Posts

Showing posts from February 9, 2018

Chanzo Cha Maumivu Ya Tumbo Mara Kwa Mara!

Image
Maumivu ya tumbo. MAUMIVU ya tumbo ni tatizo linaloweza kumpata mtu yeyote, mwanamke au mwanaume, mkubwa au mdogo. Maumivu haya husumbua kwani huwa hayaishi, yaani yanatulia kwa muda flani na kurudi tena, aina hii ya maumivu pia inaweza kuwa ya moja kwa moja, yaani hayatulii na wakati mwingine mgonjwa hupata nafuu kwa kujikunja au kushikilia tumbo. Maumivu yanaweza kuwa upande wa juu wa tumbo au upande wa chini na yanatulia kwa vipindi na kurudi yakiwa makali au madogo lakini hayaishi. JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA Kama tulivyoona, humtokea yeyote mwanamke au mwanaume, utokeaji wake hutofautiana kwa jinsi. Kwa mwanaume vyanzo vya maumivu haya vinaweza kuwa hernia au ngiri au matatizo kwenye korodani, lakini kwa wote vyanzo vinaweza kuwa vidonda vya tumbo, matatizo ya mkojo, kidole tumbo, matatizo ya utumbo mkubwa, kukosa au kufunga kupata haja kubwa, gesi kujaa tumboni. Yapo mengine kama kuwa na mawe kwenye mfumo wa mkojo au kifuko cha nyongo, matatizo ya ini na mengi

Professor Jay;Sugu kaniambia niwaambie msiogope endeleeni kupaza sauti

Image
Baada ya Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule (Professor Jay) kwenda Mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili Mbunge wa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu), Mbunge huyo amesema kuwa Sugu amesema kuwa wasiogope waendelee kupaza sauti. Professor Jay amesema kuwa kesi hiyo itaendelea kusikilizwa leo ambapo RCO na RPC wa Mbeya watasimama kutoa ushahidi wao. “SUGU kaniambia niwaambie ‘MSIOGOPE’ bali endeleeni kupaza Sauti!!Kesi yao inaendelea leo saa Tatu asubuhi hii katika mahakama kuu ya Mbeya, ambapo RCO na RPC wa Mbeya watasimama kutoa ushahidi wao LEO,” ameandika Proffesor Jay kwenye ukurasa wake wa Insta. Sugu anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya uchochezi dhidi ya Rais Magufuli. Ambayo wanadaiwa kuitoa Disemba 30 kwenye mkutano wa hadahara uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mwenge.

PUTIN ASEMA: SIJAWAHI KUWA NA ‘SMARTPHONE’

Image
Rais wa Russia, Vladimir Putin (kulia) aliyekiri hana simu ya kisasa (smartphone). Kiongozi huyo aliyewahi kuongoza pia shirika la ujasusi la Urusi ya Kisoviet (KGB) amesema huwatumia wasaidizi wake kumtafutia habari anazotaka. “SINA simu ya smartphone,” ndivyo ambavyo husema Rais wa Russia, Vladimir Putin, kila anapoulizwa iwapo ana simu hizo za kisasa. Licha ya kuambiwa kwamba “kila mtu ana smartphone mfukoni”  huko Siberia, nchini Russia, wakati akiwa ziarani, kiongozi huyo pia aliwahi kusema kwamba hataki kutumia tovuti (website) na aliwahi kukiri kwamba mtandao wa Internet ni kimradi cha shirika la ujasusi la Marekani – CIA – na kwamba nusu ya kazi yake ni kuonyesha ngono. Pamoja na kwamba watu wengi nchini mwake, wakiwemo wanafunzi,  huchakarika ili kupata aina hizo za simu, Putin amefichua kwamba analitawala taifa hilo la watu milioni 144 bila kutumia smartphone. Akiwa amekiri pia kwamba hapendi mambo ya technolojia mpya, amesema kamwe huwa hatumi

Wema apigwa mamilioni ya pesa

Image
Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu. Wiki moja baada ya akaunti ya Mtandao wa Kijamii wa Instagram ya Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu kudukuliwa na wajanja wa mjini, mrembo huyo anadaiwa kupigwa mamilioni. Habari zilizolifikia dawati la gazeti hili zilieleza kuwa, tangu mrembo huyo adukuliwe akaunti yake hiyo yenye wafuasi zaidi ya milioni tatu, wajanja hao wamekuwa wakiitumia ndivyo sivyo kwa kuposti matangazo mbalimbali ya kibiashara ambapo wanachukua pesa bila ya Wema kujua. Inaelezwa kuwa, Wema alikuwa akitumia akaunti hiyo kupitia namba ya simu ya mtandao maarufu wa mawasiliano nchini ambapo wadukuzi walifanikiwa kumiliki namba hiyo ambayo hutumia moja kwa moja kuwasiliana na wafanyabiashara mbalimbali wa mtandao kwa mgongo wa Wema na kuvuna pesa. Wajanja hao, kwa siku moja tu hutumia akaunti hiyo kuvuna zaidi ya laki saba ambapo kwa wastani wa tangazo moja huchukua kiasi cha shilingi elfu hamsini hadi laki moja. WATAALAMU WANASEMAJE?

Chanzo Cha Maumivu Ya Tumbo Mara Kwa Mara!

Image
Maumivu ya tumbo. MAUMIVU ya tumbo ni tatizo linaloweza kumpata mtu yeyote, mwanamke au mwanaume, mkubwa au mdogo. Maumivu haya husumbua kwani huwa hayaishi, yaani yanatulia kwa muda flani na kurudi tena, aina hii ya maumivu pia inaweza kuwa ya moja kwa moja, yaani hayatulii na wakati mwingine mgonjwa hupata nafuu kwa kujikunja au kushikilia tumbo. Maumivu yanaweza kuwa upande wa juu wa tumbo au upande wa chini na yanatulia kwa vipindi na kurudi yakiwa makali au madogo lakini hayaishi. JINSI TATIZO LINAVYOTOKEA Kama tulivyoona, humtokea yeyote mwanamke au mwanaume, utokeaji wake hutofautiana kwa jinsi. Kwa mwanaume vyanzo vya maumivu haya vinaweza kuwa hernia au ngiri au matatizo kwenye korodani, lakini kwa wote vyanzo vinaweza kuwa vidonda vya tumbo, matatizo ya mkojo, kidole tumbo, matatizo ya utumbo mkubwa, kukosa au kufunga kupata haja kubwa, gesi kujaa tumboni. Yapo mengine kama kuwa na mawe kwenye mfumo wa mkojo au kifuko cha nyongo, matatizo ya ini na m

MWANAUME AOA WANAWAKE SITA KWA KULIPWA,SABABU Z A TUKIO HILO HIZI HAPA

Image
mmoja wa Marekani katika Jimbo la Massachusetts ameshtakiwa Mahakamani kwa hati ya makosa ya jinai baada ya kuoa wanawake wengi katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2013.   Mtuhumiwa huyu Peter Hicks, 57, alifanya vitendo hivi huku akilipwa kwa lengo la kuwasaidia wanawake hao kukwepa hatua za kupata nyaraka zote za kuwatambua kama wahamiaji wa nchi hiyo. Inaelezwa kuwa Hicks alioa wanawake 6 katika kipindi hicho chote. Wanawake hao wanaripotiwa kutoka katika nchi za Kusini mwa Afrika na alikuwa tayari ameshaomba haki zote wanazotakiwa kupewa wahamiaji wanne kati yao

MZEE MAJUTO: Niombeeni Jamani, Tezi Dume Si Mchezo!

Image
Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ MKONGWE wa filamu za Kibongo aliye kipenzi cha wengi, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ambaye kwa sasa ni mgonjwa ametoa ya moyoni kuwa bado anaumwa hivyo kuwaomba wasanii wenzake na Watanzania kumuombea. Akizungumza na Star Mix, Mzee Majuto alisema Februari 11, mwaka huu anatarajia kurudi tena katika Hospitali ya Tumaini, Dar alikokuwa amelazwa awali na kuruhusiwa baada ya daktari wake kufiwa ambapo ndiyo ataenda kufanyiwa upasuaji wa ugonjwa wa tezi dume unaomsumbua.   “Niliruhusiwa Jumamosi iliyopita lakini bado naumwa, tezi dume si mchezo, ninachoweza kuwaambia wasanii wenzangu na Watanzania kwa jumla, waniombee tu,” alisema Mzee Majuto

Hivi Ndivyo Vitu Hatari Vinavyoweza Kuharibu Na Kuvunja Ndoa Ya Wapendanao Katika Familia

Image
WAPENZI wanagombana, ndoa zinavunjika na familia nyingi zipo kwenye msoto kwa sababu ya ubinafsi. Tunazungumza mengi lakini ukweli ni kwamba endapo kila mmoja atafanikiwa kuushinda ubinafasi, upendo utashamiri kila kona. Ubinafsi una matawi mengi. Mtu anaposaliti, maana yake ametekwa na tamaa binafsi. Anashindwa kutambua kwamba yeye ni mpenzi wa mtu, kwa hiyo anatakiwa kulinda penzi la mwenzake. Hajui kama anachokifanya ni dhuluma ya hali ya juu. Ukweli ni kwamba unapoanzisha uhusiano na mtu, maana yake umeamua kumchagua yeye ndiye amiliki penzi lako. Kwa hiyo ukienda kulitoa kwa mwingine, huo ni ubinafsi. Umeingiwa na umimi kwa kuona kwamba unatoa rasilimali za ndani ya mwili wako mwenyewe. Kwa nini ukimfumania mwenzi wako panachimbika? Ni kwa sababu alichokitoa kwa mtu mwingine ni chako, kwa maana hiyo amekutendea dhuluma. Ndiyo maana ukawa na jeuri ya kupigana kwa sababu haki yako imetumika ndivyo sivyo. Hivyo basi, usaliti ni ubinafsi. Umei

Rose Ndauka: Natamani Kuongeza Mtoto Mwingine

Image
Rose Ndauka MUIGIZAJI mwenye mikogo Bongo Muvi, Rose Ndauka amefunguka kuwa anatamani sana kuongeza mtoto mwingine kutokana na raha anayoipata kutoka kwa mtoto wake huyo wa kike aitwaye Naveen lakini bado hajapata wa kuongeza naye. Akizungumza na Star Mix, Rose alisema kuwa, mtoto wake amekuwa akimpa faraja sana kila wakati hivyo kumpa hamu tena ya kuongeza mtoto mwingine ili azidishe furaha aliyonayo sasa. “Kwa kweli nisiwe muongo, natamani sana kuongeza mtoto mwingine maana nishaona ndiyo faraja yangu ila tatizo ni mwanaume wa kuzaa naye sijampata, hata hivyo Mungu ni mwema naamini atapatikana tu,” alisema Rose.