Posts

Showing posts from May 22, 2018

Binti Aliyedai Kutelekezwa na Lowassa Zengwe Jipya Laibuka!

Image
  U KISEMA unatafuta maisha usisahau kwamba kuna wakati nayo yanakutafuta ili mcheze ngoma moja; tuhuma za Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa kudaiwa kutelekeza mtoto zina funzo ndani yake. Siku chache baada ya msichana aitwaye Fatuma Lowassa kujitokeza ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kutoa madai ya kutelekezwa na Lowassa na hatimaye ishu hiyo ‘kupotelea hewani’, Uwazi limenasa zegwe jipya. “Kama ni kujitokeza na madai hayo ya kutelekezwa na Lowassa hii si mara ya kwanza kwa msichana huyo, sikumbuki ni lini lakini miaka ya nyuma aliwahi kufanya hivyo. “Mi nawaamini mkifanya uchunguzi wenu mtapata jambo hili, kuna watu wanayo video ya mahojiano ya msichana huyo pamoja na mama yake wakilalamika kutelekezwa. “Mimi nimejaribu kuipata nimeshindwa ila nasikia inaandaliwa itolewe ili kufufua upya tuhuma,” chanzo makini kililidokeza Uwazi na kulifanya lipange kikosi kazi kwa lengo la kufuatilia uwepo wa video hiyo .     Fatuma Lowassa  

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI AWATEMBELEA WANANCHI JAMII YA WAHADZABE NA WATATOGA KATA YA ESHKESH WILAYANI MBULU MKOA WA MANYARA

Image
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akizungumza na wananchi wa jamii za Wahdzabe Watatoga na Wasukuma wakati alipotembelea Kata ya Eshkesh  kijiji cha Dumanga Yaeda Chini wilayani Mbulu mkoa wa Manyara wakati alipozitembelea jamii hizo ili kuzungumza nao kuhusu maisha yao pamoja na uhifazi wa tamaduni na mila zao ambao unaweza kuwa Kivutio cha Utalii pia lakini pia kujua mahitaji yao ya muhimu katika maisha ya jamii hizo.   Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akizungumza na wananchi wa jamii za Wahdzabe Watatoga na Wasukuma wakati alipotembelea Kata ya Eshkesh  kijiji cha Dumanga kutoka kulia ni Gesso Bajuta diwani wa kata ya Endamilay wilayani Mbulu., Kaimu Mkurugenzi wa Utamaduzi Wizara ya habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi Beleko na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Bw. Hudson Kamoga.  Wananchi wa Eshkesh Jamii ya Watatoga wakiwa katika mkutano huo.

SHIDA YA UMEME KUSINI IMEKWISHA – MAJALIWA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Mradi wa Upanuzi wa Kituo cha Kufua Umeme kwa  Gesi Asilia Mtwara, Mei 21, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na  kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa.  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe wakati alipozindua Mradi wa Upanuzi wa Kituo  cha Kufua Umeme kwa Gesi Asilia Mtwara, Mei 21, 2018. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo litakalotumika kupakuwa mafuta kutoka  kwenye meli hadi kwenye matangi ya kuhifadhi mafuta katika bandari ya Mtwara, Mei 21, 2018. Majenereta mawili ya kuzalisha umeme yaliyonunuliwa serikali na kufungwa kwenye eneo la  TANESCO lenye mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi asilia katika Manispaa ya Mtwara ili  kupanua uzalishaji umeme wa gesi asilia Mtwara .  Majenereta hayo yalizinduliwa na  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mei 21, 2018 . WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema shida ya umeme iliyokuwa inaikabili mikoa ya Lindi na Mtwar

Polisi Waibua Balaa Ishu ya Wanawake Wenye Makalio Makubwa!

Image
D AR ES SALAAM: Huu mchezo wa baadhi ya wanaume kuona wanawake wenye makalio makubwa na kujifanya kurukwa na akili kwa kuwapigia miruzi, kujikohoza au kuzomeazomea umefikia mwisho. Jeshi la polisi na hasa Visiwani Zanzibar liko ‘siriazi’ na ishu hii ambapo hivi karibuni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Magharibi ‘RPC’, Hassan Nassir (pichani), alitoa tamko ambalo limeibua balaa mitaani. SIKIA TAMKO LA RPC Hebu kabla ya kuelezea balaa lilolopo kuhusu tamko hilo ni bora kujipa muda wa kumsikiliza RPC Nassir kile alichosema alipozungumza katika semina ya kulinda utu wa mwanamke na mtoto iliyofanyika hivi karibuni mkoani humo. “Naomba wananchi wajue mwanamke kupita pengine maumbile yake yamejazajaza ukaanza kukohoa, mmh, mmmh, hilo ni shambulio la aibu tutakukamata tukupeleke mahakamani. “Maana wengine wanafikiri ni mchezo tu ina maana mama zetu, dada zetu, watoto wetu wenye maumbile makubwa wasitembee mitaani; maana wakitembea watu wanaanza kukohoa mmh, kama una kihozi nen

IGP Simon Sirro Akutana na Rais wa TLS

Image
MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Fatma Karume aliyefika makao makuu ya Jeshi la Polisi kwa lengo la kujitambulisha tangu alipochaguliwa kuongoza chama hicho ambapo pia walijadiliana masuala kadhaa ya kisheria. MKUU wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro (kushoto) akiongea na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Fatma Karume aliyefika  makao makuu ya Jeshi la Polisi. Mazunguzo yakiendelea.

Tende, Maji Zinavyofaa Wakati wa Mfungo wa Ramadhani

Image
V YAKULA vinavyofaa kuliwa wakati huu wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni vingi, leo tutaanza kuchambua kimoja baada ya kingine, Mbali na Waislamu, uchambuzi huu unawafaa pia wale ambao siyo Waislamu. Chakula kilichozoeleka zaidi kwa futari ni tende. Baada ya kushinda kutwa nzima na Swaumu, kiwango cha sukari ya mwili hupungua na hivyo, kuhitaji kujazilizwa tena. Aina ya kwanza ya sukari itumikayo mwilini na hasahasa ubongoni ni glukosi. Mshuko wa sukari walioupata wale ambao hawakula au kunywa kwa kipindi kirefu, unaweza kusababisha ulegevu wa mwili. Pindi sukari inapoliwa kwa njia ya chakula au kinywaji, viwango vya glukosi ya mwili hujisawazisha vyenyewe na kumfanya mtu aliyefunga asijihisi kuchoka sana na huwa na nuru zaidi ya macho. Ingawaje tende, mara nyingi, si chakula kinachopendelewa sana na watu wenye njaa, lakini ndicho chakula kisicho na mafuta, na ni chanzo madhubuti cha sukari. Nusu ya sukari zitolewazo na tende ni kwa ajili ya glukosi pek

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI,SANAA UTAMADUNI NA MICHEZOAMTEMBELEA MWANARIADHA ANAYEHESHIMIKA DUNIANI MZEE JOHN STEVEN AKHWARI NYUMBANI KWAKE MBULU MKOANI MANYARA

Image
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Suzan Mlawi akisalimiana na Mzee John Steven Akhwari  Mwanariadha anayeheshimika Duniani mara baada kwasili alipomtembelea nyumbani kwake Eneo la Sani mjini Mbulu  mkoani Manyara jana, John Steven Akhwari aliiwakilisha nchi katika michezo ya Olimpiki iliyofanyika Mexco  City mwaka 1968 John Steven Akwari aliyekuwa wa mwisho kumaliza mashindano ya marathon mwaka 1968 Mexico City katika mioyo ya mamilioni ya watu anakumbukwa kama shujaa ambapo mwaka 2008 katika mashindano ya Olimpiki ya Beijing nchini China miaka 40 baadaye, Akhwari aliteuliwa kuwa balozi wa heshima wa Olimpiki. Katika mashindano hayo ya mwaka 1968, Akwari akiwa na umri wa miaka 30 akiiwakilisha Tanzania alikuwa mwanariadha wa mwisho (57) kumaliza mashindano kati ya 75 walioanza.   Mshindi wa mashindano hayo Mamo Wolde wa Ethiopia alitumia saa 2:20:26 huku Akhwari akimaliza zaidi ya saa moja baadaye yaani alitumia