDI upande wa serikali kesi ya Wema Sepetu kutuhumiwa kutumia madawa ya kulevya amesema msokoto wa bangi ulikutwa ukiwa kabatini jikoni kwake. Hayo yamesemwa na ofisa wa ofisi ya Mkuu wa Upelelezi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Inspekta Willy akimweleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula. Inspekta Willy anakumbuka Februari 4, mwaka huu aliitwa na mkuu wake wa kazi na kupewa jukumu la kufanya upekuzi nyumbani kwa              Wema Sepetu ambapo aliongozana na maofisa wenzake hadi nyumbani anakoishi huko Ununio jijini Dar es Salaam. Alisema baada ya kufika nyumbani kwa Wema walimkuta mfanyakazi wake wa ndani wa kike ambaye walimuomba waonane na mjumbe wa shina wa maeneo hayo ambapo baada ya kufanikwa kumwona walimweleza shida yao na kuanza kazi ya uchunguzi ili kutafuta dawa za kule

JPM Amjulia Hali Meja Jenerali Mstaafu Aliyejeruhiwa kwa Risasi

Image
Rais Magufuli akimjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini Lugalo. RAIS John  Magufuli leo Jumanne ametembelea Hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Lugalo, Jijini Dar es Salaam na kumjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini hapo baada ya kushambuliwa na watu wenye silaha wakati akiingia nyumbani kwake Ununio, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Rais Magufuli akisalimiana na mtoto. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imeeleza kuwa Mritaba alishambuliwa kwa risasi jana  mchana na kisha kupelekwa katika hospitali ya jeshi Lugalo kwa matibabu. Rais Magufuli akimjulia hali Meja Jenerali Mstaafu Vincent Mribata aliyelazwa hospitalini Lugalo. Mkuu wa kituo cha tiba cha hospitali hiyo na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Brigedia Jenerali Paul Massawe amemueleza Rais Magufuli kuwa Mritaba anaendelea vizuri baada ya madaktari kufanikiwa kutoa

Zitto Kabwe amjia juu Spika Job Ndugai

Image
Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Zitto Kabwe amefunguka na kumjia juu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai na kusema kuwa anamsikitika sana kama haoni jeshi heshima ya Bunge inavyoshuka. Zitto Kabwe amesema hayo leo kupitia mitandao yake ya kijamii baada ya Spika wa Bunge Job Ndugai kuagiza na kuwataka wabunge Zitto Kabwe pamoja na Saed Kubenea wa Ubungo kufika kwenye Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kutokana na kauli zao ambazo wamezitoa hivi karibuni. Kufuatia wito huo Zitto Kabwe amesema yeye atafika kwenye kamati hiyo ya maadili na Madaraka ya Bunge kama ambavyo Spika wa Bunge Job Ndugai ameagiza na kusema kuwa spika huyo kama angeweza kujua nguvu yake wala asingehaika na wabunge ambao wanakosoa kwa staha. "Spika Ndugai anajua ninavyomheshimu kama imefikia haoni heshima ya Bunge inavyoporomoka namsikitikia. Nitakwenda Kamati ya Maadili, Ndugai amekuwa Spika wa kwanza katika historia ya nchi yetu k

HAMISO MOBETTO AFUNGWA MDOMO,KISA KUZAA NA MSANII

Image
             Hamisa Mobetto. MAMA mzazi wa mwanamitindo maarufu Bongo, Hamisa Mobetto ambaye hivi karibuni alijifungua mtoto anayedaiwa kuzaa na msanii wa Bongo Flava, amecharuka akisema kuwa, japokuwa mtoto wake huyo anapigwa vijembe, lakini kamwe hawatamsikia akisema kwa sababu amemwambia afunge mdomo. Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mama Mobetto alisema kuwa, yeye kama mama anasikia uchungu kuona mwanaye huyo anavyosengenywa, lakini kwa busara amemtaka kutofungua mdomo kujibizana na mtu yeyote kuhusiana na ishu hiyo. Hamisa hatafungua mdomo kuzungumza chochote kuhusiana na mtoto wake na siyo mjinga kunyamaza, ila tu hatutaki malumbano na mtu,” alisema mama Mobetto.

Katibu Mkuu Chadema Ahojiwa Kuhusu ‘Watu Wasiojulikana’

Image
Dk Vincent Mashinji. KATIBU Mkuu wa Chadema , Dk Vincent Mashinji amesema polisi wamemhoji wakitaka kujua kuhusu kauli zake za watu wasiojulikana kama anaweza kuwatambua. “Watu wasiojulikana ambao tulikuwa tunawaongelea ni kwamba, imezoeleka kwa polisi kunapokuwa na tukio kubwa wanasema watu wasiojulikana, kwa hiyo lengo langu lilikuwa ni kuita wananchi  kurudi kwenye Polisi Jamii ili kuondokana na hili la watu wasiojulikana,” alisema Dk Mashinji. Katibu mkuu huyo wa Chadema, leo Jumatatu ameamua kwenda kuripoti Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini hapa. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Chadema, Tumaini Makene ilisema Dk Mashinji aliambatana na wasaidizi wake kutoka makao makuu ya chama hicho. “Katibu mkuu amewasili Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam, kuitikia wito wa Polisi uliotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, kuwa anatakiwa kufika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (

Breaking News: Watu Wasiojulikana Wavamia Ofisi za Wakili wa Manji

Image
Polisi wakiwa eneo la tukio. Ofisi ya mawakili ya Prime Attorneys imevamiwa usiku wa manane na watu wasiojulikana ambao wameiba kasiki lenye fedha na nyaraka. Mmoja wa mawakili katika ofisi hiyo,  Hudson Ndusyepo amesema ofisi yao imevunjwa na tayari ameenda polisi kutoa taarifa. Ndusyepo ambaye ni miongoni mwa mawakili wanaomtetea mfanyabiashara maarufu Yusuf Manji katika kesi ya uhujumu uchumi, amesema kabla ya wizi huo, waliohusika walimfunga mlinzi kwa kamba.   Milango ilivyovunjwa. Kampuni ya Prime Attorneys katika tovuti yake inaeleza ilianzishwa mwaka 2010. Ofisi za kampuni hiyo zipo Jengo la Prime House lililopo Mtaa wa Tambaza, Upanga jijini Dar es Salaam. Ofisi hizo zipo kwenye jengo la ghorofa tano lililopo jirani na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wilayani Ilala. Leo Asubuhi barabara ya kuingia eneo hilo ilifungwa kwa muda na polisi ambao walitumia magari yao kuziba njia na kuweka uzio wa  utepe wa rangi ya njano. Wakili

Vyakula Vinavyoliwa na Mgonjwa wa Vidonda Vya Tumbo

Image
LEO tutaangazia vyakula tiba kwa wagonjwa wa vidonda vya tumbo. Tutaangalia aina ya vyakula anavyopaswa kula au kuviepuka mgonjwa wa vidonda vya tumbo (Ulcers) ili kupata nafuu na kuishi bila kusumbuliwa nao. Ili kupunguza makali au kujiepusha kabisa na ugonjwa huo unapaswa kujiepusha kula vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi. Epuka ulaji wa vyakula vilivyopikwa na kuungwa viungo vingi vya aina mbalimbali, kama vile pilipili kali za aina zote na viungo vingine vyenye ladha ya ukali ambavyo hutiwa ndani ya mboga ama chakula ili kuongeza ladha. Pombe na kahawa au vinywaji vingine vyenye caffeine, vinaweza kuleta matatizo kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo na kwa mtu asiye navyo anaweza kupatwa na tatizo, hivyo ni vyema kuepuka au kutumia kwa kiasi kidogo vinywaji hivyo kwani huongeza asidi tumboni na hivyo vinaweza kusababisha vidonda au kuzidisha maumivu kwa anayeumwa. Kuna uhusiano kati ya ulaji chumvi na vidonda vya tumbo. Mgonjwa anashauriwa kuepuka ulaji wa